Hesabu 1:1-54

  • Wanaume waandikishwa jeshini (1-46)

  • Walawi hawakuandikishwa jeshini (47-51)

  • Kambi yapangwa kwa utaratibu (52-54)

1  Na Yehova akazungumza na Musa katika nyika ya Sinai,+ kwenye hema la mkutano,+ siku ya kwanza ya mwezi wa pili katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchini Misri.+ Akamwambia:  “Wahesabu+ Waisraeli wote,* kila mmoja wao* kulingana na familia yake, kulingana na ukoo wake,* orodhesha majina ya wanaume wote.  Wewe na Haruni mnapaswa kuwaandikisha watu wote wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi+ wanaoweza kutumikia katika jeshi la Israeli, kulingana na vikosi vyao.*  “Mchukueni mwanamume mmoja kutoka katika kila kabila, kila mmoja wao anapaswa kuwa kiongozi wa ukoo wake.*+  Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia ninyi: kutoka kabila la Rubeni, Elisuri+ mwana wa Shedeuri;  kabila la Simeoni, Shelumieli+ mwana wa Zurishadai;  kabila la Yuda, Nashoni+ mwana wa Aminadabu;  kabila la Isakari, Nethaneli+ mwana wa Zuari;  kabila la Zabuloni, Eliabu+ mwana wa Heloni; 10  wana wa Yosefu: kabila la Efraimu,+ Elishama mwana wa Amihudi; kabila la Manase, Gamalieli mwana wa Pedazuri; 11  kabila la Benjamini, Abidani+ mwana wa Gidioni; 12  kabila la Dani, Ahiezeri+ mwana wa Amishadai; 13  kabila la Asheri, Pagieli+ mwana wa Okrani; 14  kabila la Gadi, Eliasafu+ mwana wa Deueli; 15  kabila la Naftali, Ahira+ mwana wa Enani. 16  Hao ndio waliochaguliwa miongoni mwa Waisraeli. Hao ndio wakuu+ wa makabila ya baba zao, viongozi wa maelfu katika Israeli.”+ 17  Basi Musa na Haruni wakawachukua wanaume hao waliotajwa majina. 18  Wakawakusanya Waisraeli wote siku ya kwanza ya mwezi wa pili, ili kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi aandikishwe kulingana na jina lake, familia yake, na ukoo wake,*+ 19  kama Yehova alivyomwamuru Musa. Basi akawaandikisha katika nyika ya Sinai.+ 20  Wana wa Rubeni, wazao wa mzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 21  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Rubeni walikuwa 46,500. 22  Wazao wa Simeoni+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 23  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Simeoni walikuwa 59,300. 24  Wazao wa Gadi+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 25  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Gadi walikuwa 45,650. 26  Wazao wa Yuda+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 27  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Yuda walikuwa 74,600. 28  Wazao wa Isakari+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 29  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Isakari walikuwa 54,400. 30  Wazao wa Zabuloni+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 31  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Zabuloni walikuwa 57,400. 32  Wazao wa Yosefu kupitia Efraimu+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 33  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Efraimu walikuwa 40,500. 34  Wazao wa Manase+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 35  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Manase walikuwa 32,200. 36  Wazao wa Benjamini+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 37  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Benjamini walikuwa 35,400. 38  Wazao wa Dani+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 39  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Dani walikuwa 62,700. 40  Wazao wa Asheri+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 41  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Asheri walikuwa 41,500. 42  Wazao wa Naftali+ waliorodheshwa kulingana na majina yao, familia zao, na ukoo wao.* Kila mwanamume mwenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambaye angeweza kutumikia katika jeshi alihesabiwa, 43  wale walioandikishwa kutoka katika kabila la Naftali walikuwa 53,400. 44  Hao ndio walioandikishwa na Musa na Haruni na wale wakuu 12 wa Israeli, kila mmoja wao aliwakilisha ukoo wake.* 45  Waisraeli wote wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi ambao wangeweza kutumikia katika jeshi la Israeli waliandikishwa kulingana na ukoo wao,* 46  watu wote walioandikishwa walikuwa 603,550.+ 47  Lakini Walawi+ hawakuandikishwa pamoja nao, kulingana na makabila ya baba zao.+ 48  Basi Yehova akamwambia Musa: 49  “Ni kabila la Lawi tu ambalo hutaliandikisha, nawe hupaswi kuwahesabu pamoja na Waisraeli wengine.+ 50  Unapaswa kuwaweka rasmi Walawi wasimamie hema la Ushahidi+ na vyombo vyake vyote na kila kitu kilichomo.+ Watabeba hema hilo na vyombo vyake vyote,+ nao watalitunza+ na kupiga kambi kulizunguka.+ 51  Wakati wowote hema hilo linapohamishwa, Walawi ndio wanaopaswa kulifungua;+ na wakati linaposimamishwa, Walawi ndio wanaopaswa kulisimamisha; na mtu yeyote asiye na idhini* akilikaribia anapaswa kuuawa.+ 52  “Kila Mwisraeli anapaswa kupiga hema lake katika kambi aliyogawiwa, kila mwanamume kulingana na kundi lake la makabila matatu,*+ kulingana na kikosi chake.* 53  Walawi wanapaswa kupiga kambi kuzunguka hema la Ushahidi, ili hasira yangu isiwawakie Waisraeli;+ na lazima Walawi wawajibike kulitunza* hema la Ushahidi.”+ 54  Waisraeli walifanya mambo yote ambayo Yehova alimwamuru Musa. Hivyo ndivyo walivyofanya.

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “kila kichwa.”
Tnn., “wana wote wa Israeli.”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “mgeni yeyote,” yaani, mtu ambaye si wa familia ya Haruni.
Au “alama yake.”
Tnn., “jeshi lake.”
Au “kulilinda; kutumikia katika.”