Ezekieli 6:1-14

  • Dhidi ya milima ya Israeli (1-14)

    • Sanamu zinazochukiza zitafedheheshwa (4-6)

    • “Mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova” (7)

6  Neno la Yehova likanijia tena likisema:  “Mwana wa binadamu, uelekeze uso wako kwenye milima ya Israeli na utabiri dhidi yake.  Nawe utasema, ‘enyi milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyoiambia milima, vilima, vijito na mabonde: “Tazameni! Ninaleta upanga dhidi yenu, nami nitaharibu mahali penu pa juu.  Madhabahu zenu zitabomolewa na vinara vyenu vya uvumba vitavunjwa,+ na waliouawa kati yenu nitawatupa chini mbele ya sanamu zenu zinazochukiza.*+  Nami nitazitupa maiti za watu wa Israeli mbele ya sanamu zao zinazochukiza, nami nitaitawanya mifupa yenu kuzunguka pande zote za madhabahu zenu.+  Katika makao yenu yote, majiji yataharibiwa+ na mahali pa juu patabomolewa na kuachwa ukiwa.+ Madhabahu zenu zitaharibiwa na kuvunjwa vipandevipande, sanamu zenu zinazochukiza zitaharibiwa, vinara vyenu vya uvumba vitakatwakatwa, na kazi zenu zitafutiliwa mbali.  Na wale waliouawa wataanguka katikati yenu,+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+  “‘“Lakini nitaacha wengine wabaki, kwa maana baadhi yenu wataponyoka upanga miongoni mwa mataifa mtakapotawanywa katika nchi mbalimbali.+  Na wale watakaoponyoka watanikumbuka kati ya mataifa ambamo watapelekwa mateka.+ Watatambua kwamba nilikuwa nimevunjika moyo kwa sababu ya moyo wao usio na uaminifu* ulioniacha+ na macho yao ambayo yanatamani sana* sanamu zao zinazochukiza.+ Wataaibika na kuchukizwa na mambo yote maovu na yenye kuchukiza ambayo wametenda.+ 10  Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova na kwamba vitisho vyangu vya kuwaletea msiba huu havikuwa vya bure.”’+ 11  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Piga makofi na upige mguu chini, na uomboleze kwa sababu ya mambo yote maovu na yanayochukiza yaliyofanywa na watu wa nyumba ya Israeli, kwa maana watakufa kwa upanga, kwa njaa kali na kwa ugonjwa hatari.+ 12  Yule aliye mbali sana atakufa kwa ugonjwa hatari, na yule aliye karibu atauawa kwa upanga, na yeyote anayeponyoka mambo hayo na kubaki atakufa kwa njaa kali; nami nitawamwagia kikamili ghadhabu yangu.+ 13  Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova+ wakati waliouawa miongoni mwao watakapotapakaa kati ya sanamu zao zinazochukiza kuzunguka pande zote za madhabahu zao,+ juu ya kila kilima kirefu, juu ya vilele vyote vya milima, na chini ya kila mti wenye majani mengi, na chini ya matawi ya miti mikubwa, mahali ambapo wametoa dhabihu zenye harufu nzuri* ili kuzituliza sanamu zao zote zinazochukiza.+ 14  Nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yao na kuifanya nchi iwe ukiwa, na makao yao yote yatakuwa ukiwa kuliko nyika iliyo karibu na Dibla. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”

Maelezo ya Chini

Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “yanayofuatilia kwa upotovu wa kimaadili.”
Au “uliopotoka kimaadili; wa ukahaba.”
Au “wametoa harufu zinazovutia.”