Habakuki 3:1-19

  • Nabii asali ili Yehova achukue hatua (1-19)

    • Mungu atawaokoa watiwa-mafuta wake (13)

    • Nitashangilia katika Yehova (17, 18)

3  Sala ya nabii Habakuki, aliyoitoa kama nyimbo za huzuni:*   Ee Yehova, nimesikia habari kukuhusu. Ninaogopa matendo yako, Ee Yehova. Uyafufue kati ya ile miaka!* Uyafanye yajulikane kati ya hiyo miaka.* Nawe ukumbuke kuonyesha rehema wakati wa msukosuko.+   Mungu alikuja kutoka Temani,Yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani.+ (Sela)* Utukufu wake ulifunika mbingu;+Na dunia ikajaa sifa yake.   Aling’aa kama nuru.+ Miale miwili ilimweka kutoka mkononi mwake,Ambamo nguvu zake zilikuwa zimefichika.   Ugonjwa hatari ulitangulia mbele zake,+Na homa kali ilimfuata miguuni.   Alisimama tuli na kuitikisa dunia.+ Alitazama mara moja tu, akayafanya mataifa yaruke.+ Milima ya milele ikavunjwavunjwa,Na vilima vya kale vikainama chini.+ Vijia vya zamani za kale ni vyake.   Niliona taabu katika mahema ya Kushani. Vitambaa vya mahema ya nchi ya Midiani vilitetemeka.+   Je, umeikasirikia mito, Ee Yehova,Je, hasira yako inawaka dhidi ya mito? Au unaikasirikia vikali bahari?+ Kwa sababu ulipanda farasi wako;+Magari yako ya vita yalishinda.*+   Upinde wako umefunuliwa na uko tayari. Fito zimepewa* kazi kwa kiapo.* (Sela) Unaipasua dunia kwa mito. 10  Milima ilipindapinda kwa maumivu ilipokuona.+ Mvua kubwa ilinyesha nchini. Kilindi cha maji kilinguruma kwa sauti yake.+ Kikainua mikono yake juu. 11  Jua na mwezi vilisimama tuli kwenye makao yake yaliyo juu sana.+ Mishale yako ilitoka kama nuru.+ Radi ya mkuki wako ilikuwa nyangavu. 12  Ulipiga mwendo duniani kwa ghadhabu. Ukayakanyaga-kanyaga* mataifa kwa hasira. 13  Ulitoka ili kuwaokoa watu wako, kumwokoa mtiwa-mafuta wako. Ulimpondaponda kiongozi wa* nyumba ya waovu. Ilifunuliwa wazi kuanzia kwenye msingi hadi juu.* (Sela) 14  Uliwachoma vichwa mashujaa wake kwa silaha* zake mwenyeweWalipoondoka kwa kishindo ili kunitawanya. Walishangilia sana kumnyafua kisiri mtu anayeteseka. 15  Ulivuka bahari kwa farasi wako,Katikati ya mawimbi yaliyoinuka ya maji mengi. 16  Nilisikia nikatetemeka kwa ndani;*Niliposikia sauti hiyo midomo yangu ilitetemeka. Uozo ukaingia mifupani mwangu;+Miguu yangu ikatetemeka. Lakini nangojea kimyakimya ile siku ya taabu,+Kwa sababu inawajia watu wanaotushambulia. 17  Ingawa huenda mtini usichanue,Na huenda mizabibu isiwe na matunda;Ingawa huenda mizeituni isizae,Na mashamba yasiwe na mazao yoyote;Ingawa huenda mazizi yasiwe na kondoo,Na mabanda yasiwe na ng’ombe; 18  Lakini mimi nitashangilia katika Yehova;Nitakuwa na shangwe katika Mungu wa wokovu wangu.+ 19  Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ni nguvu zangu;+Ataifanya miguu yangu iwe kama ya paaNa kuniwezesha kutembea mahali palipoinuka.+

Maelezo ya Chini

Au “nyimbo za maombolezo.”
Au labda, “wakati wetu!”
Au labda, “wakati wetu!”
Angalia Kamusi.
Au “yalikuwa wokovu.”
Au labda, “Mishale imepewa.”
Au labda, “Viapo vya makabila vimesemwa.”
Tnn., “Ukayapura.”
Tnn., “Ulikipondaponda kichwa cha.”
Tnn., “shingoni.”
Tnn., “fito.”
Tnn., “na tumbo langu likatetemeka.”