Isaya 21:1-17

  • Tangazo dhidi ya nyika ya bahari (1-10)

    • Kulinda kwenye mnara wa mlinzi (8)

    • “Babiloni ameanguka!” (9)

  • Tangazo dhidi ya Duma na nchi tambarare ya jangwani (11-17)

    • “Mlinzi, kuna habari gani za usiku?” (11)

21  Tangazo dhidi ya nyika ya bahari:*+ Msiba unakuja kama pepo za dhoruba zinazovuma kusini,Kutoka nyikani, kutoka katika nchi inayotisha.+   Nimeambiwa maono ya kutisha: Mwenye hila anatenda kwa hila,Na mwangamizaji, anaangamiza. Nenda juu, ewe Elamu! Zingira, ewe Umedi!+ Nitakomesha kilio chote cha uchungu alichosababisha.+   Ndiyo sababu nina maumivu makali.*+ Ninafurukuta kwa uchungu,Uchungu kama wa mwanamke anayezaa. Nimetaabika sana hivi kwamba siwezi kusikia;Nimesumbuka sana hivi kwamba siwezi kuona.   Moyo wangu unadundadunda; ninatetemeka kwa hofu. Gizagiza la jioni nililotamani sana linanifanya nitetemeke.   Andaeni meza na mpange viti! Mle na mnywe!+ Simameni, enyi wakuu, itieni* ngao mafuta.   Kwa maana Yehova aliniambia hivi: “Nenda, mweke mlinzi na umwambie aseme yale anayoyaona.”   Naye akaona gari la vita pamoja na kundi la farasi,Gari la vita la punda,Gari la vita la ngamia. Alitazama kwa makini, akiwa amekaza fikira sana.   Kisha akaita kwa sauti kama simba: “Ee Yehova, ninasimama daima juu ya mnara wa mlinzi wakati wa mchana,Nami ninasimama katika kituo changu cha ulinzi kila usiku.+   Tazama kinachokuja: Wanaume wakiwa katika gari la vita na kundi la farasi wa vita!”+ Kisha akasema: “Ameanguka! Babiloni ameanguka!+ Sanamu zake zote za kuchongwa za miungu yake amezivunjavunja na kuziangusha chini!”+ 10  Enyi watu wangu waliopurwa,Mazao ya* uwanja wangu wa kupuria,+Nimewaambia yale niliyosikia kutoka kwa Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli. 11  Tangazo dhidi ya Duma:* Kuna mtu anayeniita kutoka Seiri:+ “Mlinzi, kuna habari gani za usiku? Mlinzi, kuna habari gani za usiku?” 12  Mlinzi akasema: “Asubuhi inakuja, na usiku pia. Ikiwa mnataka kuuliza, ulizeni. Njooni tena!” 13  Tangazo dhidi ya jangwa tambarare: Mtakaa usiku kucha msituni katika nchi tambarare ya jangwani,Enyi misafara ya Dedani.+ 14  Leteni maji ili mkampokee mwenye kiu,Enyi wakaaji wa nchi ya Tema,+Mleteeni mkate yule anayekimbia. 15  Kwa maana wamekimbia kwa sababu ya panga, kwa sababu ya upanga uliochomolewa,Kwa sababu ya upinde uliopindwa, na kwa sababu ya ukatili wa vita. 16  Kwa maana Yehova aliniambia hivi: “Katika muda wa mwaka mmoja, kulingana na miaka ya kibarua,* utukufu wote wa Kedari+ utafikia mwisho. 17  Wapiga upinde waliobaki kati ya mashujaa wa Kedari watakuwa wachache, kwa maana Yehova Mungu wa Israeli amesema hivyo.”

Maelezo ya Chini

Inaonekana kwamba usemi huu unarejelea eneo la Babilonia ya kale.
Tnn., “kiuno changu kimejaa maumivu.”
Au “ipakeni.”
Tnn., “Mwana wa.”
Maana yake “Kimya.”
Au “iliyohesabiwa kwa uangalifu kama kibarua anavyofanya”; yaani, kwa mwaka mmoja kamili.