Hesabu 21:1-35

  • Mfalme wa Aradi ashindwa (1-3)

  • Nyoka wa shaba (4-9)

  • Waisraeli wazunguka Moabu (10-20)

  • Mfalme Sihoni wa Waamori ashindwa (21-30)

  • Mfalme Ogu wa Waamori ashindwa (31-35)

21  Mfalme Mkanaani wa Aradi,+ aliyeishi Negebu, aliposikia kwamba Waisraeli walipitia njia ya Atharimu, aliwashambulia na kuwateka baadhi yao.  Kwa hiyo Waisraeli wakamwekea Yehova nadhiri hii: “Ukiwatia watu hawa mikononi mwetu, bila shaka tutayaangamiza majiji yao.”  Kwa hiyo Yehova akawasikiliza Waisraeli na kuwatia Wakanaani mikononi mwao, Waisraeli wakawaangamiza pamoja na majiji yao. Basi wakapaita mahali hapo Horma.*+  Walipoendelea na safari yao kutoka Mlima Hori+ kupitia njia ya Bahari Nyekundu ili kuizunguka nchi ya Edomu,+ watu wakachoshwa na safari.  Na watu wakaendelea kumnung’unikia Mungu na Musa,+ wakisema: “Kwa nini mmetutoa Misri ili tufe nyikani? Hakuna chakula wala maji,+ nasi tumeuchukia mkate huu unaochukiza.”+  Basi Yehova akaleta nyoka wenye sumu* katikati ya watu, na nyoka hao wakawauma sana hivi kwamba Waisraeli wengi wakafa.+  Kwa hiyo watu wakaja kwa Musa na kumwambia: “Tumetenda dhambi kwa kumnung’unikia Yehova na wewe pia.+ Msihi Yehova atuondolee nyoka hawa.” Basi Musa akamsihi Mungu kwa niaba ya watu.+  Kisha Yehova akamwambia Musa: “Tengeneza mfano wa nyoka mwenye sumu na uuweke juu ya nguzo. Mtu yeyote akiumwa na nyoka, ni lazima autazame mfano huo ili aendelee kuishi.”  Mara moja Musa akatengeneza nyoka wa shaba+ na kumweka juu ya nguzo,+ na mtu yeyote aliyeumwa na nyoka na kumtazama nyoka huyo wa shaba, aliendelea kuishi.+ 10  Kisha Waisraeli wakaendelea na safari na kupiga kambi Obothi.+ 11  Halafu wakaondoka Obothi na kupiga kambi Iye-abarimu,+ katika nyika inayoelekeana na Moabu, upande wa mashariki. 12  Kutoka huko wakasafiri na kupiga kambi karibu na Bonde la Zeredi.+ 13  Wakaondoka huko na kupiga kambi katika eneo la Arnoni,+ lililo katika nyika inayoanzia kwenye mpaka wa Waamori, kwa maana eneo la Arnoni ni mpaka wa Moabu, kati ya Wamoabu na Waamori. 14  Ndiyo sababu kitabu cha Vita vya Yehova kinasema kuhusu “Jiji la Vahebu katika eneo la Sufa na mabonde* ya Arnoni, 15  na miteremko ya mabonde, inayofika katika mji wa Ari na kufika kwenye mpaka wa Moabu.” 16  Kisha wakasafiri mpaka Beeri. Ni kwenye kisima hicho ambapo Yehova alimwambia Musa hivi: “Wakusanye watu, niwape maji.” 17  Wakati huo, Waisraeli waliimba wimbo huu: “Bubujika, Ee kisima!—Kiimbieni!* 18  Kisima kilichochimbwa na wakuu, kilichochimbwa na watu mashuhuri,Kwa fimbo ya kiongozi na kwa fimbo zao wenyewe.” Kisha wakatoka nyikani na kwenda Matana, 19  kutoka Matana mpaka Nahalieli, na kutoka Nahalieli mpaka Bamothi.+ 20  Wakatoka Bamothi na kwenda kwenye bonde lililo katika eneo la Moabu,+ juu ya Pisga,+ linaloelekeana na Yeshimoni.*+ 21  Sasa Waisraeli wakawatuma wajumbe wakamwambie hivi Sihoni mfalme wa Waamori:+ 22  “Turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutageuka na kuingia katika mashamba yenu au shamba lolote la mizabibu. Hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutafuata Barabara ya Mfalme mpaka tutakapokuwa tumepita katika eneo lako.”+ 23  Lakini Sihoni hakuwaruhusu Waisraeli wapitie katika eneo lake. Badala yake, Sihoni akawakusanya watu wake wote kwenda kuwashambulia Waisraeli nyikani, akafika Yahazi na kuanza kupigana nao.+ 24  Lakini Waisraeli wakamshinda kwa upanga+ na kumiliki nchi yake+ kuanzia Arnoni+ mpaka Yaboki,+ karibu na Waamoni, kwa sababu jiji la Yazeri+ linapakana na eneo la Waamoni.+ 25  Basi Waisraeli wakachukua majiji hayo yote, wakaanza kuishi katika majiji yote ya Waamori,+ huko Heshboni na miji yake yote. 26  Kwa maana Heshboni lilikuwa jiji la Sihoni, mfalme wa Waamori ambaye alikuwa amepigana na mfalme wa Moabu na kuchukua nchi yake yote mpaka Arnoni. 27  Ndiyo maana watu walitunga shairi hili la dhihaka: “Njooni Heshboni. Jiji la Sihoni na lijengwe na kuimarishwa kabisa. 28  Kwa maana moto ulitoka Heshboni, mwali wa moto ulitoka katika mji wa Sihoni. Umeteketeza jiji la Ari la Moabu, mabwana wa milima ya Arnoni. 29  Ole wako, Moabu! Mtaangamizwa, enyi watu wa Kemoshi!+ Huwafanya wanawe kuwa wakimbizi na binti zake kuwa mateka wa Sihoni, mfalme wa Waamori. 30  Acheni tuwapige mishale;Heshboni litaangamizwa mpaka Diboni;+Acheni tuliharibu kabisa mpaka Nofa;Moto utasambaa mpaka Medeba.”+ 31  Basi Waisraeli wakaanza kuishi katika nchi ya Waamori. 32  Kisha Musa akawatuma watu fulani wakapeleleze Yazeri.+ Wakateka miji yake na kuwafukuza Waamori waliokuwa humo. 33  Halafu wakageuka na kupanda kupitia njia ya Bashani. Ndipo Ogu+ mfalme wa Bashani akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana vita nao huko Edrei.+ 34  Yehova akamwambia Musa: “Usimwogope,+ kwa maana nitamtia mikononi mwako pamoja na watu wake wote na nchi yake,+ nawe utamtendea kama ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, aliyeishi Heshboni.”+ 35  Basi wakaendelea kumshambulia pamoja na wanawe na watu wake wote hivi kwamba hakuna mtu yeyote kati ya watu wake aliyeokoka,+ nao wakaichukua nchi yake.+

Maelezo ya Chini

Maana yake “Kuangamiza.”
Tnn., “wenye moto.”
Au “makorongo.”
Au “Kiitikieni.”
Au labda, “jangwa; nyika.”