Habakuki 1:1-17

  • Nabii alilia msaada (1-4)

    • ‘Ee Yehova, mpaka lini?’ (2)

    • “Kwa nini unavumilia ukandamizaji?” (3)

  • Wakaldayo, watumiwa na Mungu kutekeleza hukumu (5-11)

  • Nabii amsihi Yehova (12-17)

    • ‘Mungu wangu, wewe hufi’ (12)

    • ‘Wewe ni safi sana usiweze kutazama uovu’ (13)

1  Tangazo ambalo nabii Habakuki* alipokea katika maono:   Ee Yehova, nililie msaada mpaka lini, lakini wewe hunisikii?+ Nitaomba msaada kwa sababu ya ukatili mpaka lini, lakini huingilii kati?*+   Kwa nini unanifanya nione mambo mabaya? Na kwa nini unavumilia ukandamizaji? Kwa nini uharibifu na ukatili uko mbele yangu? Na kwa nini ugomvi na mizozo inaongezeka?   Kwa hiyo sheria haifanyi kazi,Na haki haitekelezwi kamwe. Kwa maana mwovu amemzingira mwadilifu;Ndiyo sababu haki imepotoshwa.+   “Tazameni miongoni mwa mataifa, kazeni uangalifu! Tazameni kwa mshangao na kustaajabu;Kwa maana jambo fulani litatukia katika siku zenuAmbalo hamtaamini hata mkiambiwa.+   Kwa maana tazama, ninawainua Wakaldayo,+Taifa katili na linalotenda haraka-haraka,Wanasambaa upesi katika maeneo makubwa sana ya duniaIli wachukue kwa nguvu makao ambayo si yao.+   Wanatisha na kuogopesha. Wanaweka sheria* yao wenyewe na mamlaka* yao wenyewe.+   Farasi wao wanakimbia kasi kuliko chui,Nao ni wakali kuliko mbwamwitu wakati wa usiku.+ Farasi wao wa vita hukimbia mbele kwa kasi;Farasi wao hutoka mbali sana. Wanashuka chini kwa kasi kama tai anayekimbilia chakula.+   Wote huja wakikusudia kutenda ukatili.+ Nyuso zao kwa pamoja ni kama upepo wa mashariki,+Nao huchota mateka kama mchanga. 10  Wanawadhihaki wafalmeNa kuwacheka maofisa wakuu.+ Wanaicheka kila ngome;+Wanatengeneza daraja kwa rundo la udongo na kuiteka. 11  Kisha wanasonga mbele kama upepo na kupita humo,Lakini watakuwa na hatia,+Kwa sababu wanasema nguvu zao zinatoka kwa mungu wao.”*+ 12  Je, wewe si wa tangu milele, Ee Yehova?+ Ee Mungu wangu, Mtakatifu wangu, wewe hufi.*+ Ee Yehova, uliwachagua ili watekeleze hukumu;Mwamba wangu,+ uliwaweka ili watekeleze adhabu.*+ 13  Macho yako ni safi sana yasiweze kutazama uovu,Nawe huwezi kuvumilia uovu.+ Basi, kwa nini unawavumilia wenye hila+Na kunyamaza mtu mwovu anapommeza mtu mwadilifu kuliko yeye?+ 14  Kwa nini unamfanya mwanadamu awe kama samaki wa baharini,Kama viumbe wanaotambaa ambao hawana mtawala? 15  Hao wote yeye* huwavua kwa ndoano. Huwakamata kwa wavu wake wa kukokotwa,Naye huwakusanya katika wavu wake wa kuvulia samaki. Ndiyo sababu anashangilia sana.+ 16  Ndiyo sababu anatoa dhabihu kwa ajili ya wavu wake wa kukokotwaNa kutoa dhabihu* kwa ajili ya wavu wake wa kuvulia samaki;Kwa maana nyavu hizo zimemletea utajiri,*Na chakula chake ni bora. 17  Je, ataendelea kutoa samaki katika wavu wake wa kukokotwa?* Je, ataendelea kuyaangamiza mataifa bila huruma?+

Maelezo ya Chini

Huenda jina hili linamaanisha “Kumbatio Changamfu.”
Au “huniokoi.”
Au “haki.”
Au “heshima.”
Au labda, “nguvu zao ni mungu wao.”
Au labda, “sisi hatutakufa.”
Au “wakaripie.”
Yaani, jeshi la Wakaldayo.
Au “kufukiza moshi wa dhabihu.”
Tnn., “Kwa maana kupitia hizo fungu lake limetiwa mafuta mengi.”
Au labda, “kuchomoa upanga wake.”