Isaya 18:1-7

  • Ujumbe dhidi ya Ethiopia (1-7)

18  Ole wa nchi ya wadudu wenye mabawa yanayovumaKatika eneo la mito ya Ethiopia!+   Inatuma wajumbe kupitia baharini,Wanaovuka maji katika vyombo vya mafunjo, ikisema: “Nendeni, enyi wajumbe wenye mbio,Kwa taifa lenye watu warefu na walio na ngozi laini,*Kwa watu wanaoogopwa kila mahali,+Kwa taifa lenye nguvu, linaloshinda,*Ambalo nchi yake imefagiliwa na mito.”   Enyi wakaaji wote wa nchi nanyi wakaaji wa dunia,Mtakachoona kitakuwa kama ishara* iliyoinuliwa juu ya milima,Nanyi mtasikia sauti kama ya pembe inapopigwa.   Kwa maana Yehova aliniambia hivi: “Nitaendelea kutulia na kutazama* mahali pangu palipofanywa imara,Kama joto linalometameta pamoja na mwangaza wa jua,Kama wingu la umande katika joto la mavuno.   Kwa maana kabla ya mavuno,Ua linapokamilika na kuwa zabibu inayoiva,Machipukizi yake yatakatwa kwa miunduVikonyo vitakatwa na kuondolewa.   Wote wataachwa waliwe na ndege wanaowinda wa milimaniNa wanyama wa duniani. Ndege wanaowinda watawala wakati wa kiangazi,Na wanyama wote wa dunia watawala wakati wa mavuno.   Wakati huo zawadi italetwa kwa Yehova wa majeshi,Kutoka kwa taifa lenye watu warefu na walio na ngozi laini,*Kutoka kwa watu wanaoogopwa kila mahali,Kutoka kwa taifa lenye nguvu, linaloshinda,*Ambalo nchi yake imefagiliwa na mito,Mpaka mahali pa jina la Yehova wa majeshi, Mlima Sayuni.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “taifa lenye watu waliochomoza juu na kusuguliwa.”
Au “taifa lenye nguvu nyingi linaloyakanyaga mataifa mengine.”
Au “nguzo ya ishara.”
Au labda, “kutazama kutoka.”
Tnn., “taifa lenye watu waliochomoza juu na kusuguliwa.”
Au “taifa lenye nguvu nyingi linaloyakanyaga mataifa mengine.”