Isaya 17:1-14

  • Tangazo dhidi ya Damasko (1-11)

  • Mataifa yatakemewa na Yehova (12-14)

17  Tangazo dhidi ya Damasko:+ “Tazama! Damasko halitakuwa jiji tena,Nalo litakuwa rundo la magofu.+   Majiji ya Aroeri+ yataachwa;Yatakuwa mahali ambapo mifugo italalaNa hakuna yeyote atakayeiogopesha.   Majiji yenye ngome yatatoweka Efraimu,+Na ufalme kutoka Damasko;+Na wale wanaobaki wa SiriaWatakuwa kama utukufu wa Waisraeli,”* asema Yehova wa majeshi.   “Siku hiyo utukufu wa Yakobo utafifia,Na mwili wake wenye afya utakonda.*   Itakuwa kama mvunaji anapovuna nafaka iliyo shambaniNa mkono wake unapovuna masuke ya nafaka,Kama mtu anayeokota masalio ya nafaka katika Bonde la* Refaimu.+   Ni masalio tu yatakayobaki,Kama mzeituni unapopigwa: Ni zeituni mbili au tatu tu zilizoiva zinazobaki kwenye tawi refu zaidi,Ni nne au tano tu kwenye matawi yanayozaa matunda,”+ asema Yehova Mungu wa Israeli.  Siku hiyo mwanadamu atamtazama Muumba wake, na macho yake yatamtazama Mtakatifu wa Israeli.  Hatazitazama madhabahu,+ kazi ya mikono yake;+ naye hatatazama kile ambacho vidole vyake vimetengeneza, iwe ni miti mitakatifu* au vinara vya uvumba.   Siku hiyo majiji yake yenye ngome yatakuwa kama mahali palipoachwa mwituni,+Kama tawi lililoachwa mbele ya Waisraeli;Litakuwa ukiwa. 10  Kwa maana umemsahau Mungu+ wa wokovu wako;Hukumkumbuka Mwamba+ wa ngome yako. Ndiyo sababu unapanda mashamba makubwa maridadi*Na kupanda humo chipukizi la mgeni.* 11  Mchana unalizungushia shamba lako ua kwa uangalifu,Asubuhi unachipusha mbegu zako,Lakini mavuno yatatoweka katika siku ya ugonjwa na maumivu yasiyoweza kuponywa.+ 12  Sikilizeni! Kuna vurugu za watu wengi,Walio na msukosuko kama wa bahari! Kuna kelele za mataifa,Ambao sauti yao ni kama mngurumo wa maji yenye nguvu! 13  Mataifa yatatoa sauti kama mngurumo wa maji mengi. Atayakemea, nayo yatakimbia mbali sana,Yakifukuzwa kama makapi ya milima mbele ya upepoKama mchongoma unaopeperushwa na* upepo wa dhoruba. 14  Jioni kuna tisho la ghafla. Kabla ya asubuhi hayapo tena. Hilo ndilo fungu la wale wanaotuporaNa kura ya wale wanaotunyang’anya mali zetu.

Maelezo ya Chini

Tnn., “wana wa Israeli.”
Tnn., “mafuta ya nyama yake yatapungua.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Angalia Kamusi.
Au “yanayopendeza.”
Au “mungu wa kigeni.”
Au “mbaruti katika.”