Ezekieli 9:1-11

  • Wanaume sita wanaoangamiza na mwanamume mwenye kidau cha wino (1-11)

    • Hukumu itaanzia patakatifu (6)

9  Kisha nikamsikia akisema hivi kwa sauti kubwa: “Waiteni wale watakaoliadhibu jiji hili, kila mmoja wao akiwa na silaha yake ya kuangamiza mkononi mwake!”  Nikaona wanaume sita wakija kutoka upande wa lango la juu+ linalotazama kaskazini, kila mmoja akiwa na silaha yake ya kuponda mkononi mwake; na kulikuwa na mwanamume mmoja kati yao aliyevaa kitani, akiwa na kidau cha wino cha mwandishi kiunoni,* nao wakaingia ndani na kusimama kando ya madhabahu ya shaba.+  Kisha utukufu wa Mungu wa Israeli+ ukainuka kutoka mahali ulipokuwa umetulia juu ya makerubi na kwenda kwenye kizingiti cha mlango wa nyumba hiyo,+ naye akaanza kumwita kwa sauti yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino cha mwandishi kiunoni.  Yehova akamwambia: “Pita kotekote jijini, katika jiji lote la Yerusalemu, nawe uyatie alama mapaji ya nyuso za watu wanaolia kwa uchungu na kwa maumivu makali+ kwa sababu ya mambo yote yanayochukiza yanayofanywa jijini.”+  Naye akawaambia wale wengine huku nikisikia: “Piteni kotekote jijini baada yake na kuua. Jicho lenu lisisikitike, wala msiwe na huruma hata kidogo.+  Mnapaswa kuwaua wote kabisa, mzee, kijana, bikira, mtoto mdogo, na wanawake.+ Lakini msimkaribie mtu yeyote aliye na ile alama.+ Mnapaswa kuanzia mahali pangu patakatifu.”+ Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya ile nyumba.+  Kisha akawaambia: “Itieni nyumba unajisi na kuzijaza nyua wale waliouawa.+ Nendeni!” Basi wakaenda na kuwaua watu jijini.  Walipokuwa wakiwaua, nilibaki mimi peke yangu, nikaanguka kifudifudi na kupaza sauti: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Je, utawaangamiza Waisraeli wote wanaobaki unapolimwagia ghadhabu yako jiji la Yerusalemu?”+  Basi akaniambia: “Kosa la watu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni kubwa sana, kubwa kwelikweli.+ Nchi imejaa umwagaji wa damu,+ nalo jiji limejaa ufisadi.+ Kwa maana wanasema, ‘Yehova ameiacha nchi hii, na Yehova haoni.’+ 10  Lakini mimi, jicho langu halitasikitika; wala sitawahurumia.+ Nitawaletea madhara ya njia yao juu ya kichwa chao wenyewe.” 11  Ndipo nikamwona yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino kiunoni, akirudi na kuleta habari akisema: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.”

Maelezo ya Chini

Au “chombo cha kuwekea wino cha mwandishi.”