Hesabu 13:1-33

  • Wapelelezi 12 watumwa Kanaani (1-24)

  • Wapelelezi kumi waleta habari mbaya (25-33)

13  Yehova akamwambia Musa:  “Watume wanaume wakaipeleleze nchi ya Kanaani ninayowapa Waisraeli. Mtume mwanamume mmoja kutoka katika kila kabila la baba yake, kila mmoja wao anapaswa kuwa mkuu+ katika kabila lake.”+  Basi Musa akawatuma kutoka katika nyika ya Parani+ kama Yehova alivyomwagiza. Wanaume hao wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.  Haya ndiyo majina yao: kutoka katika kabila la Rubeni, Shamua mwana wa Zakuri;  kutoka katika kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;  kutoka katika kabila la Yuda, Kalebu+ mwana wa Yefune;  kutoka katika kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;  kutoka katika kabila la Efraimu, Hoshea+ mwana wa Nuni;  kutoka katika kabila la Benjamini, Palti mwana wa Rafu; 10  kutoka katika kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi; 11  kutoka katika kabila la Yosefu,+ kwa ajili ya kabila la Manase,+ Gadi mwana wa Susi; 12  kutoka katika kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali; 13  kutoka katika kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli; 14  kutoka katika kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofsi; 15  kutoka katika kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki. 16  Hayo ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kuipeleleza nchi. Musa alimpa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.*+ 17  Musa alipokuwa akiwatuma kuipeleleza nchi ya Kanaani, aliwaambia: “Pandeni mwingie Negebu, na kwenda juu kwenye eneo lenye milima.+ 18  Chunguzeni mwone nchi hiyo ilivyo+ na kama watu wanaoishi humo ni wenye nguvu au dhaifu, wengi au wachache, 19  na kama nchi hiyo ni nzuri au ni mbaya na kama majiji wanamoishi ni kambi au ni ngome. 20  Chunguzeni ikiwa ni nchi tajiri au maskini,+ ina miti au haina. Ni lazima muwe jasiri+ na kuchukua baadhi ya matunda ya nchi hiyo.” Ulikuwa wakati wa kuiva kwa zabibu za kwanza.+ 21  Basi wakaenda na kuipeleleza nchi kuanzia nyika ya Zini+ hadi Rehobu+ mpaka Lebo-hamathi.*+ 22  Walipopanda na kuingia Negebu, walifika Hebroni,+ ambako Ahimani, Sheshai, na Talmai,+ wazao wa Anaki+ waliishi. Sasa, Jiji la Hebroni lilijengwa miaka saba kabla ya jiji la Soani lililoko Misri. 23  Walipofika kwenye Bonde la Eshkoli,+ walikata tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, na wanaume wawili wakalibeba kwa ufito pamoja na makomamanga kadhaa na tini.+ 24  Wakapaita mahali hapo Bonde la Eshkoli*+ kwa sababu ya kishada ambacho Waisraeli walikata kutoka huko. 25  Baada ya kuipeleleza nchi kwa siku 40,+ wanaume hao walirudi. 26  Walirudi kwa Musa, Haruni, na Waisraeli wote katika nyika ya Parani, huko Kadeshi.+ Wakawaletea habari Waisraeli wote na kuwaonyesha matunda ya nchi hiyo. 27  Hivi ndivyo walivyomwambia Musa: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, na kwa kweli inatiririka maziwa na asali,+ na haya ndiyo matunda yake.+ 28  Lakini watu wanaoishi katika nchi hiyo wana nguvu, na majiji yao yenye ngome ni makubwa sana. Tuliona pia wazao wa Anaki huko.+ 29  Waamaleki+ wanaishi katika nchi ya Negebu,+ nao Wahiti, Wayebusi,+ na Waamori+ wanaishi katika eneo lenye milima, na Wakanaani+ wanaishi karibu na bahari+ na kwenye kingo za Yordani.” 30  Kisha Kalebu akajaribu kuwatuliza watu waliosimama mbele ya Musa kwa kuwaambia: “Twendeni mara moja, na bila shaka tutaimiliki, kwa maana kwa hakika tunaweza kuishinda.”+ 31  Lakini wanaume waliopanda huko pamoja naye wakasema: “Hatuwezi kwenda kupigana na watu hao, kwa sababu wana nguvu kuliko sisi.”+ 32  Nao wakaendelea kuwapa Waisraeli habari mbaya+ kuhusu nchi waliyoipeleleza, wakisema: “Nchi tuliyoenda kuipeleleza ni nchi inayowameza wakaaji wake, na watu wote tuliowaona huko ni wakubwa isivyo kawaida.+ 33  Na huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki,+ wazao wa Wanefili, tulijiona kuwa kama panzi mbele yao, na ndivyo walivyotuona.”

Maelezo ya Chini

Au “Yehoshua,” linalomaanisha Yehova Ni Wokovu.
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Maana yake “Kishada cha Zabibu.”