Ezekieli 46:1-24

  • Matoleo ya pindi mbalimbali (1-15)

  • Kurithi mali ya kiongozi (16-18)

  • Sehemu za kuchemshia dhabihu (19-24)

46  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Lango la ua wa ndani linalotazama mashariki+ linapaswa kubaki likiwa limefungwa+ kwa siku sita za kazi,+ lakini siku ya Sabato na siku ya mwezi mpya linapaswa kufunguliwa.  Kiongozi ataingia ndani kupitia njia ya ukumbi wa lango,+ naye atasimama kando ya mwimo wa lango. Makuhani watatoa dhabihu yake nzima ya kuteketezwa na dhabihu zake za ushirika, naye atainama chini kwenye kizingiti cha lango na kutoka nje. Lakini lango linapaswa kubaki wazi mpaka jioni.  Watu wa nchi watainama chini pia mbele za Yehova kwenye kizingiti cha lango hilo siku za Sabato na wakati wa miezi mipya.+  “‘Siku ya Sabato kiongozi atamtolea Yehova dhabihu nzima ya kuteketezwa ya wanakondoo dume sita wasio na kasoro na kondoo dume asiye na kasoro.+  Toleo la nafaka litakuwa efa moja* kwa ajili ya yule kondoo dume na chochote anachoweza kutoa kwa ajili ya wale wanakondoo dume, pamoja na hini moja* ya mafuta kwa kila efa.+  Siku ya mwezi mpya atatoa ng’ombe dume mchanga wa kundi asiye na kasoro, wanakondoo sita dume, na kondoo dume mmoja; hawapaswi kuwa na kasoro.+  Atatoa toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya yule ng’ombe dume mchanga, na efa moja kwa ajili ya yule kondoo dume, na chochote anachoweza kutoa kwa ajili ya wale wanakondoo dume. Naye anapaswa kutoa hini moja ya mafuta kwa kila efa.  “‘Kiongozi anapoingia, anapaswa kuingia kupitia njia ya ukumbi wa lango, naye anapaswa kutoka kupitia njia hiyohiyo.+  Na watu wa nchi wanapoingia mbele za Yehova wakati wa sherehe,+ wale wanaoingia kupitia lango la kaskazini+ ili kuabudu, wanapaswa kutoka kupitia lango la kusini,+ na wale wanaoingia kupitia lango la kusini wanapaswa kutoka kupitia lango la kaskazini. Mtu yeyote asirudi kupitia lango aliloingilia, kwa maana wanapaswa kutoka kupitia lango lililo upande mwingine. 10  Naye kiongozi aliye miongoni mwao, anapaswa kuingia wanapoingia, na kutoka wanapotoka. 11  Wakati wa sherehe na majira ya sherehe anapaswa kutoa toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya yule ng’ombe dume mchanga, efa moja kwa ajili ya yule kondoo dume, na chochote anachoweza kutoa kwa ajili ya wale wanakondoo dume, pamoja na hini moja ya mafuta kwa kila efa.+ 12  “‘Ikiwa kiongozi atatoa dhabihu nzima ya kuteketezwa+ au dhabihu za ushirika ziwe toleo la hiari kwa Yehova, atafunguliwa lango linalotazama mashariki, naye atatoa dhabihu yake nzima ya kuteketezwa na dhabihu zake za ushirika kama anavyofanya siku ya Sabato.+ Baada ya kutoka nje, lango linapaswa kufungwa.+ 13  “‘Kila siku unapaswa kumtoa mwanakondoo dume asiye na kasoro aliye katika mwaka wake wa kwanza awe dhabihu nzima ya kuteketeza kwa Yehova.+ Unapaswa kufanya hivyo kila asubuhi. 14  Pamoja na mwanakondoo huyo, kila asubuhi unapaswa kutoa sehemu ya sita ya efa iwe toleo la nafaka, pamoja na sehemu ya tatu ya hini ya mafuta ili inyunyizwe juu ya unga laini kama toleo la kawaida la nafaka kwa Yehova. Hii ni sheria ya kudumu. 15  Wanapaswa kumtoa mwanakondoo dume, toleo la nafaka, na mafuta kila asubuhi kama dhabihu nzima ya kuteketezwa ya kawaida.’ 16  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kiongozi akimpa zawadi kila mmoja wa wanawe iwe urithi, itakuwa mali ya wanawe. Hiyo ni miliki yao waliyorithi. 17  Lakini akimpa mmoja wa watumishi wake zawadi kutoka katika urithi wake, itakuwa yake mpaka mwaka wa uhuru;+ kisha itarudi kwa kiongozi. Urithi wa wanawe tu ndio utakaokuwa wao daima. 18  Kiongozi hapaswi kuchukua urithi wowote wa watu kwa kuwalazimisha waondoke katika mali yao. Anapaswa kuwapa wanawe urithi kutoka kwenye mali yake mwenyewe, ili mtu yeyote miongoni mwa watu wangu asiondolewe kwa lazima katika mali yake.’” 19  Kisha akaniingiza kupitia njia+ iliyokuwa kando ya lango linaloelekea kwenye vyumba vitakatifu vya kulia chakula* vya makuhani, vilivyotazama kaskazini,+ na hapo nikaona mahali upande wa nyuma kuelekea magharibi. 20  Akaniambia: “Hapa ndipo mahali ambapo makuhani watachemshia dhabihu ya hatia na dhabihu ya dhambi na mahali ambapo wataokea toleo la nafaka,+ ili wasibebe chochote na kukipeleka kwenye ua wa nje na kuwapitishia watu utakatifu.”*+ 21  Akanitoa nje kwenye ua wa nje na kuniongoza kupitia zile pembe nne za ua, nami nikaona ua kando ya kila pembe ya ua wa nje. 22  Kwenye hizo pembe nne za ua kulikuwa na nyua ndogo, zenye urefu wa mikono 40* na upana wa mikono 30. Nyua zote nne zilikuwa na ukubwa uleule.* 23  Kulikuwa na vidato* kuzunguka nyua zote nne, na chini ya vidato hivyo walijenga sehemu za kuchemshia dhabihu. 24  Kisha akaniambia: “Hizi ndizo nyumba ambamo wahudumu wa hekalu huchemshia dhabihu zinazoletwa na watu.”+

Maelezo ya Chini

Au “vyumba vitakatifu.”
Tnn., “kuwatakasa watu.”
Hiki ni kipimo cha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.
Au “Zote nne na nyua zake za pembeni zilikuwa na ukubwa uleule.”
Au “safu.”