Ezekieli 43:1-27

  • Utukufu wa Yehova wajaa hekaluni (1-12)

  • Madhabahu (13-27)

43  Kisha akanipeleka kwenye lango linalotazama mashariki.+  Hapo nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka mashariki,+ na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji yenye kishindo;+ nayo dunia iling’aa kwa utukufu wake.+  Mambo niliyoona yalikuwa kama maono niliyoona nilipokuja* kuliangamiza jiji, na yalionekana kama mambo niliyoona karibu na mto Kebari;+ nami nikaanguka kifudifudi.  Kisha utukufu wa Yehova ukaingia hekaluni* kupitia lango lililotazama mashariki.+  Ndipo roho ikaniinua na kuniingiza kwenye ua wa ndani, nami nikaona kwamba hekalu lilikuwa limejaa utukufu wa Yehova.+  Kisha nikasikia mtu akizungumza nami kutoka katika lile hekalu, na mtu huyo akaja na kusimama kando yangu.+  Akaniambia: “Mwana wa binadamu, hapa ndipo mahali pa kiti changu cha ufalme+ na mahali pa nyayo za miguu yangu,+ ambapo nitakaa kati ya watu wa Israeli milele.+ Watu wa nyumba ya Israeli hawatalichafua tena jina langu takatifu,+ wao na wafalme wao, kwa ukahaba wao wa kiroho na kwa maiti za wafalme wao wanapokufa.  Kwa kuweka kizingiti chao kando ya kizingiti changu na mwimo wa mlango wao kando ya mwimo wa mlango wangu, kukiwa na ukuta tu kati yangu nao,+ walilichafua jina langu takatifu kwa mambo yanayochukiza waliyotenda hivi kwamba nikawaangamiza kabisa kwa hasira yangu.+  Basi sasa na wauweke mbali nami ukahaba wao wa kiroho na maiti za wafalme wao, nami nitakaa miongoni mwao milele.+ 10  “Na wewe, mwana wa binadamu, waeleze watu wa nyumba ya Israeli kuhusu hekalu+ ili waaibike kwa sababu ya makosa yao,+ nao wanapaswa kuichunguza ramani yake.* 11  Ikiwa wataaibika kwa sababu ya mambo yote ambayo wamefanya, unapaswa kuwaonyesha ramani ya hekalu, mpangilio wake, na njia zake za kutokea, na za kuingilia.+ Waonyeshe ramani zake zote na maagizo yake, ramani zake na sheria zake, nawe uziandike mbele ya macho yao, ili waone ramani zake zote na kufuata maagizo yake.+ 12  Hii ndiyo sheria ya hekalu. Eneo lote kuzunguka juu ya mlima ni takatifu zaidi.+ Tazama! Hii ndiyo sheria ya hekalu. 13  “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa kipimo cha mikono+ (kila mkono uliongezwa kiganja kimoja).* Sehemu yake ya chini ni mkono mmoja na upana wake mkono mmoja. Ina ukingo ambao upana wake ni shubiri* moja kuzunguka pembeni. Hiyo ndiyo sehemu ya chini ya madhabahu. 14  Kuanzia sehemu ya chini ya sakafu mpaka kwenye kidato cha chini kinachozunguka pande zote ni mikono miwili, na upana wake ni mkono mmoja. Kuanzia kidato kidogo kinachozunguka pande zote mpaka kwenye kidato kikubwa kinachozunguka pande zote ni mikono minne, na upana wake ni mkono mmoja. 15  Jiko la madhabahu lina urefu wa mikono minne, na kutoka kwenye jiko la madhabahu kuelekea juu kuna zile pembe nne.+ 16  Jiko la madhabahu ni la mraba, urefu wake ni mikono 12 na upana wake ni mikono 12.+ 17  Pande nne za kidato kinachozunguka zina urefu wa mikono 14 na upana wa mikono 14; na ukingo unaozunguka ni nusu mkono, na sehemu yake ya chini ni mkono mmoja pande zote. “Na ngazi zake zinatazama upande wa mashariki.” 18  Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Hii ndiyo miongozo ya kufuata madhabahu inapotengenezwa, ili dhabihu nzima za kuteketezwa zitolewe na damu inyunyizwe juu yake.’+ 19  “‘Utawapa makuhani Walawi wazao wa Sadoki+ wanaonikaribia ili kunihudumia ng’ombe dume mchanga wa kundi kwa ajili ya dhabihu ya dhambi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 20  ‘Unapaswa kuchukua kiasi fulani cha damu yake na kuitia kwenye zile pembe nne za madhabahu, juu ya ncha nne za kidato kinachozunguka pande zote, na juu ya ukingo unaozunguka pande zote, ili kuitakasa kutokana na dhambi na kufunika dhambi yake.+ 21  Kisha utamchukua yule ng’ombe dume mchanga, ile dhabihu ya dhambi, ili umteketeze mahali palipochaguliwa pa hekalu, nje ya patakatifu.+ 22  Katika siku ya pili utatoa mbuzi dume ambaye hana kasoro kwa ajili ya dhabihu ya dhambi; nao wataitakasa madhabahu kutokana na dhambi kama walivyoitakasa kutokana na dhambi kwa kutumia yule ng’ombe dume mchanga.’ 23  “‘Utakapomaliza kuitakasa kutokana na dhambi, utatoa ng’ombe dume mchanga wa kundi ambaye hana kasoro na kondoo dume wa kundi ambaye hana kasoro. 24  Nawe utawaleta kwa Yehova, na makuhani watawanyunyizia chumvi+ na kuwatoa kwa Yehova wakiwa dhabihu nzima ya kuteketezwa. 25  Kwa siku saba utamtoa mbuzi dume kwa ajili ya dhabihu ya dhambi kila siku,+ pia ng’ombe dume mchanga wa mifugo, na kondoo dume kutoka katika kundi; utawatoa wanyama ambao hawana kasoro.* 26  Kwa siku saba watafunika dhambi ya madhabahu, nao wataitakasa na kuiweka tayari. 27  Baada ya siku hizo kwisha, siku ya nane+ na kuendelea, kuhani atatoa dhabihu zenu* nzima za kuteketezwa na dhabihu za ushirika kwenye madhabahu; nami nitafurahishwa nanyi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

Maelezo ya Chini

Au labda, “alipokuja.”
Tnn., “kwenye ile nyumba.”
Tnn., “kupima kielelezo chake.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Yaani, upana wa kiganja cha mkono kuanzia kidole gumba hadi kidole kidogo, karibu sentimita 22.2 ( inchi 8.75). Angalia Nyongeza B14.
Au “walio kamili.”
Yaani, za watu.