Kwa Filemoni 1:1-25

  • Salamu (1-3)

  • Upendo na imani ya Filemoni (4-7)

  • Paulo amsihi Filemoni kwa ajili ya Onesimo (8-22)

  • Salamu za mwisho (23-25)

 Paulo, mfungwa+ kwa ajili ya Kristo Yesu, na Timotheo+ ndugu yetu, kwa Filemoni mfanyakazi mwenzetu mpendwa,  na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipo+ mwanajeshi mwenzetu, na kwa kutaniko lililo katika nyumba yako:+  Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.  Sikuzote ninamshukuru Mungu wangu ninapokutaja katika sala zangu,+  ninapoendelea kusikia kuhusu imani na upendo wako kwa* Bwana Yesu na kwa* watakatifu wote.  Ninasali kwamba imani unayoshiriki na wengine ikuchochee kutambua kila jambo jema tulilo nalo kupitia Kristo.  Kwa maana nilipata shangwe nyingi na faraja niliposikia kuhusu upendo wako, kwa sababu wewe ndugu umeburudisha mioyo ya watakatifu.*  Kwa sababu hiyo, ingawa nina uhuru mkubwa wa kusema kuhusiana na Kristo wa kukuagiza ufanye jambo linalofaa,  ni afadhali nikusihi kwa msingi wa upendo, kwa kuwa mimi Paulo ni mwanamume mzee, ndiyo, sasa pia ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu. 10  Ninakusihi kwa ajili ya mwanangu Onesimo,+ ambaye nimekuwa baba yake+ nikiwa gerezani.* 11  Zamani hakukufaa kitu, lakini sasa ni mwenye faida kwako na kwangu pia. 12  Ninamrudisha kwako, ndiyo yeye, moyo wangu mwenyewe.* 13  Ningependa akae nami hapa, ili achukue nafasi yako katika kunihudumia nikiwa nimefungwa kwa ajili ya habari njema.+ 14  Lakini sitaki kufanya jambo lolote bila ruhusa yako, ili ufanye tendo lako jema kwa hiari, bali si kwa kulazimishwa.+ 15  Kwa kweli, labda ndiyo sababu alitoroka kwa muda mfupi,* ili arudi kwako milele, 16  si akiwa mtumwa tena,+ bali zaidi ya mtumwa, akiwa ndugu mpendwa,+ hasa kwangu, lakini hata zaidi kwako katika mwili na katika Bwana. 17  Kwa hiyo, ikiwa unaniona mimi kuwa rafiki yako,* mpokee kwa fadhili jinsi ambavyo ungenipokea mimi. 18  Zaidi ya hayo, ikiwa alikukosea au ana deni lako, basi nidai mimi. 19  Mimi Paulo ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: Nitakulipa—sihitaji kukukumbusha kwamba hata wewe una deni langu, yaani, uhai wako mwenyewe. 20  Ndiyo, ndugu, ninaomba unisaidie jambo hili katika Bwana; burudisha moyo wangu* kuhusiana na Kristo. 21  Ninakuandikia nikiwa na uhakika kwamba utakubali, nikijua utafanya hata zaidi ya jambo ninalokuomba. 22  Lakini pamoja na hayo, pia nitayarishie makao, kwa maana ninatumaini kwamba kupitia sala zenu nitarudishwa kwenu.*+ 23  Epafra+ mfungwa mwenzangu katika muungano na Kristo Yesu anakusalimu, 24  pia wafanyakazi wenzangu Marko, Aristarko,+ Dema,+ na Luka.+ 25  Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na ziwe na roho mnayoonyesha.

Maelezo ya Chini

Au “kuelekea”
Au “kuelekea”
Au “upendo mwororo wa watakatifu.”
Tnn., “katika vifungo.”
Au “upendo wangu mwororo.”
Tnn., “saa moja.”
Tnn., “mshiriki wako.”
Au “upendo wangu mwororo.”
Au “nitawekwa huru kwa ajili yenu.”