Isaya 15:1-9

  • Tangazo dhidi ya Moabu (1-9)

15  Tangazo dhidi ya Moabu:+ Kwa sababu limeharibiwa kwa usiku mmoja,Jiji la Ari+ la Moabu limenyamazishwa. Kwa sababu limeharibiwa kwa usiku mmoja,Jiji la Kiri+ la Moabu limenyamazishwa.   Amepanda mpaka kwenye Nyumba* na mpaka Diboni,+Kwenye mahali pa juu ili kulia. Moabu inaombolezea Nebo+ na Medeba.+ Kila kichwa kimenyolewa upara,+ ndevu zote zimenyolewa.+   Wamevaa nguo za magunia katika barabara zake. Kwenye paa zao na katika viwanja vyao vya jiji, wote wanaomboleza kwa sauti;Wanashuka chini wakilia.+   Heshboni na Eleale+ wanalia kwa sauti;Sauti yao inasikika mpaka Yahazi.+ Ndiyo sababu watu wenye silaha wa Moabu wanaendelea kupaza sauti. Anatetemeka.*   Moyo wangu unamlilia Moabu. Wakimbizi wake wamekimbia mpaka Soari+ na Eglath-shelishiya.+ Kwenye njia inayopanda kwenda Luhithi wanalia wakipanda;Kwenye njia ya kwenda Horonaimu wanalia kwa sauti kwa sababu ya msiba.+   Kwa maana maji ya Nimrimu yamekuwa ukiwa;Majani mabichi yamekauka,Majani yamekwisha na hakuna chochote kibichi kilichobaki.   Ndiyo sababu wanabeba kilichobaki katika maghala yao na utajiri wao;Wanavuka bonde* la mierebi.   Kwa maana kilio kinasikika katika eneo lote la Moabu.+ Maombolezo yanafika Eglaimu;Maombolezo yanafika Beer-elimu.   Kwa maana maji ya Dimoni yamejaa damu,Nami nina mengi zaidi kwa ajili ya Dimoni: Simba kwa ajili ya watu wa Moabu wanaoponyokaNa kwa ajili ya wale wanaobaki nchini.+

Maelezo ya Chini

Au “Hekalu.”
Au “Nafsi yake inatetemeka.”
Au “korongo.”