Isaya 1:1-31

  • Baba na wanawe waasi (1-9)

  • Yehova anachukia ibada ya kidesturi (10-17)

  • “Tunyooshe mambo kati yetu” (18-20)

  • Sayuni litakuwa jiji lenye uaminifu tena (21-31)

1  Maono ambayo Isaya*+ mwana wa Amozi aliona kuhusu Yuda na Yerusalemu katika siku za Uzia,+ Yothamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda:+   Sikieni, enyi mbingu, na usikilize, ewe dunia,+Kwa maana Yehova amesema: “Nimelea wana wakakua,+Lakini wameniasi.+   Ng’ombe anamjua vizuri aliyemnunua,Na punda anaijua vizuri hori ya mmiliki wake;Lakini Israeli hanijui,*+Watu wangu mwenyewe hawatendi kwa uelewaji.”   Ole kwa taifa lenye dhambi,+Watu waliolemewa na dhambi,Uzao wa watu waovu, watoto waliopotoka! Wamemwacha Yehova;+Wamemvunjia heshima Mtakatifu wa Israeli;Wamemgeuzia migongo yao.   Ni wapi mtakapopigwa tena kwa kuwa mnazidi kuasi?+ Kichwa chote ni kigonjwa,Na moyo wote ni mgonjwa.+   Kuanzia wayo wa mguu mpaka kichwani, hakuna sehemu yenye afya. Kuna majeraha na michubuko na vidonda vilivyo wazi—Havijatibiwa* wala kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta.+   Nchi yenu ni ukiwa. Majiji yenu yameteketezwa kwa moto. Wageni wanaila nchi yenu mbele ya macho yenu.+ Ni kama nchi iliyo ukiwa iliyoharibiwa kabisa na wageni.+   Binti ya Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu,Kama nyumba ya msonge katika shamba la matango,Kama jiji lililozingirwa.+   Kama Yehova wa majeshi hangetuachia waokokaji wachache,Tungekuwa kama Sodoma,Na tungefanana na Gomora.+ 10  Sikieni neno la Yehova, enyi madikteta* wa Sodoma.+ Sikilizeni sheria* ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora.+ 11  “Dhabihu zenu nyingi zina faida gani kwangu?”+ asema Yehova. “Nimetosheka na dhabihu zenu za kuteketezwa za kondoo dume+ na mafuta ya wanyama waliolishwa vizuri,+Nami sipendezwi na damu+ ya ng’ombe dume wachanga+ na wanakondoo na mbuzi.+ 12  Mnapokuja kusimama mbele zangu,+Ni nani ambaye amewataka mfanye hivyo,Mzikanyage-kanyage nyua zangu?+ 13  Acheni kuleta matoleo zaidi ya nafaka yasiyo na thamani. Uvumba wenu unanichukiza.+ Miezi mipya,+ sabato,+ kuita makusanyiko+—Siwezi kuvumilia matumizi ya nguvu za uchawi+ pamoja na kusanyiko lenu takatifu. 14  Nimechukia* miezi yenu mipya na sherehe zenu. Zimekuwa mzigo kwangu;Nimechoka kuzibeba. 15  Na mnaponyoosha mikono yenu,Mimi huficha macho yangu nisiwaone.+ Ingawa mnatoa sala nyingi,+Mimi sisikilizi;+Mikono yenu imejaa damu.+ 16  Jiosheni, jisafisheni;+Ondoeni matendo yenu maovu mbele za macho yangu;Acheni kutenda mabaya.+ 17  Jifunzeni kutenda mema, tafuteni haki,+Mrekebisheni mkandamizaji,Teteeni haki za yatima,Nanyi mteteeni mjane.”+ 18  “Sasa, njooni, na tunyooshe mambo kati yetu,” asema Yehova.+ “Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu,Zitafanywa kuwa nyeupe kama theluji;+Ingawa ni nyekundu kama kitambaa chekundu,Zitakuwa kama sufu. 19  Mkionyesha utayari na kusikiliza,Mtakula vitu vyema vya nchi.+ 20  Lakini mkikataa na kuasi,Mtaliwa na upanga,+Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hayo.” 21  Jinsi mji mwaminifu+ umekuwa kahaba!+ Ulikuwa umejaa haki;+Uadilifu ulikuwa ukikaa ndani yake,+Lakini sasa wauaji wanakaa ndani yake.+ 22  Fedha yako imekuwa takataka,+Na pombe yako* imechanganywa na maji. 23  Wakuu wako ni wakaidi na wanashirikiana na wezi.+ Kila mmoja wao anapenda rushwa na kutafuta zawadi kwa bidii.+ Hawawatendei kwa haki mayatima,Na kesi ya mjane haiwafikii kamwe.+ 24  Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,Mwenye Nguvu wa Israeli, anasema: “Ah! Nitawaondoa wapinzani wangu,Nami nitalipiza kisasi dhidi ya maadui wangu.+ 25  Nitaugeuza mkono wangu dhidi yako,Nitayeyusha takataka yako kama kwa sabuni,Nami nitauondoa uchafu wako wote.+ 26  Nitawarudisha waamuzi wenu kama mwanzoniNa washauri wenu kama awali.+ Kisha wewe utaitwa Jiji la Uadilifu, Mji Mwaminifu.+ 27  Sayuni atakombolewa kwa haki,+Na watu wake wanaorudi, kwa uadilifu. 28  Waasi na watenda dhambi watavunjwa pamoja,+Na wale wanaomwacha Yehova watafikia mwisho wao.+ 29  Kwa maana wataona aibu kwa sababu ya miti mikubwa ambayo mlitamani,+Nanyi mtafedheheka kwa sababu ya bustani* ambazo mlichagua.+ 30  Kwa maana mtakuwa kama mti mkubwa ambao majani yake yananyauka,+Na kama bustani isiyo na maji. 31  Mwanamume mwenye nguvu atakuwa kitani,*Na kazi yake itakuwa cheche ya moto;Atateketea motoni pamoja na kazi yake,Na hapatakuwa na yeyote wa kuwazima.”

Maelezo ya Chini

Maana yake “Wokovu wa Yehova.”
Au “hamjui bwana wake.”
Tnn., “Havijafinywa; Havijatumbuliwa.”
Au “watawala.”
Au “mafundisho.”
Au “Nafsi yangu imechukia.”
Au “pombe yako ya ngano.”
Inaonekana ni miti na bustani zilizohusiana na ibada ya sanamu.
Nyuzi zinazoshika moto kwa urahisi ambazo zinafanana na kamba.