Hesabu 26:1-65

  • Makabila ya Waisraeli yahesabiwa mara ya pili (1-65)

26  Baada ya pigo hilo,+ Yehova akamwambia hivi Musa na Eleazari mwana wa kuhani Haruni:  “Wahesabuni Waisraeli wote wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi, kulingana na koo zao,* wahesabuni wote wanaoweza kutumikia katika jeshi la Israeli.”+  Basi Musa na kuhani Eleazari+ wakawaambia watu hivi katika jangwa tambarare la Moabu+ karibu na Yordani huko Yeriko:+  “Wahesabuni watu wenye umri wa kuanzia miaka 20 na zaidi, kama Yehova alivyomwamuru Musa.”+ Kwa hiyo Waisraeli waliotoka nchini Misri walikuwa:  Rubeni,+ mzaliwa wa kwanza wa Israeli; wana wa Rubeni+ walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;  kutoka kwa Hezroni, ukoo wa Wahezroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.  Hizo ndizo zilizokuwa koo za Warubeni, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 43,730.+  Mwana wa Palu alikuwa Eliabu.  Na wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani, na Abiramu. Huyu ndiye Dathani na Abiramu, wakuu wa Waisraeli ambao walimpinga Musa+ na Haruni na kujiunga na kikundi cha Kora+ kilichompinga Yehova.+ 10  Kisha dunia ikafunguka* na kuwameza. Lakini Kora alikufa pamoja na watu waliomuunga mkono moto ulipowateketeza watu 250.+ Wakawa onyo kwa wengine.+ 11  Hata hivyo, wana wa Kora hawakufa.+ 12  Wana wa Simeoni+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka kwa Yakini, ukoo wa Wayakini; 13  kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli. 14  Hizo ndizo zilizokuwa koo za Wasimeoni: walikuwa 22,200.+ 15  Wana wa Gadi+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Sefoni, ukoo wa Wasefoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni; 16  kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri; 17  kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli. 18  Hizo ndizo zilizokuwa koo za wana wa Gadi, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 40,500.+ 19  Wana wa Yuda+ walikuwa Eri na Onani.+ Hata hivyo, Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani.+ 20  Na wana wa Yuda kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela,+ ukoo wa Washela; kutoka kwa Perezi,+ ukoo wa Waperezi; kutoka kwa Zera,+ ukoo wa Wazera. 21  Na wana wa Perezi walikuwa: kutoka kwa Hezroni,+ ukoo wa Wahezroni; kutoka kwa Hamuli,+ ukoo wa Wahamuli. 22  Hizo ndizo zilizokuwa koo za Yuda, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 76,500.+ 23  Wana wa Isakari+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola,+ ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuni; 24  kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni. 25  Hizo ndizo zilizokuwa koo za Isakari, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 64,300.+ 26  Wana wa Zabuloni+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yahleeli, ukoo wa Wayahleeli. 27  Hizo ndizo zilizokuwa koo za Wazabuloni, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 60,500.+ 28  Wana wa Yosefu+ kulingana na koo zao walikuwa Manase na Efraimu.+ 29  Wana wa Manase+ walikuwa: kutoka kwa Makiri,+ ukoo wa Wamakiri; naye Makiri alikuwa baba ya Gileadi;+ kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi. 30  Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi: kutoka kwa Yezeri, ukoo wa Wayezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki; 31  kutoka kwa Asrieli, ukoo wa Waasrieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu; 32  kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi. 33  Sasa Selofehadi mwana wa Heferi hakuwa na watoto wa kiume, alikuwa na mabinti tu,+ na majina ya mabinti wa Selofehadi+ ni Mala, Noa, Hogla, Milka, na Tirsa. 34  Hizo ndizo zilizokuwa koo za Manase, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 52,700.+ 35  Hawa ndio waliokuwa wana wa Efraimu+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Shuthela,+ ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani. 36  Na hawa ndio wana wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani. 37  Hizo ndizo zilizokuwa koo za wana wa Efraimu, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 32,500.+ Hao ndio waliokuwa wana wa Yosefu kulingana na koo zao. 38  Wana wa Benjamini+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela,+ ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu; 39  kutoka kwa Shefufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu. 40  Wana wa Bela ni Ardi na Naamani:+ kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani. 41  Hao ndio waliokuwa wana wa Benjamini kulingana na koo zao, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 45,600.+ 42  Hawa ndio waliokuwa wana wa Dani+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizo ndizo zilizokuwa koo za Dani kulingana na wazao wao. 43  Watu walioandikishwa kutoka katika koo zote za Washuhamu walikuwa 64,400.+ 44  Wana wa Asheri+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia; 45  kutoka kwa wana wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli. 46  Binti ya Asheri aliitwa Sera. 47  Hizo ndizo zilizokuwa koo za wana wa Asheri, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 53,400.+ 48  Wana wa Naftali+ kulingana na koo zao walikuwa: kutoka kwa Yahzeeli, ukoo wa Wayahzeeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni; 49  kutoka kwa Yezeri, ukoo wa Wayezeri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu. 50  Hizo ndizo zilizokuwa koo za Naftali kulingana na wazao wao, na watu walioandikishwa kutoka katika koo hizo walikuwa 45,400.+ 51  Wanaume wote Waisraeli walioandikishwa walikuwa 601,730.+ 52  Kisha Yehova akamwambia Musa hivi: 53  “Watu hao wanapaswa kugawiwa urithi wa nchi kulingana na orodha ya majina.*+ 54  Unapaswa kuyapa makundi makubwa urithi mkubwa, na makundi madogo urithi mdogo.+ Kila kundi linapaswa kupewa urithi wake kulingana na idadi ya watu walioorodheshwa. 55  Hata hivyo, nchi inapaswa kugawanywa kwa kura.+ Watu wanapaswa kupokea urithi wao kulingana na majina ya makabila ya baba zao. 56  Kila urithi utagawanywa kwa kura, na makundi makubwa na madogo yatapewa urithi wao.” 57  Sasa hawa ndio Walawi walioandikishwa+ kulingana na koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi,+ ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari. 58  Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni,+ ukoo wa Wahebroni,+ ukoo wa Wamali,+ ukoo wa Wamushi,+ ukoo wa Wakora.+ Kohathi alikuwa baba ya Amramu.+ 59  Na mke wa Amramu alikuwa Yokebedi,+ binti ya Lawi; Yokebedi alizaliwa nchini Misri. Naye alimzalia Amramu, Haruni na Musa na Miriamu dada yao.+ 60  Kisha Haruni akamzaa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.+ 61  Lakini Nadabu na Abihu walikufa kwa sababu ya kumtolea Yehova moto haramu.+ 62  Wanaume wote wenye umri wa kuanzia mwezi mmoja na zaidi walioandikishwa walikuwa 23,000.+ Hawakuandikishwa pamoja na Waisraeli wengine,+ kwa sababu hawakupaswa kupewa urithi miongoni mwa Waisraeli.+ 63  Hao ndio walioandikishwa na Musa na kuhani Eleazari walipowaandikisha Waisraeli katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani huko Yeriko. 64  Lakini hakuna hata mmoja wao aliyeandikishwa na Musa na kuhani Haruni wakati walipowahesabu Waisraeli katika nyika ya Sinai.+ 65  Kwa maana Yehova alikuwa amesema hivi kuwahusu: “Ni lazima wafe nyikani.”+ Kwa hiyo hakuna mwanamume hata mmoja kati yao aliyebaki isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “ikafungua kinywa chake.”
Au “kulingana na idadi ya majina yaliyoorodheshwa.”