Hosea 11:1-12

  • Mungu ampenda Israeli tangu utotoni (1-12)

11  “Israeli alipokuwa mvulana, nilimpenda,+Nikamwita mwanangu atoke Misri.+   Kadiri walivyowaita,*Ndivyo walivyoenda mbali nao.+ Waliendelea kutoa dhabihu kwa sanamu za Baali+Na kutoa dhabihu kwa sanamu za kuchongwa.+   Lakini mimi ndiye niliyewafundisha Waefraimu kutembea,+ nikawabeba mikononi mwangu;+Lakini hawakutambua kwamba niliwaponya.   Niliendelea kuwavuta kwa kamba za wanadamu,* kwa kamba za upendo;+Nami nilikuwa kwao kama mtu anayeinua nira kutoka kwenye mataya yao,Na kwa upole nikamletea kila mmoja wao chakula.   Hawatarudi katika nchi ya Misri, lakini watatawaliwa na Ashuru,+Kwa sababu walikataa kunirudia.+   Na upanga utavuma dhidi ya majiji yao+Na kuharibu makomeo yao na kuwanyafua kwa sababu ya njama zao.+   Watu wangu wana mwelekeo wa kutokuwa waaminifu kwangu.+ Ingawa waliwaita wapande juu,* hakuna yeyote anayeinuka.   Enyi Waefraimu, kwa nini niwaache?+ Enyi Waisraeli, kwa nini niwatie mikononi mwa maadui wenu? Kwa nini niwatendee kama Adma? Kwa nini niwafanye kama Seboiimu?+ Moyo wangu umebadilika;Na pia nimechochewa kuwahurumia.+   Sitamwaga hasira yangu inayowaka. Sitawaangamiza tena Waefraimu,+Kwa maana mimi ni Mungu, mimi si mwanadamu,Mtakatifu aliye miongoni mwenu;Nami sitawashambulia kwa hasira. 10  Watatembea wakimfuata Yehova, naye atanguruma kama simba;+Atakaponguruma, wanawe watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.+ 11  Watatoka Misri wakitetemeka kama ndege,Kama njiwa kutoka nchi ya Ashuru;+Nami nitawapa makao katika nyumba zao,”* asema Yehova.+ 12  “Waefraimu wamenizingira wakisema uwongo,Na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.+ Lakini watu wa Yuda bado wanazunguka huku na huku* pamoja na Mungu,Nao ni waaminifu kwangu mimi, niliye Mtakatifu Zaidi.”+

Maelezo ya Chini

Yaani, manabii na watu wengine waliotumwa kuwafundisha Waisraeli.
Au “kamba za fadhili,” kama zile zinazotumiwa na mzazi.
Yaani, kwenye ibada iliyokwezwa.
Tnn., “nitafanya wakae katika nyumba zao.”
Au “wanatembea.”