Hesabu 29:1-40

  • Taratibu za kutoa dhabihu mbalimbali (1-40)

    • Siku ya kupiga tarumbeta (1-6)

    • Siku ya Kufunika Dhambi (7-11)

    • Sherehe ya Vibanda (12-38)

29  “‘Na siku ya kwanza ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+ Mnapaswa kupiga tarumbeta siku hiyo.+  Mtatoa ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, wanakondoo dume saba wote wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova, wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro,  pamoja na toleo la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya ng’ombe dume, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kondoo dume,  na sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume saba,  na mwanambuzi dume mmoja ili kuwa dhabihu ya dhambi kwa ajili ya kufunika dhambi zenu.  Mtatoa vitu hivyo pamoja na dhabihu ya kuteketezwa ya kila mwezi na toleo lake la nafaka+ na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la nafaka+ na matoleo yake ya kinywaji,+ mkifuata utaratibu wa kawaida wa kutoa dhabihu hizo, ili iwe dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova.  “‘Na siku ya kumi ya mwezi huo wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu,+ nanyi mnapaswa kujitesa.* Hampaswi kufanya kazi yoyote.+  Mtamtoa ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wote wa umri wa mwaka mmoja kuwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayompendeza* Yehova; wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro.+  Mtawatoa pamoja na toleo lao la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya ng’ombe dume, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kondoo dume mmoja, 10  sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume saba, 11  na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya dhambi inayotolewa kwa ajili ya kufunika dhambi+ na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji. 12  “‘Na siku ya 15 ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu, nanyi mnapaswa kumfanyia Yehova sherehe kwa siku saba.+ 13  Mtatoa ng’ombe dume wachanga 13, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja kuwa dhabihu inayochomwa+ kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova; wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro.+ 14  Mtawatoa pamoja na toleo lao la nafaka la unga laini uliochanganywa na mafuta; sehemu tatu za kumi kwa ajili ya kila ng’ombe dume kati ya wale ng’ombe dume 13, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya kila kondoo dume kati ya wale kondoo dume 2, 15  na sehemu ya kumi kwa ajili ya kila mwanakondoo dume kati ya wale wanakondoo dume 14, 16  na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+ 17  “‘Na siku ya pili mtatoa ng’ombe dume wachanga 12, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 18  na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 19  na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji.+ 20  “‘Na siku ya tatu mtatoa ng’ombe dume 11, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 21  na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 22  na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+ 23  “‘Na siku ya nne mtatoa ng’ombe dume 10, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 24  na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 25  na pia mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+ 26  “‘Na siku ya tano mtatoa ng’ombe dume 9, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 27  na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 28  na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+ 29  “‘Na siku ya sita mtatoa ng’ombe dume 8, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 30  na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 31  na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na matoleo yake ya kinywaji.+ 32  “‘Na siku ya saba mtatoa ng’ombe dume 7, kondoo dume 2, na wanakondoo dume 14 wote wa umri wa mwaka mmoja, wanyama wasio na kasoro,+ 33  na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya hao ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 34  na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+ 35  “‘Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.+ 36  Mtatoa ng’ombe dume mmoja, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wote wa mwaka mmoja kuwa dhabihu inayochomwa kwa moto yenye harufu inayompendeza* Yehova, wanyama wote hawapaswi kuwa na kasoro,+ 37  na toleo la nafaka na matoleo ya kinywaji kwa ajili ya huyo ng’ombe dume, kondoo dume, na wanakondoo dume kulingana na idadi yao, mkifuata utaratibu wa kawaida, 38  na pia mbuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi, mbali na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida, pamoja na toleo lake la nafaka na toleo lake la kinywaji.+ 39  “‘Mtamtolea Yehova dhabihu hizo wakati wa sherehe zenu za majira,+ mbali na dhabihu zenu za nadhiri+ na matoleo yenu ya hiari+ yakiwa dhabihu zenu za kuteketezwa;+ na pia matoleo yenu ya nafaka+ na matoleo yenu ya kinywaji+ na dhabihu zenu za ushirika.’”+ 40  Musa aliwaambia Waisraeli mambo yote ambayo Yehova alimwamuru.

Maelezo ya Chini

Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Kwa ujumla inaeleweka kwamba “kujitesa” kunamaanisha kujinyima kwa njia mbalimbali, kutia ndani kufunga.
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”
Au “inayomtuliza.”