Hesabu 7:1-89

  • Matoleo ya kuzindua hema la ibada (1-89)

7  Siku ambayo Musa alimaliza kutengeneza hema la ibada,+ alilitia mafuta+ na kulitakasa pamoja na vyombo vyake vyote, na madhabahu na vyombo vyake vyote.+ Baada ya kuvitia mafuta na kuvitakasa vitu hivyo,+  wakuu wa Israeli,+ viongozi wa koo zao,* wakaleta matoleo. Wakuu hao wa makabila waliosimamia kazi ya kuwaandikisha watu  wakamletea Yehova matoleo yao; walileta magari sita yaliyofunikwa na pia ng’ombe dume 12, gari moja kutoka kwa kila wakuu wawili na ng’ombe dume mmoja kutoka kwa kila mkuu; wakaleta vitu hivyo mbele ya hema la ibada.  Yehova akamwambia Musa:  “Pokea vitu hivyo kutoka kwao, kwa maana vitatumiwa katika utumishi wa hema la mkutano, nawe unapaswa kuwapa Walawi vitu hivyo, utampa kila mmoja kulingana na mahitaji ya kazi yake.”  Basi Musa akapokea magari hayo pamoja na ng’ombe na kuwapa Walawi.  Aliwapa wana wa Gershoni magari mawili na ng’ombe dume wanne kulingana na mahitaji ya kazi yao;+  akawapa wana wa Merari magari manne na ng’ombe dume wanane kulingana na mahitaji ya kazi yao, chini ya usimamizi wa Ithamari mwana wa kuhani Haruni.+  Lakini hakuwapa chochote wana wa Kohathi kwa sababu majukumu yao yalihusisha kutumikia mahali patakatifu,+ nao walibeba vitu vitakatifu mabegani.+ 10  Basi wakuu wakaleta matoleo yao siku ya kuzindua*+ madhabahu na kuitia mafuta. Wakuu walipoleta matoleo yao mbele ya madhabahu, 11  Yehova akamwambia Musa: “Kila siku, mkuu mmoja ataleta matoleo yake kwa ajili ya kuizindua madhabahu.” 12  Yule aliyeleta matoleo yake siku ya kwanza alikuwa Nashoni+ mwana wa Aminadabu wa kabila la Yuda. 13  Alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130* na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,*+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 14  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba;* 15  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 16  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 17  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Nashoni mwana wa Aminadabu.+ 18  Siku ya pili, Nethaneli+ mwana wa Zuari, mkuu wa Isakari, alileta matoleo yake. 19  Alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 20  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 21  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 22  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 23  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Nethaneli mwana wa Zuari. 24  Siku ya tatu, mkuu wa wana wa Zabuloni, Eliabu+ mwana wa Heloni, 25  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 26  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 27  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 28  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 29  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Eliabu+ mwana wa Heloni. 30  Siku ya nne, mkuu wa wana wa Rubeni, Elisuri+ mwana wa Shedeuri, 31  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 32  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 33  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 34  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 35  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 36  Siku ya tano, mkuu wa wana wa Simeoni, Shelumieli+ mwana wa Zurishadai, 37  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 38  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 39  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 40  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 41  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 42  Siku ya sita, mkuu wa wana wa Gadi, Eliasafu+ mwana wa Deueli, 43  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 44  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 45  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 46  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 47  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Eliasafu+ mwana wa Deueli. 48  Siku ya saba, mkuu wa wana wa Efraimu, Elishama+ mwana wa Amihudi, 49  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 50  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 51  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 52  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 53  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Elishama+ mwana wa Amihudi. 54  Siku ya nane, mkuu wa wana wa Manase, Gamalieli+ mwana wa Pedazuri, 55  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 56  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 57  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 58  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 59  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 60  Siku ya tisa, mkuu+ wa wana wa Benjamini, Abidani+ mwana wa Gidioni, 61  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 62  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 63  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 64  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 65  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Abidani+ mwana wa Gidioni. 66  Siku ya kumi, mkuu wa wana wa Dani, Ahiezeri+ mwana wa Amishadai, 67  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 68  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 69  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 70  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 71  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 72  Siku ya 11, mkuu wa wana wa Asheri, Pagieli+ mwana wa Okrani, 73  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 74  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 75  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 76  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 77  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Pagieli+ mwana wa Okrani. 78  Siku ya 12, mkuu wa wana wa Naftali, Ahira+ mwana wa Enani, 79  alileta sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli 70 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,+ vyombo vyote viwili vilikuwa vimejaa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya toleo la nafaka;+ 80  kikombe kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli 10, kilichojaa uvumba; 81  ng’ombe dume mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa;+ 82  mwanambuzi mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi;+ 83  na kwa ajili ya dhabihu ya ushirika+ alileta ng’ombe wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano, na wanakondoo dume watano kila mmoja wao akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo yaliyokuwa matoleo ya Ahira+ mwana wa Enani. 84  Haya ndiyo matoleo ya kuzindua+ madhabahu yaliyoletwa na wakuu wa Israeli siku ilipotiwa mafuta: sahani 12 za fedha, mabakuli 12 ya fedha, vikombe 12 vya dhahabu;+ 85  kila sahani ya fedha ilikuwa na uzito wa shekeli 130, na kila bakuli lilikuwa na uzito wa shekeli 70, fedha yote iliyotengeneza vyombo hivyo ilikuwa na uzito wa shekeli 2,400 kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu;+ 86  vile vikombe 12 vya dhahabu vilivyojaa uvumba vilikuwa na uzito wa shekeli 10 kila kikombe kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu, dhahabu yote iliyotengeneza vikombe hivyo ilikuwa na uzito wa shekeli 120. 87  Ng’ombe dume wote walioletwa kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa walikuwa 12, pia kondoo dume 12, wanakondoo dume 12 kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja na matoleo yao ya nafaka, na wanambuzi 12 kwa ajili ya dhabihu ya dhambi; 88  na ng’ombe dume wote walioletwa kwa ajili ya dhabihu ya ushirika walikuwa 24, pia kondoo dume 60, mbuzi dume 60, na wanakondoo dume 60 kila mmoja akiwa na umri wa mwaka mmoja. Hayo ndiyo matoleo yaliyotolewa kwa ajili ya kuizindua+ madhabahu baada ya kuitia mafuta.+ 89  Kila mara Musa alipoingia katika hema la mkutano kuongea na Mungu,+ alisikia sauti ikizungumza naye kutoka juu ya kifuniko+ cha sanduku la Ushahidi, kutoka katikati ya wale makerubi wawili;+ Mungu aliongea naye.

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “kuweka wakfu.”
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “shekeli takatifu.”
Au “bakuli dogo lenye uzito wa shekeli 10, lililojaa uvumba.”