Habakuki 2:1-20

  • ‘Nitakaa macho kuhusu atakalosema’ (1)

  • Yehova amjibu nabii (2-​20)

    • ‘Endelea kutarajia maono’ (3)

    • Mwadilifu ataishi kwa uaminifu (4)

    • Ole tano kwa Wakaldayo (6-20)

      • Dunia yote itajaa ujuzi kumhusu Yehova (14)

2  Nitaendelea kusimama katika kituo changu cha ulinzi,+ Nami nitasimama juu ya boma. Nitaendelea kukaa macho ili nione atakalosema kupitia kwanguNa lile nitakalojibu nitakapokaripiwa.   Kisha Yehova akanijibu: “Andika maono haya, na uyaandike waziwazi kwenye mabamba,+Ili anayeyasoma kwa sauti, ayasome kwa urahisi.*+   Kwa maana maono hayo bado yatatimia kwa wakati wake uliowekwa,Nayo yanasonga haraka kuelekea mwisho* wake, nayo hayatasema uwongo. Hata yakikawia,* endelea kuyatarajia!*+ Kwa maana hakika yatatimia. Hayatachelewa!   Mwangalie mtu mwenye kiburi;*Hana unyoofu ndani yake. Lakini mwadilifu ataishi kwa uaminifu wake.*+   Kwa kweli, kwa sababu divai ina hila,Mtu mwenye kiburi hatatimiza lengo lake. Hufanya hamu* yake iwe kubwa kama Kaburi;*Yeye ni kama kifo na hawezi kutoshelezwa. Huendelea kuyakusanya mataifa yoteNa kujikusanyia watu wa mataifa yote.+   Je, hao wote hawatasema methali, fumbo, na vitendawili kumshutumu?+ Watasema: ‘Ole wake anayejirundikia vitu visivyo vyake—Mpaka lini?—Na kufanya deni lake mwenyewe liwe kubwa hata zaidi!   Je, wanaokudai hawatainuka kwa ghafla? Wataamka na kukutikisa kwa fujo,Nawe utakuwa kitu cha kuporwa nao.+   Kwa sababu ulipora mataifa mengi,Mataifa mengine yote yatakupora,+Kwa sababu ulimwaga damu ya wanadamuNa kwa sababu ya ukatili ulioitendea dunia,Majiji na wale wanaoishi humo.+   Ole wake anayeitafutia nyumba yake faida ya uovu,Ili aweke kiota chake juu,Aepuke kunaswa na msiba! 10  Umepanga njama ya aibu dhidi ya nyumba yako. Kwa kuyaangamiza mataifa mengi unatenda dhambi dhidi yako mwenyewe.*+ 11  Kwa maana jiwe litapaza sauti kutoka ukutani,Na kutoka kwenye mbao za paa, boriti italijibu jiwe hilo. 12  Ole wake anayejenga jiji kwa umwagaji wa damu,Na kuusimamisha mji kwa ukosefu wa uadilifu! 13  Tazama! Je, si Yehova wa majeshi anayesababisha mataifa yafanye kazi kwa bidii ili kuulisha moto,Na kusababisha mataifa yajichoshe bure?+ 14  Kwa maana dunia itajaa ujuzi wa utukufu wa YehovaKama maji yanavyoifunika bahari.+ 15  Ole wake anayewapa wenzake kinywaji,Na kuongeza ghadhabu na hasira ndani yake ili awaleweshe,Kusudi atazame uchi wao! 16  Utajaa kabisa aibu badala ya utukufu. Wewe pia—kunywa na kufunua hali yako ya kutotahiriwa.* Kikombe kilicho kwenye mkono wa kuume wa Yehova kitazunguka na kufika kwako,+Na fedheha itafunika kabisa utukufu wako; 17  Kwa sababu ukatili ulioitendea Lebanoni utakufunika,Na maangamizi yaliyowatisha wanyama yatakujia,Kwa sababu ulimwaga damu ya wanadamuNa kwa sababu ya ukatili ulioitendea dunia,Uliyoyatendea majiji na wale wanaoishi humo.+ 18  Sanamu ya kuchongwa ina faida ganiNa mtu ndiye aliyeichonga? Sanamu ya chuma* na mwalimu wa uwongo ana faida gani,Hata ingawa yule aliyeitengeneza anaitumaini,Akitengeneza miungu ya ubatili ambayo haiwezi kuongea?+ 19  Ole wake anayekiambia kipande cha ubao, “Amka!” Au anayeliambia jiwe lisiloweza kuongea, “Amka! Tufundishe!” Tazama! Sanamu hiyo imefunikwa kwa dhahabu na fedha,+Nayo haina pumzi yoyote ndani yake.+ 20  Lakini Yehova yuko katika hekalu lake takatifu.+ Dunia yote na inyamaze mbele zake!’”+

Maelezo ya Chini

Au “kwa ufasaha.”
Au “utimizo.”
Au “Hata ikionekana kwamba yanakawia.”
Au “kuyangojea kwa hamu!”
Au “Tazama! Nafsi yake imefutuka.
Au labda, “imani yake; itikadi yake.”
Au “nafsi.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “dhidi ya nafsi yako.”
Au labda, “na kupepesuka.”
Au “sanamu ya kuyeyushwa.”