Hesabu 17:1-13

  • Fimbo ya Haruni iliyochanua maua yatumika kuwa onyo (1-13)

17  Kisha Yehova akamwambia Musa,  “Zungumza na Waisraeli na uchukue kutoka kwao fimbo moja kwa ajili ya kila kabila, kutoka kwa wakuu wa kila kabila,+ jumla ya fimbo 12. Andika jina la kila mmoja wao kwenye fimbo yake.  Unapaswa kuandika jina la Haruni kwenye fimbo ya Lawi, kwa sababu kuna fimbo moja kwa ajili ya kiongozi wa kila kabila.  Ziweke fimbo hizo ndani ya hema la mkutano mbele ya sanduku la Ushahidi,+ mahali ambapo mimi hukutokea kwa ukawaida.+  Na fimbo ya mtu nitakayemchagua+ itachipua, nami nitakomesha manung’uniko ya Waisraeli dhidi yangu,+ ambayo pia wanakunung’unikia.”+  Basi Musa akazungumza na Waisraeli, na wakuu wao wote wakampa fimbo—fimbo moja kutoka kwa kila mkuu wa kabila, fimbo 12—nayo fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao.  Kisha Musa akaziweka fimbo hizo mbele za Yehova katika hema la Ushahidi.  Siku iliyofuata, Musa alipoingia katika hema la Ushahidi, aliona fimbo ya Haruni ya kabila la Lawi imetokeza matumba nayo ilikuwa ikichanua maua na kuzaa matunda ya lozi yaliyoiva.  Kisha Musa akazichukua fimbo zote kutoka mbele za Yehova na kuzileta mbele ya Waisraeli wote. Wakazitazama na kila mkuu akachukua fimbo yake. 10  Halafu Yehova akamwambia Musa, “Irudishe fimbo ya Haruni+ mbele ya sanduku la Ushahidi ili iwekwe kuwa onyo+ kwa wana wa kuasi,+ ili manung’uniko yao dhidi yangu yakome na ili wasife.” 11  Mara moja Musa akafanya kama Yehova alivyomwamuru. Hivyo ndivyo alivyofanya. 12  Kisha Waisraeli wakamwambia Musa, “Sasa tutakufa, bila shaka tutaangamia, sisi sote tutaangamia! 13  Hata mtu yeyote atakayekaribia hema la Yehova la ibada atakufa!+ Je, ni lazima sote tufe kwa njia hiyo?”+

Maelezo ya Chini