Ezra 10:1-44

  • Agano la kuwafukuza wanawake wa kigeni (1-14)

  • Wanawake wa kigeni wafukuzwa (15-44)

10  Ezra alipokuwa akisali+ na kuungama, akilia na kulala kifudifudi mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli, umati mkubwa wa wanaume, wanawake, na watoto wa Israeli wakakusanyika kumzunguka, kwa maana watu walikuwa wakilia sana.  Ndipo Shekania mwana wa Yehieli+ wa wana wa Elamu+ akamwambia Ezra: “Tumetenda kwa ukosefu wa uaminifu dhidi ya Mungu wetu kwa kuoa* wanawake wa kigeni kutoka kwa mataifa ya nchi hii.+ Ingawa hivyo, bado kuna tumaini kwa Israeli.  Basi na tufanye agano na Mungu wetu+ la kuwafukuza wake hao wote na watoto wao kulingana na mwongozo wa Yehova na wa wale wanaohofu* amri ya Mungu wetu.+ Na tutende kulingana na Sheria.  Simama, kwa maana jambo hili ni jukumu lako, nasi tuko pamoja nawe. Uwe imara na uchukue hatua.”  Ndipo Ezra akasimama, akawaapisha wakuu wa makuhani, Walawi, na Waisraeli wote kwamba watafanya kama ilivyosemwa.+ Basi wakaapa.  Sasa Ezra akaondoka mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli na kwenda katika chumba cha* Yehohanani mwana wa Eliashibu. Ingawa alienda huko, hakula chakula wala kunywa maji, kwa maana alikuwa akiomboleza kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wa watu waliotoka uhamishoni.+  Ndipo wakatangaza kotekote katika Yuda na Yerusalemu kwamba watu wote waliotoka uhamishoni wakusanyike Yerusalemu;  na wakuu na wanaume wazee wakaamua kwamba yeyote ambaye hangekuja katika muda wa siku tatu, mali zake zote zingechukuliwa,* naye angefukuzwa kutoka kwenye kutaniko la watu waliotoka uhamishoni.+  Basi wanaume wote wa Yuda na Benjamini wakakusanyika Yerusalemu katika muda wa siku tatu, yaani, katika mwezi wa tisa siku ya 20 ya mwezi huo. Watu wote walikuwa wameketi kwenye uwanja wa nyumba ya Mungu wa kweli, wakitetemeka kwa sababu ya jambo hilo na kwa sababu ya mvua kubwa. 10  Kisha kuhani Ezra akasimama na kuwaambia: “Mmetenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa kuoa wanawake wa kigeni+ na hivyo mmeongeza hatia ya Israeli. 11  Sasa ungameni kwa Yehova Mungu wa mababu zenu na mfanye mapenzi yake. Jitengeni na watu wa mataifa na hawa wake wa kigeni.”+ 12  Ndipo kutaniko lote likajibu hivi kwa sauti kubwa: “Ni wajibu wetu kufanya kikamili mambo unayotuambia. 13  Hata hivyo, watu ni wengi, na haya ni majira ya mvua. Haiwezekani kusimama nje, na jambo hili halitamalizika kwa siku moja au mbili, kwa maana tumeasi sana katika jambo hili. 14  Basi, tafadhali, acha wakuu wetu waliwakilishe kutaniko lote;+ na watu wote katika majiji yetu ambao wameoa wanawake wa kigeni waje wakati uliowekwa, pamoja na wazee na waamuzi wa kila jiji, mpaka tutakapoituliza hasira inayowaka ya Mungu wetu kuhusiana na jambo hili.” 15  Hata hivyo, Yonathani mwana wa Asaheli na Yahzeya mwana wa Tikva wakapinga jambo hilo, na Meshulamu na Shabethai, waliokuwa Walawi,+ wakawaunga mkono. 16  Lakini watu waliotoka uhamishoni wakafanya kama ilivyokubaliwa; na kuhani Ezra na viongozi wa koo,* watu wote ambao majina yao yalikuwa yameorodheshwa, wakakusanyika peke yao siku ya kwanza ya mwezi wa kumi ili kuchunguza jambo hilo; 17  na kufikia siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakamaliza kuwachunguza wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni. 18  Na ikagunduliwa kwamba baadhi ya wana wa makuhani walikuwa wameoa wanawake wa kigeni:+ kutoka kwa wana wa Yeshua+ mwana wa Yehosadaki na ndugu zake, Maaseya, Eliezeri, Yaribu, na Gedalia. 19  Lakini wakaahidi* kuwafukuza wake zao, na kwa kuwa walikuwa na hatia, wangetoa kondoo dume wa kundi kwa ajili ya hatia yao.+ 20  Kutoka kwa wana wa Imeri,+ kulikuwa na Hanani na Zebadia; 21  na kutoka kwa wana wa Harimu,+ Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli, na Uzia; 22  na kutoka kwa wana wa Pashuri,+ Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi, na Eleasa. 23  Na kutoka kwa Walawi, kulikuwa na Yozabadi, Shimei, Kelaya (yaani, Kelita), Pethahia, Yuda, na Eliezeri; 24  na kutoka kwa waimbaji, Eliashibu; na kutoka kwa walinzi wa malango, Shalumu, Telemu, na Uri. 25  Na kutoka Israeli, kutoka kwa wana wa Paroshi,+ kulikuwa na Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya, na Benaya; 26  na kutoka kwa wana wa Elamu,+ Matania, Zekaria, Yehieli,+ Abdi, Yeremothi, na Eliya; 27  na kutoka kwa wana wa Zatu,+ Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi, na Aziza; 28  na kutoka kwa wana wa Bebai,+ Yehohanani, Hanania, Zabai, na Athlai; 29  na kutoka kwa wana wa Bani, Meshulamu, Maluku, Adaya, Yashubu, Sheali, na Yeremothi; 30  na kutoka kwa wana wa Pahath-moabu,+ Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui, na Manase; 31  na kutoka kwa wana wa Harimu,+ Eliezeri, Ishiya, Malkiya,+ Shemaya, Shimeoni, 32  Benjamini, Maluku, na Shemaria; 33  kutoka kwa wana wa Hashumu,+ Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase, na Shimei; 34  kutoka kwa wana wa Bani, Maadai, Amramu, na Ueli, 35  Benaya, Bedeya, Keluhi, 36  Vania, Meremothi, Eliashibu, 37  Matania, Matenai, na Yaasu; 38  na kutoka kwa wana wa Binui, Shimei, 39  Shelemia, Nathani, Adaya, 40  Maknadebai, Shashai, Sharai, 41  Azareli, Shelemia, Shemaria, 42  Shalumu, Amaria, na Yosefu; 43  na kutoka kwa wana wa Nebo, Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli, na Benaya. 44  Wote hao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni,+ basi wakawafukuza wake zao pamoja na wana wao.+

Maelezo ya Chini

Au “kwa kuwaingiza ndani ya nyumba zetu.”
Tnn., “wanaotetemekea.”
Au “jumba la kulia chakula la.”
Au “zingezuiliwa.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “walipeana mikono yao ili.”