Ezekieli 7:1-27

  • Mwisho umefika (1-27)

    • Msiba wa pekee (5)

    • Pesa zatupwa barabarani (19)

    • Hekalu litatiwa unajisi (22)

7  Neno la Yehova likanijia tena likisema:  “Nawe Mwana wa binadamu, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anavyoiambia nchi ya Israeli: ‘Mwisho! Mwisho umezifikia pembe nne za nchi.  Sasa mwisho umekufikia, nami nitakumwagia hasira yangu, nami nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuadhibu* kwa sababu ya matendo yako yote yanayochukiza.  Jicho langu halitakusikitikia; wala sitakuhurumia,+ kwa maana nitakuletea matokeo ya njia zako mwenyewe, nawe utapatwa na madhara ya matendo yako yanayochukiza.+ Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+  “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Tazama! Msiba, msiba wa pekee, unakuja.+  Mwisho unakuja; mwisho utakuja; utainuka* wenyewe dhidi yako. Tazama! Unakuja.  Zamu yako imefika,* wewe unayekaa nchini. Wakati unakuja, siku hiyo iko karibu.+ Kuna vurugu, wala si kelele za shangwe milimani.  “‘Hivi karibuni nitakumwagia ghadhabu yangu,+ nami nitakumwagia hasira yangu yote,+ nami nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuadhibu* kwa sababu ya matendo yako yote yanayochukiza.  Jicho langu halitakusikitikia; wala sitakuhurumia.+ Kwa maana nitakuletea matokeo ya njia zako mwenyewe, nawe utapatwa na madhara ya matendo yako mwenyewe yanayochukiza. Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, ndiye ninayewapiga.+ 10  “‘Tazama, ile siku! Tazama, inakuja!+ Zamu yako imefika;* fimbo imechanua na kimbelembele kimechipuka. 11  Ukatili umesitawi na kuwa fimbo ya uovu.+ Wao wenyewe, mali yao, umati wao, wala umashuhuri wao hautaokoka. 12  Wakati utakuja, siku hiyo itafika. Mnunuzi asishangilie, na muuzaji asiomboleze, kwa maana kuna ghadhabu dhidi ya umati wao wote.*+ 13  Kwa maana muuzaji hatakirudia kitu alichouza, hata uhai wake ukiokolewa, kwa maana maono hayo yanahusu umati wote. Hakuna atakayerudi, na kwa sababu ya kosa lake,* hakuna atakayeokoa uhai wake. 14  “‘Wamepiga tarumbeta+ na kila mtu yuko tayari, lakini hakuna anayeenda vitani, kwa sababu nina ghadhabu dhidi ya umati wote.+ 15  Upanga uko nje,+ na ugonjwa hatari na njaa kali zimo ndani. Yeyote aliye uwanjani atakufa kwa upanga, na njaa kali na ugonjwa hatari vitawameza wale walio jijini.+ 16  Watu wao watakaofanikiwa kuponyoka wataenda milimani, na kama njiwa wa mabondeni, kila mmoja ataomboleza kwa sababu ya kosa lake.+ 17  Mikono yao yote italegea, na magoti yao yote yatadondosha maji.*+ 18  Wamevaa nguo za magunia,+ nao wanatetemeka.* Kila mtu ataaibishwa, na kila kichwa kitakuwa na upara.*+ 19  “‘Watatupa fedha yao barabarani, nayo dhahabu yao itawachukiza. Wala fedha yao wala dhahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya ghadhabu ya Yehova.+ Hawatashiba,* wala kuyajaza matumbo yao, kwa maana vitu hivyo* vimekuwa kikwazo kinachosababisha kosa lao. 20  Walijivunia urembo wa mapambo yao, nao wakayatumia* kutengeneza mifano yao inayochukiza, sanamu zao zinazochukiza.+ Ndiyo sababu nitaifanya fedha na dhahabu yao kuwa chukizo kwao. 21  Nami nitaitia* mikononi mwa wageni ili waipore na kuwapa waovu wa dunia kuwa nyara, nao wataitia unajisi. 22  “‘Nami nitaugeuza uso wangu kutoka kwao,+ nao watapatia unajisi mahali pangu palipofichika,* na wanyang’anyi wataingia mahali hapo na kupatia unajisi.+ 23  “‘Tengeneza mnyororo,*+ kwa maana nchi imejaa hukumu yenye madoa ya damu+ na jiji limejaa ukatili.+ 24  Nami nitaingiza mataifa mabaya kabisa,+ nayo yatamiliki nyumba zao,+ nami nitakikomesha kiburi cha wenye nguvu, na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi.+ 25  Maumivu yao yatakapokuja, watatafuta amani lakini haitakuwepo.+ 26  Msiba utakuja juu ya msiba, na habari baada ya habari, na watu watatafuta maono kutoka kwa nabii,+ lakini sheria itatoweka* kutoka kwa kuhani na ushauri* kutoka kwa wazee.+ 27  Mfalme ataomboleza,+ naye mkuu atavaa kukata tamaa,* na mikono ya watu wa nchi itatetemeka kwa hofu. Nitawatendea kulingana na njia zao, nami nitawahukumu kama walivyohukumu. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”+

Maelezo ya Chini

Au “kukufanya uwajibike.”
Tnn., “utaamka.”
Au labda, “Shada lako la maua limefika.”
Au “kukufanya uwajibike.”
Au labda, “Shada lako la maua limefika.”
Yaani, wale wanaonunua mali na pia wale wanaouza hawatafaidika, kwa maana wote wataangamizwa.
Au labda, “kwa kosa lake.”
Yaani, watajikojolea kwa sababu ya woga.
Yaani, vichwa vyao vitanyolewa kwa sababu ya maombolezo.
Tnn., “wamefunikwa na hofu.”
Au “Nafsi zao hazitashiba.”
Yaani, fedha yao na dhahabu yao.
Yaani, mapambo ya dhahabu na fedha.
Yaani, fedha yao na dhahabu yao waliyotumia kutengeneza sanamu.
Inaonekana ni sehemu ya ndani zaidi ya mahali patakatifu pa Yehova.
Yaani, minyororo ya utekwa.
Au “mafundisho yatatoweka.”
Au “mashauri.”
Au “ukiwa.”