Ezekieli 33:1-33

  • Majukumu ya mlinzi (1-20)

  • Habari kuhusu kuanguka kwa Yerusalemu (21, 22)

  • Ujumbe kwa wakaaji wa magofu ya Yerusalemu (23-29)

  • Watu wapuuza ujumbe (30-33)

    • Ezekieli “kama wimbo wa mapenzi” (32)

    • “Nabii alikuwa miongoni mwao” (33)

33  Na neno la Yehova likanijia likisema:  “Mwana wa binadamu, zungumza na wana wa watu wako,+ uwaambie, “‘Ikiwa nitaleta upanga uishambulie nchi,+ na watu wote wa nchi hiyo wamchukue mtu fulani na kumfanya awe mlinzi wao,  naye aone upanga ukija kuishambulia nchi, kisha apige pembe na kuwaonya watu,+  ikiwa mtu atasikia sauti ya pembe lakini asitii onyo,+ nao upanga uje na kumuua,* damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.+  Aliisikia sauti ya pembe, lakini hakutii onyo. Damu yake itakuwa juu yake mwenyewe. Kama angetii onyo, angeokoa uhai wake.*  “‘Lakini mlinzi akiuona upanga ukija naye asipige pembe+ na watu wasipate onyo nao upanga uje na kumuua mmoja wao, mtu huyo atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe, lakini nitaidai damu yake kutoka kwa mlinzi.’*+  “Na wewe, mwana wa binadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa watu wa nyumba ya Israeli; unaposikia neno kutoka katika kinywa changu lazima uwape onyo langu.+  Ninapomwambia mtu mwovu, ‘Wewe mwovu, hakika utakufa!’+ lakini wewe humwonyi waziwazi mtu huyo mwovu ili abadili njia yake, yeye kwa kuwa ni mwovu atakufa kwa sababu ya kosa lake mwenyewe,+ lakini damu yake nitaidai kutoka kwako.  Lakini ukimwonya mtu mwovu aiache njia yake naye akatae kubadili njia yake, atakufa kwa sababu ya kosa lake,+ lakini wewe kwa hakika utauokoa uhai wako.*+ 10  “Na wewe, mwana wa binadamu, waambie hivi watu wa nyumba ya Israeli: ‘Ninyi mmesema hivi: “Maasi yetu na dhambi zetu zinatulemea sana na kutufanya tudhoofike;+ basi tunawezaje kuendelea kuishi?”’+ 11  Waambie, ‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “Mimi sifurahishwi na kifo cha mwovu,+ bali kwamba mtu mwovu abadili njia yake+ na kuendelea kuishi.+ Geukeni, geukeni mziache njia zenu mbaya,+ kwa nini mfe, enyi watu wa nyumba ya Israeli?”’+ 12  “Na wewe, mwana wa binadamu, waambie wana wa watu wako, ‘Uadilifu wa mtu mwadilifu hautamwokoa akiasi;+ wala uovu wa mwovu hautamkwaza akiacha uovu wake;+ wala hakuna mtu yeyote mwadilifu atakayeendelea kuishi kwa sababu ya uadilifu wake siku atakayotenda dhambi.+ 13  Ninapomwambia mtu mwadilifu: “Hakika utaendelea kuishi,” naye autumaini uadilifu wake mwenyewe na kutenda kosa,*+ hakuna tendo lolote la uadilifu alilotenda litakalokumbukwa, lakini atakufa kwa sababu ya kosa alilotenda.+ 14  “‘Ninapomwambia mtu mwovu: “Hakika utakufa,” naye aiache dhambi yake na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu,+ 15  na mtu huyo mwovu arudishe kitu kilichowekwa rehani+ na kulipa vitu alivyomnyang’anya mwingine,+ naye atembee katika sheria za uzima kwa kutotenda kosa, hakika ataendelea kuishi.+ Hatakufa. 16  Hataadhibiwa kwa sababu ya dhambi yoyote aliyotenda.*+ Kwa hakika ataendelea kuishi kwa sababu ya kutenda mambo ya haki na ya uadilifu.’