Isaya 19:1-25

  • Tangazo dhidi ya Misri (1-15)

  • Wamisri watamjua Yehova (16-25)

    • Madhabahu kwa ajili ya Yehova nchini Misri (19)

19  Tangazo dhidi ya Misri:+ Tazama! Yehova amepanda juu ya wingu linaloenda kwa kasi, naye anakuja Misri. Miungu ya ubatili ya Misri itatetemeka mbele zake,+Na moyo wa Misri utayeyuka ndani yake.   “Nitawachochea Wamisri dhidi ya Wamisri,Nao watapigana,Kila mmoja atapigana na ndugu yake na jirani yake,Jiji litapigana na jiji, ufalme utapigana na ufalme.   Na roho ya Misri itakuwa na msukosuko ndani yake,Nami nitavuruga mipango yake.+ Watatafuta msaada kutoka kwa miungu ya ubatili,Kwa wachawi na kwa wanaowasiliana na roho na kwa wabashiri.+   Nitaitia Misri mikononi mwa bwana aliye katili,Na mfalme mkali atawatawala,”+ asema Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi.   Na maji ya bahari yatakaushwa,Na mto utakauka na kuwa mkavu.+   Na mito itanuka;Mifereji ya Nile ya Misri itapungua na kukauka. Matete na mafunjo yataoza.+   Mimea iliyo kandokando ya Mto Nile, kwenye kinywa cha Mto Nile,Na ardhi yote iliyopandwa mbegu kandokando ya Nile+ itakauka.+ Itapeperushwa mbali, nayo haitakuwepo tena.   Na wavuvi wataomboleza,Wale wanaotupa ndoano ndani ya Mto Nile wataomboleza,Na wale wanaotandaza nyavu zao juu ya maji watapungua.   Mafundi wa kitani kilichochambuliwa+Na wafumaji wa vitambaa vyeupe wataaibishwa. 10  Wafumaji wake watapondwa;Vibarua wote watahuzunika.* 11  Wakuu wa Soani+ ni wapumbavu. Washauri wenye hekima zaidi wa Farao wanatoa ushauri usio wa busara.+ Mnawezaje kumwambia Farao: “Mimi ni mzao wa watu wenye hekima,Mzao wa wafalme wa kale”? 12  Basi, wako wapi watu wenu wenye hekima?+ Acheni wawaambie kama wanajua kile ambacho Yehova wa majeshi ameamua kuhusu Misri. 13  Wakuu wa Soani wametenda kwa upumbavu;Wakuu wa Nofu*+ wamedanganywa;Wakuu wa makabila yake wameipotosha Misri. 14  Yehova amemmwagia roho ya mvurugo;+Nao wameipotosha Misri katika kila jambo inalofanya,Kama mlevi anavyogaagaa kwenye matapishi yake. 15  Na Misri haitakuwa na kazi yoyote ya kufanya,Iwe ni kwa ajili ya kichwa au mkia, chipukizi au utete.* 16  Siku hiyo Misri itakuwa kama wanawake, itatetemeka na kuogopa kwa sababu ya mkono wenye kutisha ambao Yehova wa majeshi anainua dhidi yake.+ 17  Na nchi ya Yuda itaifanya Misri iogope. Watahofu kila mara Yuda inapotajwa kwa sababu ya uamuzi ambao Yehova wa majeshi amefanya dhidi yao.+ 18  Siku hiyo kutakuwa na majiji matano katika nchi ya Misri yanayozungumza lugha ya Kanaani+ na kuapa kuwa washikamanifu kwa Yehova wa majeshi. Jiji moja litaitwa Jiji la Kubomoa. 19  Siku hiyo kutakuwa na madhabahu kwa ajili ya Yehova katikati ya nchi ya Misri na nguzo kwa ajili ya Yehova kwenye mpaka wake. 20  Itakuwa ishara na ushahidi kwa Yehova wa majeshi nchini Misri; kwa maana watamlilia Yehova kwa sauti kwa sababu ya wakandamizaji, naye atawapelekea mwokozi, aliye mkuu, ambaye atawaokoa. 21  Na Yehova atajulikana kwa Wamisri, na Wamisri watamjua Yehova siku hiyo, nao watatoa dhabihu na zawadi na kuweka nadhiri kwa Yehova na kuitimiza. 22  Yehova ataipiga Misri,+ ataipiga na kuiponya; nao watamrudia Yehova, naye atasikiliza maombi yao ya kusihi na kuwaponya. 23  Siku hiyo kutakuwa na barabara kuu+ kutoka Misri kwenda Ashuru. Kisha Ashuru itakuja Misri, na Misri itaenda Ashuru; na Misri itamtumikia Mungu pamoja na Ashuru. 24  Siku hiyo Israeli itakuwa ya tatu pamoja na Misri na pamoja na Ashuru,+ baraka katikati ya dunia, 25  kwa maana Yehova wa majeshi atakuwa amewabariki, akisema: “Wabarikiwe watu wangu, Misri, na kazi ya mikono yangu, Ashuru, na urithi wangu, Israeli.”+

Maelezo ya Chini

Au “watahuzunika katika nafsi.”
Au “Memfisi.”
Au labda, “tawi la mtende au tete.”