Ezra 8:1-36

  • Orodha ya wale waliorudi pamoja na Ezra (1-14)

  • Maandalizi ya safari (15-30)

  • Kuondoka Babiloni na kufika Yerusalemu (31-36)

8  Basi hawa ndio waliokuwa viongozi wa koo* na hii ndiyo orodha ya ukoo wa wale waliopanda pamoja nami kutoka Babiloni wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:+  ukoo wa wana wa Finehasi,+ Gershomu; wa wana wa Ithamari,+ Danieli; wa wana wa Daudi, Hatushi;  wa wana wa Shekania, wa wana wa Paroshi, Zekaria, na pamoja naye kulikuwa na wanaume 150 walioandikishwa;  wa wana wa Pahath-moabu,+ Elieho-enai mwana wa Zeraya, na wanaume 200 pamoja naye;  wa wana wa Zatu,+ Shekania mwana wa Yahazieli, na wanaume 300 pamoja naye;  wa wana wa Adini,+ Ebedi mwana wa Yonathani, na wanaume 50 pamoja naye;  wa wana wa Elamu,+ Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;  wa wana wa Shefatia,+ Zebadia mwana wa Mikaeli, na wanaume 80 pamoja naye;  wa wana wa Yoabu, Obadia mwana wa Yehieli, na wanaume 218 pamoja naye; 10  wa wana wa Bani, Shelomithi mwana wa Yosifia, na wanaume 160 pamoja naye; 11  wa wana wa Bebai,+ Zekaria mwana wa Bebai, na wanaume 28 pamoja naye; 12  wa wana wa Azgadi,+ Yohanani mwana wa Hakatani, na wanaume 110 pamoja naye; 13  wa wana wa Adonikamu,+ wale waliokuwa wa mwisho, haya ndiyo majina yao: Elifeleti, Yeieli, na Shemaya, na wanaume 60 pamoja nao; 14  na wa wana wa Bigvai,+ Uthai na Zabudu, na wanaume 70 pamoja nao. 15  Nikawakusanya kwenye mto unaoelekea Ahava;+ nasi tukapiga kambi hapo siku tatu. Lakini nilipowakagua watu na makuhani, sikupata Mlawi hata mmoja. 16  Kwa hiyo nikawatuma wajumbe wawaite Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria, na Meshulamu, waliokuwa viongozi, na Yoyaribu na Elnathani, waliokuwa walimu. 17  Kisha nikawapa amri kuhusu Ido kiongozi wa Kasifia. Nikawaagiza wamwambie Ido na ndugu zake, watumishi wa hekaluni* waliokuwa huko Kasifia, watuletee wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu. 18  Kwa kuwa mkono mwema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea mwanamume mwenye busara kutoka kwa wana wa Mali+ mjukuu wa Lawi mwana wa Israeli, aliyeitwa Sherebia,+ na wanawe na ndugu zake, wanaume 18; 19  na Hashabia, na pamoja naye Yeshaya kutoka kwa Wamerari,+ ndugu zake na wana wao, wanaume 20. 20  Na kulikuwa na watumishi wa hekaluni* 220, ambao Daudi na wakuu walikuwa wamewatoa kwa ajili ya utumishi wa Walawi, wote walikuwa wametajwa kwa majina. 21  Kisha nikatangaza kwamba watu wafunge hapo kwenye mto Ahava, ili tujinyenyekeze mbele za Mungu wetu, na kumwomba atuongoze katika safari yetu, sisi na watoto wetu na mali zetu zote. 22  Niliona aibu kumwomba mfalme wanajeshi na wapanda farasi watulinde dhidi ya maadui njiani, kwa sababu tulikuwa tumemwambia mfalme: “Mkono mwema wa Mungu wetu uko juu ya wale wote wanaomtafuta,+ lakini nguvu zake na hasira yake iko dhidi ya wote wanaomwacha.”+ 23  Basi tukafunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hilo, naye akasikiliza maombi yetu.+ 24  Kisha nikachagua wakuu 12 wa makuhani, yaani, Sherebia na Hashabia,+ pamoja na kumi kati ya ndugu zao. 25  Nikawapimia fedha na dhahabu na vyombo, mchango ambao mfalme na washauri wake na wakuu wake na Waisraeli wote waliokuwa hapo walitoa kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.+ 26  Basi nikapima na kuwakabidhi talanta 650 za fedha,* vyombo 100 vya fedha vyenye thamani ya talanta mbili, na talanta 100 za dhahabu, 27  mabakuli madogo 20 ya dhahabu yenye thamani ya dariki 1,000,* na vyombo viwili vya shaba bora, nyekundu inayong’aa, inayotamanika kama dhahabu. 28  Kisha nikawaambia: “Ninyi ni watakatifu kwa Yehova,+ na vyombo hivi ni vitakatifu, na fedha na dhahabu hii ni matoleo ya hiari kwa Yehova Mungu wa mababu zenu. 29  Mvilinde kwa makini hadi mtakapovipima mbele ya wakuu wa makuhani na Walawi na wakuu wa koo za Waisraeli huko Yerusalemu,+ katika vyumba vya* nyumba ya Yehova.” 30  Makuhani na Walawi wakapokea fedha na dhahabu na vyombo walivyopimiwa, ili wavilete Yerusalemu kwenye nyumba ya Mungu wetu. 31  Mwishowe tukaondoka kwenye mto Ahava+ siku ya 12 ya mwezi wa kwanza+ na kuelekea Yerusalemu, na mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye akatuokoa kutoka mikononi mwa maadui na wavamizi njiani. 32  Basi tukafika Yerusalemu+ na kukaa huko siku tatu. 33  Kisha siku ya nne tukapima ile fedha na dhahabu na vyombo katika nyumba ya Mungu wetu,+ tukamkabidhi Meremothi+ mwana wa kuhani Uriya, aliyekuwa pamoja na Eleazari mwana wa Finehasi, pamoja na Walawi Yozabadi+ mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.+ 34  Kila kitu kilihesabiwa na kupimwa, na uzito wote ukaandikwa. 35  Wale waliotoka uhamishoni, waliokuwa utekwani, wakamtolea Mungu wa Israeli dhabihu za kuteketezwa, ng’ombe dume 12+ kwa ajili ya Waisraeli wote, kondoo dume 96,+ wanakondoo dume 77, mbuzi dume 12+ kwa ajili ya dhabihu ya dhambi; hizo zote zilikuwa dhabihu za kuteketezwa zilizotolewa kwa Yehova.+ 36  Kisha tukawapa maliwali* wa mfalme+ na magavana waliokuwa Ng’ambo ya Mto*+ maagizo ya mfalme, nao wakawategemeza watu na nyumba ya Mungu wa kweli.+

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Talanta ilikuwa sawa na kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Dariki ilikuwa sarafu ya dhahabu ya Waajemi. Angalia Nyongeza B14.
Au “majumba ya kulia chakula ya.”
Cheo kinachomaanisha “walinzi wa milki,” hapa cheo hicho kinawahusu magavana wa mikoa ya Milki ya Uajemi.
Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”