Ezekieli 45:1-25

  • Mchango mtakatifu na jiji (1-6)

  • Sehemu ya kiongozi (7, 8)

  • Viongozi watatenda kwa unyoofu (9-12)

  • Michango ya watu na ya kiongozi (13-25)

45  “‘Mtakapoigawa nchi iwe urithi,+ mnapaswa kumtolea Yehova sehemu takatifu ya nchi kuwa mchango.+ Inapaswa kuwa na urefu wa mikono 25,000,* na upana wa mikono 10,000.+ Eneo hilo lote litakuwa* sehemu takatifu.  Ndani yake kutakuwa na eneo la mraba la mahali patakatifu lenye urefu wa mikono 500 na upana wa mikono 500,*+ na kila upande litakuwa na malisho yenye kipimo cha mikono 50.+  Na kutoka katika kipimo hicho utapima urefu wa 25,000 na upana wa 10,000, na ndani yake kutakuwa na mahali patakatifu, kitu kitakatifu kabisa.  Litakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani,+ wahudumu wa mahali patakatifu, wanaokaribia ili kumhudumia Yehova.+ Patakuwa mahali kwa ajili ya nyumba zao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu.  “‘Walawi, wahudumu wa hekaluni, watakuwa na sehemu yenye urefu wa mikono 25,000 na upana wa mikono 10,000,+ nao watamiliki vyumba 20 vya kulia chakula.*+  “‘Mnapaswa kutoa sehemu ya jiji yenye urefu wa mikono 25,000 (inayolingana na mchango mtakatifu) na upana wa mikono 5,000.+ Itakuwa ya watu wote wa nyumba ya Israeli.  “‘Na kwa ajili ya kiongozi kutakuwa na ardhi pande zote mbili za ule mchango mtakatifu na eneo lililogawiwa jiji. Itapakana na ule mchango mtakatifu na eneo la jiji. Itakuwa upande wa magharibi na upande wa mashariki. Urefu wake kuanzia mpaka wa magharibi hadi mpaka wa mashariki utakuwa sawa na mojawapo ya sehemu za makabila.+  Ardhi hii itakuwa mali yake katika Israeli. Nao viongozi wangu hawatawatesa tena watu wangu,+ nao watawapa nchi watu wa nyumba ya Israeli kulingana na makabila yao.’+  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Imetosha, enyi viongozi wa Israeli!’ “‘Acheni ukatili na ukandamizaji, na mtende mambo ya haki na ya uadilifu.+ Acheni kuchukua kwa nguvu mali ya watu wangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 10  ‘Mnapaswa kutumia mizani sahihi na kipimo sahihi cha efa* na kipimo sahihi cha bathi.*+ 11  Kunapaswa kuwa na kipimo hususa cha efa na cha bathi. Kipimo cha bathi kinapaswa kuwa sehemu ya kumi ya homeri* na kipimo cha efa kinapaswa kuwa sehemu ya kumi ya homeri. Homeri ndiyo itakayokuwa kiwango cha kupimia. 12  Shekeli*+ inapaswa kuwa gera 20.* Na shekeli 20 ukijumlisha na shekeli 25 na pia shekeli 15, jumla yake itakuwa mane* moja kwako.’ 13  “‘Huu ndio mchango unaopaswa kutoa: sehemu ya sita ya efa kutoka katika kila homeri ya ngano, na sehemu ya sita ya efa kutoka katika kila homeri ya shayiri. 14  Posho ya mafuta inapaswa kupimwa kwa kipimo cha bathi. Bathi ni sehemu ya kumi ya kori* na bathi kumi ni homeri moja, kwa sababu bathi kumi zinalingana na homeri moja. 15  Na kutoka katika kundi la mifugo ya Waisraeli, kondoo mmoja anapaswa kutolewa kwa kila kondoo 200. Hawa watatolewa kwa ajili ya toleo la nafaka,+ dhabihu nzima ya kuteketezwa,+ na dhabihu za ushirika,+ ili kufunika dhambi za watu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 16  “‘Watu wote nchini watatoa mchango huu+ kwa kiongozi wa Israeli. 17  Lakini kiongozi atakuwa na wajibu wa kushughulikia dhabihu nzima za kuteketezwa,+ toleo la nafaka,+ na toleo la kinywaji wakati wa sherehe,+ miezi mipya, Sabato,+ na sherehe zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli.+ Yeye ndiye atakayetoa dhabihu ya dhambi, toleo la nafaka, dhabihu nzima ya kuteketezwa, na dhabihu za ushirika, ili kufunika dhambi za watu wa nyumba ya Israeli.’ 18  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, unapaswa kumchukua ng’ombe dume mchanga asiye na kasoro kutoka katika mifugo, nawe utapatakasa mahali patakatifu kutokana na dhambi.+ 19  Kuhani atachukua sehemu ya damu ya dhabihu ya dhambi na kuiweka kwenye mwimo wa mlango wa hekalu,+ juu ya zile pembe nne za ukingo unaozunguka madhabahu, na juu ya mwimo wa lango la ua wa ndani. 20  Hivyo ndivyo utakavyofanya katika siku ya saba ya mwezi kwa sababu ya mtu yeyote anayefanya dhambi bila kukusudia au bila kujua;+ nanyi mtatoa dhabihu ya kufunika dhambi ya hekalu.+ 21  “‘Katika mwezi wa kwanza, siku ya 14 ya mwezi huo, mtafanya sherehe ya Pasaka.+ Kwa siku saba mnapaswa kula mikate isiyo na chachu.+ 22  Siku hiyo kiongozi atatoa ng’ombe dume mchanga awe dhabihu ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote nchini.+ 23  Kwa siku saba za sherehe atamtolea Yehova dhabihu nzima ya kuteketezwa ya ng’ombe dume saba wachanga wasio na kasoro na kondoo dume saba wasio na kasoro kila siku kwa siku hizo saba,+ atatoa pia mbuzi dume kila siku awe dhabihu ya dhambi. 24  Pia anapaswa kutoa toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya kila ng’ombe dume mchanga na efa moja kwa ajili ya kila kondoo dume, vilevile hini* moja ya mafuta kwa kila efa. 25  “‘Katika mwezi wa saba, siku ya 15 ya mwezi huo, kwa siku saba wakati wa sherehe,+ anapaswa kutoa dhabihu ileile ya dhambi, dhabihu nzima ya kuteketezwa, toleo la nafaka, na mafuta.’”

Maelezo ya Chini

Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Au “Sehemu yote iliyo ndani ya mipaka hiyo itakuwa.”
Tnn., “500 kwa 500.”
Au “vyumba 20.”
Au “mina.” Angalia Nyongeza B14.