Hesabu 24:1-25

  • Maneno ya tatu ya kishairi ya Balaamu (1-11)

  • Maneno ya nne ya kishairi ya Balaamu (12-25)

24  Balaamu alipoona kwamba Yehova alifurahia* kuwabariki Waisraeli, hakwenda tena kutafuta ishara za msiba,+ bali aliugeuza uso wake kutazama nyikani.  Balaamu alipotazama na kuwaona Waisraeli wakiwa wamepiga kambi kulingana na makabila yao,+ roho ya Mungu ikamjia.+  Kisha akasema maneno haya ya kishairi:+ “Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,Na maneno ya mwanamume ambaye macho yake yamefunguliwa,   Maneno ya mtu anayesikia neno la Mungu,Aliyeona maono ya Mweza-Yote,Aliyeinama chini macho yakiwa yamefumbuliwa:+   Mahema yako yanapendeza sana, Ee Yakobo,Makao yako, Ee Israeli!+   Yameenea mbali kama mabonde,+Kama bustani kando ya mto,Kama mimea ya udi iliyopandwa na Yehova,Kama mierezi kando ya maji.   Maji yanaendelea kutiririka kutoka katika ndoo zake mbili za ngozi,Na mbegu yake imepandwa* kando ya maji mengi.+ Mfalme wake+ pia atakuwa mkuu kuliko Agagi,+Na ufalme wake utakwezwa.+   Mungu anamtoa Misri;Yeye ni kama pembe za fahali mwitu kwa Waisraeli. Atayala mataifa, wale wanaomkandamiza,+Na mifupa yao ataitafuna-tafuna, naye atawapasua-pasua kwa mishale yake.   Amejikunyata, amelala chini kama simba,Na kama simba, ni nani anayethubutu kumwamsha? Wale wanaokubariki wamebarikiwa,Na wale wanaokulaani wamelaaniwa.”+ 10  Ndipo Balaki akamkasirikia sana Balaamu. Akapiga makofi kwa dharau na kumwambia Balaamu: “Nilikuita uwalaani maadui wangu,+ badala yake umewabariki mara tatu. 11  Sasa rudi nyumbani mara moja. Nilitaka kukuthawabisha sana,+ lakini Yehova amekunyima thawabu.” 12  Balaamu akamwambia Balaki: “Je, sikuwaambia hivi wajumbe uliowatuma kwangu: 13  ‘Hata Balaki akinipa nyumba yake mwenyewe iliyojaa fedha na dhahabu, siwezi kwa hiari yangu* kukiuka jambo lolote ambalo Yehova ameniagiza nifanye, liwe jambo zuri au baya. Nitasema tu jambo ambalo Yehova ataniambia’?+ 14  Na sasa naenda kwa watu wangu. Njoo nikwambie* mambo ambayo watu hawa watawatendea watu wako wakati ujao.”* 15  Kwa hiyo akasema maneno haya ya kishairi:+ “Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,Na maneno ya mwanamume ambaye macho yake yamefunguliwa,+ 16  Maneno ya mtu anayesikia neno la Mungu,Na yule anayemjua Aliye Juu Zaidi,Aliona maono ya Mweza-YoteAlipokuwa akiinama chini macho yake yakiwa yamefunguliwa: 17  Nitamwona, lakini si sasa;Nitamtazama, lakini si hivi karibuni. Nyota+ itatoka kwa Yakobo,Na fimbo ya ufalme+ itainuka katika Israeli.+ Naye hakika atapasua paji la uso la Moabu+Na fuvu la kichwa la wana wote wa vurugu. 18  Na Edomu itamilikiwa,+Naam, Seiri+ itamilikiwa na maadui wake,+Huku Israeli ikidhihirisha ujasiri wake. 19  Na mzao wa Yakobo atakuwa akishinda,+Naye atamwangamiza yeyote atakayeokoka jijini.” 20  Alipowaona Waamaleki, aliendelea kusema maneno yake ya kishairi: “Amaleki lilikuwa taifa la kwanza,+Lakini mwishowe litaangamia.”+ 21  Alipowaona Wakeni,+ aliendelea kusema maneno yake ya kishairi: “Makao yenu yako salama, yamejengwa juu ya mwamba. 22  Lakini mtu fulani atawateketeza Wakeni.* Ni muda gani unaobaki kabla ya Ashuru kuwachukua mateka?” 23  Akaendelea kusema maneno yake ya kishairi: “Lo! Ni nani atakayeokoka Mungu atakapofanya hivyo? 24  Meli zitatoka pwani ya Kitimu,+Zitashambulia Ashuru,+Na kushambulia Eberi. Lakini wao pia wataangamia* kabisa.” 25  Kisha Balaamu+ akaondoka na kurudi kwake. Balaki pia akaenda zake.

Maelezo ya Chini

Tnn., “lilikuwa jambo jema machoni pa Yehova.”
Au “uzao wake umepandwa.”
Tnn., “kutoka moyoni mwangu.”
Au “nikupe ushauri kuhusu.”
Au “siku za mwisho.”
Tnn., “ataliteketeza Kaini.”
Tnn., “yeye pia ataangamia.”