Isaya 12:1-6

  • Wimbo wa shukrani (1-6)

    • “Yah Yehova ni nguvu zangu” (2)

12  Siku hiyo hakika utasema: “Ninakushukuru, Ee Yehova,Kwa maana ingawa ulinikasirikia,Hasira yako ilipoa hatua kwa hatua, nawe ukanifariji.+   Tazama! Mungu ni wokovu wangu.+ Nitamtumaini nami sitaogopa;+Kwa maana Yah* Yehova ni nguvu zangu na uwezo wangu,Naye amekuwa wokovu wangu.”+   Mtateka maji kwa kushangiliaKutoka kwenye chemchemi za wokovu.+   Na siku hiyo mtasema: “Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,Yajulisheni mataifa matendo yake!+ Tangazeni kwamba jina lake limekwezwa.+   Mwimbieni sifa* Yehova+ kwa maana ametenda mambo makuu.+ Jambo hilo na litangazwe duniani kote.   “Paza sauti na upige kelele kwa shangwe, ewe mkaaji* wa Sayuni,Kwa maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu katikati yako.”

Maelezo ya Chini

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Mpigieni muziki.”
Tnn., “mkaaji wa kike.” Usemi huu unarejelea wakaaji wote kuwa kama mwanamke.