+ 17  “Lakini watu wako wamesema, ‘Njia ya Yehova si ya haki,’ ingawa kwa kweli ni njia yao isiyo ya haki. 18  “Mtu mwadilifu akiacha uadilifu wake na kutenda kosa, lazima afe kwa sababu ya kosa hilo.+ 19  Lakini mtu mwovu akiacha uovu wake na kutenda mambo ya haki na ya uadilifu, ataendelea kuishi kwa sababu ya kufanya hivyo.+ 20  “Lakini ninyi mnasema, ‘Njia ya Yehova si ya haki.’+ Nitamhukumu kila mmoja wenu kulingana na njia zake, enyi watu wa nyumba ya Israeli.” 21  Mwishowe katika mwaka wa 12, mwezi wa kumi, siku ya tano ya mwezi wa uhamisho wetu, mtu aliyetoroka Yerusalemu alinijia+ na kusema: “Jiji limeangamizwa!”+ 22  Basi, jioni ya siku iliyokuwa imetangulia kabla ya mtu huyo aliyetoroka kuja, mkono wa Yehova ulinijia naye akakifungua kinywa changu kabla ya mtu huyo kunijia asubuhi. Kinywa changu kilifunguliwa, nami sikuwa bubu tena.+ 23  Kisha neno la Yehova likanijia likisema: 24  “Mwana wa binadamu, wakaaji wa magofu+ haya wanasema hivi kuhusu nchi ya Israeli: ‘Abrahamu alikuwa mtu mmoja tu, hata hivyo aliimiliki nchi hii.+ Lakini sisi ni wengi; kwa hakika tumepewa nchi hii iwe mali yetu.’ 25  “Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Mnakula chakula pamoja na damu,+ nanyi mnayainua macho yenu kwa sanamu zenu zinazochukiza* na kuendelea kumwaga damu.+ Basi kwa nini mwimiliki nchi hii? 26  Mmeutegemea upanga wenu.+ Mmetenda mambo yanayochukiza, na kila mmoja wenu amemchafua mke wa jirani yake.+ Basi kwa nini mwimiliki nchi hii?”’+ 27  “Unapaswa kuwaambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Kwa hakika kama ninavyoishi, wale wanaoishi katika magofu watauawa kwa upanga; na wale walio uwanjani nitawafanya wawe chakula cha wanyama wa mwituni; na wale walio katika ngome na mapango watakufa kwa ugonjwa.+ 28  Nitaifanya nchi iwe mahame na ukiwa kabisa,+ na kiburi chake chenye majivuno kitakomeshwa, na milima ya Israeli itafanywa ukiwa,+ na hakuna yeyote atakayepitia humo. 29  Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoifanya nchi iwe mahame na ukiwa kabisa+ kwa sababu ya mambo yote yanayochukiza ambayo wamefanya.”’+ 30  “Na wewe, mwana wa binadamu, watu wako wanaongea kukuhusu kando ya kuta na kwenye vizingiti vya milango ya nyumba.+ Kila mtu anamwambia ndugu yake, ‘Hebu njoo tusikie neno linalotoka kwa Yehova.’ 31  Watakusanyika na kuketi mbele yako kama watu wangu; nao watasikia maneno yako lakini hawatayatenda.+ Kwa maana wanakusifusifu kwa vinywa vyao* lakini moyo wao una pupa ya kupata faida isiyo ya haki. 32  Tazama! Kwao, wewe ni kama wimbo wa mapenzi, unaoimbwa kwa sauti tamu na kuchezwa kwa ustadi kwa kinanda. Watasikia maneno yako, lakini hakuna yeyote atakayeyatenda. 33  Na yatakapotimia—kwa maana yatatimia—watalazimika kujua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kumwondoa.”
Au “nafsi yake.”
Au “nitamfanya mlinzi awajibike kwa sababu ya damu ya mtu huyo.”
Au “utaiokoa nafsi yako.”
Au “kutenda jambo lisilo la haki.”
Tnn., “Hakuna dhambi yoyote aliyotenda itakayokumbukwa.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “wanazungumza kwa tamaa sana.”