Hagai 2:1-23

  • Hekalu la pili kujaa utukufu (1-9)

    • Kutikiswa kwa mataifa yote (7)

    • Kukusanywa kwa vitu vyenye thamani vya mataifa (7)

  • Kujenga upya hekalu kwaleta baraka (10-19)

    • Utakatifu hauwezi kupitishwa kwa mwingine (10-14)

  • Ujumbe kwa Zerubabeli (20-23)

    • “Nitakufanya kuwa kama pete ya muhuri” (23)

2  Katika mwezi wa saba, siku ya 21 ya mwezi huo, neno la Yehova lilikuja kupitia nabii Hagai,+ likisema:  “Tafadhali muulize hivi Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli, gavana wa Yuda,+ na Yoshua+ mwana wa Yehosadaki,+ kuhani mkuu, na watu wengine wote:  ‘Ni nani aliyebaki miongoni mwenu ambaye aliiona nyumba hii* katika utukufu wake wa mwanzoni?+ Sasa mnaionaje? Je, hamwoni kwamba ni duni ikilinganishwa na ilivyokuwa?’+  “‘Lakini sasa jipe moyo Zerubabeli,’ asema Yehova, ‘jipe moyo Yoshua mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu.’ “‘Nanyi watu wote wa nchi, jipeni moyo,’+ asema Yehova, ‘na mfanye kazi.’ “‘Kwa maana niko pamoja nanyi,’+ asema Yehova wa majeshi.  ‘Kumbukeni ahadi niliyowapa mlipotoka Misri,+ na roho yangu bado imo miongoni mwenu.*+ Msiogope.’”+  “Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Kwa mara nyingine tena—baada ya muda mfupi—nitatikisa mbingu na dunia na bahari na nchi kavu.’+  “‘Nami nitayatikisa mataifa yote, na vitu vyenye thamani* vya mataifa yote vitaingia katika nyumba hii;+ nami nitaijaza nyumba hii utukufu,’+ asema Yehova wa majeshi.  “‘Fedha ni yangu, na dhahabu ni yangu,’ asema Yehova wa majeshi.  “‘Utukufu wa wakati ujao wa nyumba hii utakuwa mkubwa zaidi kuliko ule wa mwanzoni,’+ asema Yehova wa majeshi. “‘Na mahali hapa nitawapa amani,’+ asema Yehova wa majeshi.” 10  Katika siku ya 24 ya mwezi wa 9, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yehova lilimjia nabii Hagai,+ likisema: 11  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Tafadhali, waulize hivi makuhani kuhusu sheria:+ 12  “Mtu akibeba nyama takatifu ndani ya upindo wa vazi lake, na vazi lake liguse mkate au mchuzi au divai au mafuta au chakula cha aina yoyote, je, kitakuwa kitakatifu?”’” Makuhani wakajibu: “Hapana!” 13  Kisha Hagai akawauliza: “Mtu asiye safi kwa sababu ya kugusa maiti,* akigusa chochote kati ya vitu hivyo, je, kitu hicho kitakuwa kichafu?”+ Makuhani wakajibu: “Kitakuwa kichafu.” 14  Basi Hagai akasema: “‘Hivyo ndivyo watu hawa walivyo, na hivyo ndivyo taifa hili lilivyo mbele zangu,’ asema Yehova, ‘na hivyo ndivyo kazi yote ya mikono yao ilivyo; chochote wanachotoa huko ni kichafu.’ 15  “‘Lakini sasa, tafadhali, kazeni moyo wenu juu ya* jambo hili kuanzia leo na kuendelea: Kabla jiwe halijawekwa juu ya jiwe katika hekalu la Yehova,+ 16  hali ilikuwaje wakati huo? Mtu alipoenda kwenye rundo la nafaka akitarajia kupata vipimo 20, alipata vipimo 10 tu; na mtu alipoenda kwenye mtungi wa kushinikizia divai kuchota vipimo 50 kutoka kwenye pipa la divai, alipata vipimo 20 tu;+ 17  niliwapiga ninyi—kazi zote za mikono yenu—kwa upepo unaochoma na kuvu+ na mvua ya mawe, lakini hakuna hata mmoja wenu aliyenirudia,’ asema Yehova. 18  “‘Tafadhali, kazeni moyo wenu juu ya* jambo hili kuanzia leo na kuendelea, kuanzia siku ya 24 ya mwezi wa 9, kuanzia siku ambayo msingi wa hekalu la Yehova uliwekwa;+ kazeni moyo wenu juu ya jambo hili: 19  Je, bado kuna mbegu katika ghala?*+ Mzabibu, mtini, mkomamanga, na mzeituni—haijazaa matunda, au je, imezaa? Kuanzia leo nitawaletea baraka.’”+ 20  Neno la Yehova likamjia Hagai mara ya pili katika siku ya 24 ya mwezi huo,+ likisema: 21  “Mwambie Zerubabeli, gavana wa Yuda, ‘Nitazitikisa mbingu na dunia.+ 22  Nitapindua kiti cha ufalme cha falme na kuharibu kabisa nguvu za falme za mataifa;+ nami nitayapindua magari ya vita na wale wanaoyaendesha,+ na farasi na wapanda farasi watauawa, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.’” 23  “‘Siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘nitakuchukua, mtumishi wangu Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli,’+ asema Yehova, ‘nitakufanya kuwa kama pete ya muhuri, kwa sababu nimekuchagua wewe,’ asema Yehova wa majeshi.”

Maelezo ya Chini

Au “hekalu hili.”
Au labda, “na roho yangu ilipokuwa ikisimama miongoni mwenu.”
Au “kutamanika.”
Au “nafsi iliyokufa.” Angalia Kamusi.
Au “fikirieni kwa makini.”
Au “fikirieni kwa makini.”
Au “shimo la nafaka?”