Ezekieli 44:1-31

  • Lango la mashariki kubaki likiwa limefungwa (1-3)

  • Maagizo kuhusu wageni (4-9)

  • Maagizo kwa ajili ya Walawi na makuhani (10-31)

44  Akanirudisha kupitia lango la nje la patakatifu lililotazama mashariki,+ nalo lilikuwa limefungwa.+  Ndipo Yehova akaniambia: “Lango hili litabaki likiwa limefungwa. Halipaswi kufunguliwa, na hakuna mwanadamu yeyote atakayelitumia kuingia; kwa maana mimi Yehova, Mungu wa Israeli, nimeingia kupitia lango hilo,+ basi linapaswa kubaki likiwa limefungwa.  Hata hivyo, kiongozi ataketi humo ili ale mkate mbele zangu mimi Yehova,+ kwa maana yeye ni kiongozi. Ataingia kupitia ukumbi wa lango, naye atatoka kupitia lango hilo.”+  Kisha akanileta kupitia lango la kaskazini mpaka mbele ya hekalu. Nilipotazama nikaona kwamba utukufu wa Yehova ulikuwa umejaa katika hekalu la Yehova.+ Basi nikaanguka chini kifudifudi.+  Ndipo Yehova akaniambia: “Mwana wa binadamu, kaza fikira,* angalia, na usikilize kwa makini nitakayokuambia kuhusu maagizo na sheria za hekalu la Yehova. Tazama kwa makini sana njia ya kuingia hekaluni na njia zote za kutokea patakatifu.+  Utawaambia hivi watu wa nyumba ya Israeli walioasi: ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Matendo yenu yanayochukiza yametosha, enyi watu wa nyumba ya Israeli.  Mnapowaleta patakatifu pangu wageni ambao hawajatahiriwa moyoni na mwilini, wanalitia unajisi hekalu langu. Mnatoa mkate wangu, mafuta, na damu, huku agano langu likivunjwa kwa sababu ya matendo yenu yote yanayochukiza.  Hamjavitunza vitu vyangu vitakatifu.+ Badala yake mnawapa wengine majukumu ya kuhudumu mahali pangu patakatifu.”’  “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Hakuna mgeni yeyote anayeishi Israeli ambaye hajatahiriwa moyoni na mwilini atakayeingia mahali pangu patakatifu.”’ 10  “‘Lakini Walawi waliotangatanga na kwenda mbali nami+ Waisraeli waliponiacha ili kufuata sanamu zao zinazochukiza* watapata madhara ya kosa lao. 11  Nao watakuwa wahudumu wa mahali pangu patakatifu ili kusimamia malango ya hekalu+ na kuhudumu hekaluni. Watawachinja wanyama wa dhabihu nzima za kuteketezwa na dhabihu kwa ajili ya watu, nao watasimama mbele ya watu ili kuwahudumia. 12  Kwa sababu waliwahudumia mbele ya sanamu zao zinazochukiza nao wakawa kikwazo na kuwafanya watu wa nyumba ya Israeli watende dhambi,+ ndiyo sababu nimeinua mkono wangu dhidi yao na kuapa,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nao watapata madhara ya kosa lao. 13  Hawatanikaribia ili kunitumikia wakiwa makuhani wangu wala kukaribia kitu chochote kati ya vitu vyangu vitakatifu au vitu vitakatifu kabisa, nao watabeba aibu yao kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza waliyofanya. 14  Lakini nitawapa kazi ya kushughulikia majukumu ya hekalu, kushughulikia utumishi wa hekaluni na mambo yote yanayopaswa kufanywa humo.’+ 15  “‘Nao makuhani Walawi, wana wa Sadoki,+ walioshughulikia majukumu ya mahali pangu patakatifu Waisraeli waliponiacha,+ watanikaribia ili kunihudumia, nao watasimama mbele zangu ili kunitolea mafuta+ na damu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 16  ‘Hao ndio watakaoingia mahali pangu patakatifu, nao wataikaribia meza yangu ili kunihudumia,+ nao watatimiza majukumu yangu.+ 17  “‘Wanapoingia kwenye malango ya ua wa ndani, wanapaswa kuvaa mavazi ya kitani.+ Hawapaswi kuvaa vazi lolote la sufu wanapohudumu katika malango ya ua wa ndani au wakiwa ndani. 18  Wanapaswa kuvaa vilemba vya kitani kichwani, nao wanapaswa kuvaa suruali fupi za kitani viunoni mwao.+ Hawapaswi kuvaa chochote kitakachofanya watokwe na jasho. 19  Kabla ya kwenda kwenye ua wa nje—ua wa nje mahali palipo na watu—wanapaswa kuyavua mavazi waliyokuwa wamevaa walipokuwa wakihudumu+ na kuyaweka katika vyumba vitakatifu vya kulia chakula.*+ Kisha watavaa mavazi mengine, ili wasije wakawapitishia watu utakatifu* kwa mavazi hayo. 20  Hawapaswi kunyoa kichwa chao+ au kuacha nywele za kichwa chao ziwe ndefu. Wanapaswa kupunguza nywele za vichwa vyao. 21  Makuhani hawapaswi kunywa divai wanapoingia kwenye ua wa ndani.+ 22  Hawapaswi kumwoa mjane au mwanamke aliyetalikiwa;+ lakini wanaweza kumwoa bikira wa uzao wa Israeli au mjane wa kuhani.’+ 23  “‘Wanapaswa kuwafundisha watu wangu tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu cha kawaida; nao watawafundisha tofauti kati ya kitu kisicho safi na kitu kilicho safi.+ 24  Wanapaswa kuwa waamuzi katika kesi;+ ni lazima wahukumu kulingana na sheria zangu.*+ Wanapaswa kufuata sheria zangu na amri zangu zinazohusu sherehe zangu zote+ na kuzitakasa sabato zangu. 25  Hawapaswi kumkaribia mwanadamu yeyote aliyekufa, la sivyo hawatakuwa safi. Hata hivyo, wanaweza kujichafua kwa ajili ya baba, mama, mwana, binti, au dada yao ambaye hajaolewa.+ 26  Na baada ya kuhani kutakaswa, wanapaswa kumhesabia siku saba. 27  Siku anayoingia katika mahali patakatifu, katika ua wa ndani, ili kuhudumu katika mahali patakatifu anapaswa kutoa dhabihu yake ya dhambi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 28  “‘Na huu ndio utakaokuwa urithi wao: Mimi ndiye urithi wao.+ Msiwape mali yoyote katika Israeli, kwa maana mimi ndiye mali yao. 29  Wao ndio watakaokula toleo la nafaka,+ dhabihu ya dhambi, na dhabihu ya hatia,+ na kila kitu kilichotolewa katika Israeli kitakuwa chao.+ 30  Matunda yote ya kwanza yaliyo bora na kila aina ya mchango mtakaotoa utakuwa wa makuhani.+ Nanyi mnapaswa kumpatia kuhani mavuno ya kwanza ya unga wenu ambao haujakobolewa.+ Hilo litafanya baraka ikae juu ya nyumba zenu.+ 31  Makuhani hawapaswi kula ndege yeyote au mnyama yeyote aliyepatikana amekufa au kuraruliwa vipandevipande.’+

Maelezo ya Chini

Tnn., “elekeza moyo wako.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “vile vyumba vitakatifu.”
Tnn., “wasije wakawatakasa watu.”
Tnn., “maamuzi yangu ya hukumu.”