Hosea 6:1-11

  • Wasihiwa wamrudie Yehova (1-3)

  • Upendo mshikamanifu usiodumu wa Waisraeli (4-6)

    • Upendo mshikamanifu ni bora kuliko dhabihu (6)

  • Mwenendo wa aibu wa Waisraeli (7-11)

6  “Njooni, tumrudie Yehova,Kwa maana ameturarua vipandevipande,+ lakini atatuponya. Alitupiga, lakini atafunga majeraha yetu.   Atatuhuisha baada ya siku mbili. Siku ya tatu atatuinua,Nasi tutaishi mbele zake.   Tutamjua, tutajitahidi kumjua Yehova. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko;Atakuja kwetu kama mvua kubwa,Kama mvua ya masika inayolowesha dunia.”   “Niwafanyie nini, enyi Waefraimu? Niwafanyie nini, enyi watu wa Yuda,Kwa maana upendo wenu mshikamanifu ni kama ukungu wa asubuhi,Kama umande unaotoweka haraka.   Ndiyo sababu nitawakatakata kabisa kwa kutumia manabii;+Nitawaua kwa maneno ya kinywa changu.+ Na hukumu zangu dhidi yenu zitang’aa kama mwangaza.+   Kwa maana ninapendezwa na upendo mshikamanifu,* si dhabihu,Na kumjua Mungu, badala ya dhabihu nzima za kuteketezwa.+   Lakini wao, kama wanadamu tu, wamevunja agano.+ Wamenisaliti katika nchi yao.   Gileadi ni mji wa watenda maovu,+Umefunikwa kwa nyayo za damu.+   Magenge ya makuhani ni kama makundi ya wavamizi yanayomvizia mtu. Wanawaua watu barabarani kule Shekemu,+Kwa maana mwenendo wao ni wa aibu. 10  Nimeona jambo la kuchukiza sana katika nyumba ya Israeli. Huko Waefraimu hufanya ukahaba;+Waisraeli wamejichafua wenyewe.+ 11  Zaidi ya hayo, enyi watu wa Yuda, wakati wa mavuno umetengwa kwa ajili yenu,Nitakapowakusanya watu wangu waliotekwa.”+

Maelezo ya Chini

Au “rehema.”