Isaya 10:1-34

  • Mkono wa Mungu dhidi ya Israeli (1-4)

  • Ashuru⁠—​Fimbo ya hasira ya Mungu (5-11)

  • Ashuru kuadhibiwa (12-19)

  • Watu waliobaki wa Yakobo watarudi (20-27)

  • Mungu atahukumu Ashuru (28-34)

10  Ole wao wanaotunga sheria zinazodhuru,*+Ambao sikuzote huandika amri zinazokandamiza,   Ili kuwanyima maskini haki zao za kisheria,Ili kuwanyang’anya haki watu wa hali ya chini kati ya watu wangu,+Kuwafanya wajane kuwa nyara yaoNa kuwapora mayatima!+   Mtafanya nini katika siku ya kuadhibiwa,*+Uharibifu utakapokuja kutoka mbali?+ Mtamkimbilia nani ili kupata msaada+Nanyi mtauacha wapi utajiri* wenu?   Hakuna kinachobaki isipokuwa kujikunyata kati ya wafungwaAu kuanguka kati ya waliouawa. Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga.+   “Aha! Mwashuru,+Fimbo ya kuonyesha hasira yangu,+Na gongo lililo mkononi mwao kwa ajili ya shutuma yangu!   Nitamtuma yeye dhidi ya taifa lililoasi imani,+Dhidi ya watu walionikasirisha,Nitamwamuru achukue nyara nyingi na kupora mali nyingiNa kuzikanyaga kama matope barabarani.+   Lakini hatataka kufanya hivyoNa moyo wake hautapanga hila kwa njia hiyo;Kwa maana moyo wake umeazimia kuangamizaKuangamiza kabisa mataifa mengi, si machache.   Kwa maana anasema,‘Je, wakuu wangu wote si wafalme?+   Je, Kalno+ si kama tu Karkemishi?+ Je, Hamathi+ si kama Arpadi?+ Je, Samaria+ si kama Damasko?+ 10  Mkono wangu umeziteka falme za miungu ya ubatili,Ambazo sanamu zao za kuchongwa zilikuwa nyingi kuliko zile za Yerusalemu na Samaria!+ 11  Je, sitaitendea pia Yerusalemu na sanamu zakeKama vile nilivyoitendea Samaria na miungu yake ya ubatili?’+ 12  “Yehova atakapomaliza kazi yake yote kwenye Mlima Sayuni na Yerusalemu, atamwadhibu* mfalme wa Ashuru kwa sababu ya moyo wake wenye dharau na macho yake yanayotazama kwa kiburi na majivuno.+ 13  Kwa maana anasema,‘Nitafanya hivyo kwa nguvu za mkono wanguNa kwa hekima yangu, kwa maana nina hekima. Nitaiondoa mipaka ya mataifa+Na kupora hazina zao,+Nami nitawatiisha wakaaji kama mwenye nguvu.+ 14  Kama mtu anayeingiza mkono katika kiota,Mkono wangu utateka mali za mataifa;Na kama mtu anayekusanya mayai yaliyoachwa,Nitaikusanya dunia nzima! Hakuna atakayepiga mabawa yake au kufungua kinywa chake wala kunong’oneza.’” 15  Je, shoka litajikweza juu ya yule anayelitumia kukata? Je, msumeno utajikweza juu ya yule anayeutumia kukata? Je, gongo+ linaweza kumtikisa yule anayeliinua? Au je, fimbo inaweza kumwinua yule ambaye hajatengenezwa kwa mbao? 16  Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,Atawafanya watu wake walionenepa wakonde,+Na chini ya utukufu wake atawasha moto mkubwa unaoteketeza.+ 17  Nuru+ ya Israeli itakuwa moto,+Na Mtakatifu wake mwali wa moto;Utawaka na kuteketeza magugu yake na vichaka vyake vya miiba kwa siku moja. 18  Ataondoa kabisa* utukufu wa msitu wake na shamba lake la matunda;Itakuwa kama mtu mgonjwa anavyodhoofika.+ 19  Miti itakayobaki katika msitu wakeItakuwa michache sana hivi kwamba mvulana ataweza kuihesabu. 20  Siku hiyo watu wa Israeli waliobakiNa waliookoka wa nyumba ya YakoboHawatamtegemea tena yule aliyewapiga;+Bali watamtegemea Yehova,Mtakatifu wa Israeli, kwa uaminifu. 21  Ni watu wachache tu waliobaki watakaorudi,Watu wa Yakobo waliobaki, watarudi kwa Mungu Mwenye Nguvu.+ 22  Kwa maana ingawa watu wako, ewe Israeli,Ni kama chembe za mchanga wa bahari,Ni watu wachache tu waliobaki watakaorudi.+ Maangamizi yameamuliwa,+Na haki* itawafunika.+ 23  Naam, maangamizi yaliyoamuliwa na Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,Yatatekelezwa katika nchi yote.+ 24  Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, anasema: “Msiogope, watu wangu mnaokaa Sayuni, kwa sababu ya Mwashuru, aliyekuwa akiwapiga kwa fimbo+ na kuinua gongo lake dhidi yenu kama Misri ilivyofanya.+ 25  Kwa maana kwa muda mfupi sana shutuma itafika mwisho; hasira yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.+ 26  Yehova wa majeshi atatikisa mjeledi dhidi yake,+ kama aliposhinda Midiani kando ya mwamba wa Orebu.+ Na gongo lake litakuwa juu ya bahari, naye ataliinua kama alivyoitendea Misri.+ 27  “Siku hiyo mzigo wake utaondoka juu ya bega lako,+Na nira yake itaondoka kwenye shingo yako,+Na nira itavunjwa+ kwa sababu ya mafuta.” 28  Amekuja Aiathi;+Amepitia Migroni;Ameweka mizigo yake huko Mikmashi.+ 29  Wamevuka kivuko;Wamekaa Geba usiku kucha;+Rama inatetemeka, Gibea+ ya Sauli imekimbia.+ 30  Paza sauti yako na upige mayowe, Ee binti ya Galimu! Sikiliza, Ee Laisha! Ewe maskini Anathothi!+ 31  Madmena amekimbia. Wakaaji wa Gebimu wametafuta mahali pa kujificha. 32  Leo hiihii atasimama Nobu.+ Anautikisia ngumi mlima wa binti ya Sayuni,Kilima cha Yerusalemu. 33  Tazama! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,Anakata matawi kwa kishindo kikubwa sana;+Miti mirefu zaidi inakatwa,Na walio juu wanashushwa. 34  Anapiga vichaka vya msitu kwa kifaa cha chuma,*Na Lebanoni utaangushwa na mwenye nguvu.

Maelezo ya Chini

Au “masharti yanayodhuru.”
Au “kuwajibishwa.”
Au “utukufu.”
Tnn., “nitamwadhibu.”
Au “Kuanzia kwenye nafsi hadi kwenye mwili ataondoa.”
Au “adhabu.”
Au “shoka.”