Ezekieli 42:1-20

  • Majengo ya vyumba vya kulia chakula (1-14)

  • Pande nne za hekalu zapimwa (15-20)

42  Kisha akanipeleka kwenye ua wa nje kuelekea kaskazini.+ Naye akanileta kwenye jengo lenye vyumba vya kulia chakula lililopakana na eneo lililo wazi,+ upande wa kaskazini wa jengo linalofuata.+  Urefu wake katika mlango wa kaskazini ulikuwa mikono 100,* na upana wake mikono 50.  Lilikuwa kati ya ua wa ndani, ambao ulikuwa na upana wa mikono 20,+ na sakafu ya ua wa nje. Mabaraza yake yalitazamana na yalikuwa na urefu wa ghorofa tatu.  Mbele ya vyumba vya kulia chakula* kulikuwa na njia ya ndani+ yenye upana wa mikono 10 na urefu wa mikono 100,* na milango yake ilitazama kaskazini.  Vyumba vya kulia chakula vilivyokuwa juu katika jengo hilo vilikuwa vyembamba kuliko vile vya chini na vya katikati, kwa sababu mabaraza yalichukua nafasi kubwa ya vyumba hivyo.  Kwa maana mabaraza yalikuwa na urefu wa ghorofa tatu, lakini hayakuwa na nguzo kama nguzo za nyua. Ndiyo sababu nafasi kubwa zaidi ya vyumba vilivyokuwa juu ilichukuliwa na mabaraza kuliko katika ghorofa ya chini na ya katikati.  Ukuta wa nje wa mawe uliokuwa karibu na vyumba vya kulia chakula kuelekea ua wa nje uliotazama vile vyumba vingine vya kulia chakula ulikuwa na urefu wa mikono 50.  Kwa maana urefu wa vyumba vya kulia chakula vilivyotazama ua wa nje ulikuwa mikono 50, lakini vile vilivyotazama patakatifu vilikuwa na urefu wa mikono 100.  Kulikuwa na njia iliyoelekea kwenye vyumba vya kulia chakula upande wa mashariki kutoka kwenye ua wa nje. 10  Kulikuwa pia na vyumba vya kulia chakula katika* ukuta wa mawe wa ua upande wa mashariki, karibu na eneo lililo wazi na pia jengo.+ 11  Mbele ya vyumba hivyo kulikuwa na njia kama ile ya vyumba vya kulia chakula vya kaskazini.+ Vyumba hivyo vilikuwa na urefu na upana uleule, na milango yake ya kutokea na ramani yake ililingana na ya vyumba vya kaskazini vya kulia chakula. Milango yake 12  ilikuwa kama milango ya vyumba vya kusini vya kulia chakula. Kulikuwa na mlango mahali ambapo njia ilianzia, kabla ya ukuta wa mawe uliokuwa upande wa mashariki, mahali ambapo mtu angeweza kuingilia.+ 13  Kisha akaniambia: “Vyumba vya kulia chakula vya kaskazini na vyumba vya kulia chakula vya kusini vinavyopakana na eneo lililo wazi+ ndivyo vyumba vya kulia chakula vilivyo vitakatifu ambamo makuhani wanaomkaribia Yehova hula matoleo matakatifu zaidi.+ Matoleo matakatifu zaidi, toleo la nafaka, dhabihu ya dhambi, na dhabihu ya hatia huwekwa humo, kwa sababu mahali hapo ni patakatifu.+ 14  Makuhani wanapoingia, hawapaswi kutoka mahali patakatifu na kwenda kwenye ua wa nje kabla hawajavua mavazi wanayovaa wanapohudumu,+ kwa sababu ni matakatifu. Watavaa mavazi mengine ili waende katika maeneo ambayo watu wanaruhusiwa kuingia.” 15  Alipomaliza kupima sehemu ya ndani ya hekalu,* akanipeleka nje kupitia lango linalotazama mashariki,+ naye akapima eneo hilo lote. 16  Akapima upande wa mashariki kwa ule utete wa kupimia.* Ulikuwa na urefu wa tete 500 kutoka upande mmoja hadi mwingine, kulingana na utete wa kupimia. 17  Akapima upande wa kaskazini, nao ulikuwa na urefu wa tete 500, kulingana na utete wa kupimia. 18  Akapima upande wa kusini, nao ulikuwa na urefu wa tete 500, kulingana na utete wa kupimia. 19  Akazunguka upande wa magharibi. Akapima urefu wa tete 500 kwa utete wa kupimia. 20  Akapima pande nne za eneo hilo. Lilikuwa na ukuta uliolizunguka pande zote+ uliokuwa na urefu wa tete 500 na upana wa tete 500,+ ili kutenganisha kitu kitakatifu na kitu cha matumizi ya kawaida.+

Maelezo ya Chini

Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Au “vile vyumba.”
Kulingana na Septuajinti ya Kigiriki ni “urefu wa mikono 100.” Maandishi ya Kiebrania yanasema hivi: “Njia ya mkono mmoja.” Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “katika upana wa.”
Tnn., “nyumba ya ndani.”