Ezra 1:1-11

  • Agizo la Mfalme Koreshi la kujenga upya hekalu (1-4)

  • Watu walio uhamishoni wajitayarisha kurudi Babiloni (5-11)

1  Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi+ wa Uajemi, ili neno la Yehova lililosemwa na Yeremia+ litimie, Yehova aliichochea roho ya Mfalme Koreshi wa Uajemi atoe tangazo katika ufalme wake wote, ambalo pia aliliandika,+ akisema:  “Mfalme Koreshi wa Uajemi anasema hivi: ‘Yehova Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia,+ naye ameniagiza nimjengee nyumba Yerusalemu, nchini Yuda.+  Yeyote miongoni mwenu, ninyi watu wake wote, Mungu wake na awe pamoja naye, na apande kwenda Yerusalemu, kule Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli—yeye ndiye Mungu wa kweli—ambaye nyumba yake ilikuwa Yerusalemu.*  Na mkaaji mgeni yeyote,+ popote alipo, majirani zake* wamsaidie kwa kumpa fedha na dhahabu, mali na wanyama wa kufugwa, pamoja na toleo la hiari kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa kweli,+ iliyokuwa Yerusalemu.’”  Ndipo viongozi wa ukoo* wa Yuda na Benjamini na makuhani na Walawi—kila mmoja ambaye roho yake ilichochewa na Mungu wa kweli—wakajitayarisha kupanda kwenda kujenga upya nyumba ya Yehova, iliyokuwa Yerusalemu.  Wale wote waliowazunguka wakawasaidia kwa kuwapa* vyombo vya fedha na dhahabu, mali, wanyama wa kufugwa, na vitu vyenye thamani, mbali na matoleo yote ya hiari.  Pia, Mfalme Koreshi akaleta vyombo vya nyumba ya Yehova ambavyo Nebukadneza alikuwa amechukua huko Yerusalemu na kuviweka katika nyumba ya mungu wake.+  Mfalme Koreshi wa Uajemi akavikabidhi kwa Mithredathi mweka-hazina ambaye alivihesabu na kumpa Sheshbazari*+ mkuu wa Yuda.  Hii ndiyo idadi yake: vyombo 30 vya dhahabu vyenye umbo la kikapu, vyombo 1,000 vya fedha vyenye umbo la kikapu, vyombo 29 vya akiba, 10  mabakuli madogo 30 ya dhahabu, mabakuli madogo 410 ya fedha, vyombo vingine 1,000. 11  Vyombo vyote vya dhahabu na vya fedha vilikuwa 5,400. Sheshbazari alivibeba vyote wakati yeye na watu waliohamishwa+ walipoondoka Babiloni kwenda Yerusalemu.

Maelezo ya Chini

Au labda, “aliye Yerusalemu.”
Tnn., “watu wa mahali pake.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “wakaitia nguvu mikono yao kwa.”
Labda ni Zerubabeli anayetajwa kwenye Ezr 2:2; 3:8.