Ezra 5:1-17

  • Wayahudi waanza tena kujenga hekalu (1-5)

  • Barua ambayo Tatenai alimtumia Mfalme Dario (6-17)

5  Ndipo nabii Hagai+ na nabii Zekaria,+ mjukuu wa Ido+ wakawatabiria Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu, katika jina la Mungu wa Israeli aliyekuwa akiwaongoza.  Kisha Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli na Yeshua+ mwana wa Yehosadaki wakaanza kujenga upya nyumba ya Mungu,+ iliyokuwa Yerusalemu; na manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao na waliwatia moyo.+  Wakati huo Tatenai gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto* na Shethar-bozenai na wenzao wakaja na kuwauliza: “Ni nani aliyewaagiza mjenge nyumba hii na kukamilisha nguzo hizi?”*  Pia, wakawauliza: “Wanaume wanaojenga jengo hili ni akina nani?”  Lakini Mungu alikuwa pamoja na* wazee wa Wayahudi,+ nao hawangeweza kuwazuia kabla ya kumwandikia Dario na kupata barua rasmi kuhusu jambo hilo kutoka kwake.  Hii ndiyo nakala ya barua ambayo Tatenai gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto na Shethar-bozenai na wenzake, magavana wadogo wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto, walimtumia Mfalme Dario;  walimtumia habari hiyo, na hivi ndivyo walivyoandika: “Kwa Mfalme Dario: “Na uwe na amani nyingi!  Tungependa kumjulisha mfalme kwamba tulienda katika mkoa* wa Yuda kwenye nyumba ya yule Mungu mkuu, nayo inajengwa kwa mawe makubwa yaliyobingirishwa na kuwekwa mahali pake, na mbao zinawekwa katika kuta. Watu hao wanafanya kazi hiyo kwa bidii na inasonga mbele kwa jitihada zao.  Ndipo tukawauliza wazee wao: ‘Ni nani aliyewaagiza mjenge nyumba hii na kukamilisha nguzo hizi?’*+ 10  Pia, tuliwauliza majina yao ili tuandike majina ya viongozi wao na kukujulisha. 11  “Walitujibu hivi: ‘Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na dunia, na tunajenga upya nyumba iliyojengwa miaka mingi iliyopita, ambayo mfalme fulani mkuu wa Israeli aliijenga na kuikamilisha.+ 12  Lakini kwa sababu baba zetu walimkasirisha Mungu wa mbinguni,+ aliwatia mikononi mwa Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni, Mkaldayo, ambaye aliibomoa nyumba hii+ na kuwapeleka watu uhamishoni huko Babiloni.+ 13  Hata hivyo, katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi wa Babiloni, Mfalme Koreshi alitoa agizo la kuijenga upya nyumba hii ya Mungu.+ 14  Pia, Mfalme Koreshi alitoa katika hekalu la Babiloni vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua hekaluni huko Yerusalemu, na kuvileta katika hekalu la Babiloni.+ Alivikabidhi kwa mtu aitwaye Sheshbazari,*+ ambaye Koreshi alimteua kuwa gavana.+ 15  Koreshi alimwambia: “Chukua vyombo hivi, uvirudishe katika hekalu lililo Yerusalemu, na nyumba ya Mungu ijengwe upya mahali ilipokuwa awali.”+ 16  Ndipo Sheshbazari akaja, akaweka misingi ya nyumba ya Mungu,+ iliyo Yerusalemu; na tangu wakati huo mpaka leo inaendelea kujengwa lakini haijamalizika.’+ 17  “Basi mfalme ukipenda, acha uchunguzi ufanywe katika nyumba ya hazina ya mfalme iliyo Babiloni, ili ijulikane kama Mfalme Koreshi alitoa agizo la kuijenga upya nyumba ya Mungu huko Yerusalemu;+ kisha wewe mfalme ututumie uamuzi wako kuhusu jambo hili.”

Maelezo ya Chini

Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”
Au “mihimili hii.”
Tnn., “macho ya Mungu wao yalikuwa juu ya.”
Au “wilaya ya utawala.”
Au “mihimili hii.”
Labda ni Zerubabeli anayetajwa kwenye Ezr 2:2; 3:8.