Isaya 22:1-25

  • Tangazo kuhusu Bonde la Maono (1-14)

  • Eliakimu awa msimamizi badala ya Shebna (15-25)

    • Kigingi cha mfano (23-25)

22  Tangazo kuhusu Bonde la Maono:*+ Una tatizo gani hivi kwamba watu wako wote wamepanda juu ya paa?   Ulijaa machafuko,Jiji lenye msukosuko, mji wenye furaha. Watu wako waliouawa hawakuuawa kwa upanga,Wala hawakufa vitani.+   Madikteta wako wote wamekimbia pamoja.+ Walichukuliwa kuwa wafungwa bila kutumia upinde. Wote waliopatikana walichukuliwa kuwa wafungwa,+Ingawa walikuwa wamekimbilia mbali sana.   Ndiyo sababu nilisema: “Msinitazame,Nami nitalia kwa uchungu.+ Msisisitize kunifarijiKwa sababu ya kuangamizwa kwa binti ya* watu wangu.+   Kwa maana ni siku ya mvurugo na ya kushindwa na ya wasiwasi,+Kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,Katika Bonde la Maono. Ukuta unabomolewa+Na kuna kilio kwenye mlima.   Elamu+ inachukua podoPamoja na magari ya vita yenye watu na farasi,*Na Kiri+ inafunua* ngao.   Mabonde yako yaliyo mazuri zaidiYatajaa magari ya vita,Na farasi* watajipanga langoni,   Na pazia la Yuda litaondolewa.* “Siku hiyo utatazama kuelekea ghala la silaha la Nyumba ya Msitu,+  nanyi mtayaona yale mashimo mengi yaliyo katika ukuta wa Jiji la Daudi.+ Nanyi mtayakusanya maji ya kidimbwi cha chini.+ 10  Mtazihesabu nyumba za Yerusalemu, nanyi mtazibomoa nyumba hizo ili kuimarisha ukuta. 11  Nanyi mtatengeneza beseni kati ya hizo kuta mbili kwa ajili ya maji ya kidimbwi cha zamani, lakini hamtamtegemea Muumba* wake Mkuu, nanyi hamtamwona Yule aliyeibuni zamani. 12  Siku hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,Atawaambia watu walie na kuomboleza,+Wanyoe vichwa na kuvaa nguo za magunia. 13  Lakini badala yake, kuna sherehe na kushangilia,Kuchinja ng’ombe na kuchinja kondoo,Kula nyama na kunywa divai.+ ‘Acheni tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.’”+ 14  Kisha Yehova wa majeshi akajifunua masikioni mwangu: “‘Uovu huu hautafunikwa kwa ajili yenu mpaka ninyi watu mtakapokufa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.” 15  Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, anasema hivi: “Ingia kwa huyu msimamizi-nyumba, kwa Shebna,+ anayesimamia nyumba,* na umwambie,⁠ 16  ‘Una masilahi gani hapa, na je, una mtu wako hapa hivi kwamba umejichimbia kaburi hapa?’ Anachimba kaburi lake mahali palipoinuka; anajichongea mahali pa kupumzika* katika jabali. 17  ‘Tazama! Yehova atakutupa chini kwa nguvu, ewe mwanamume, na kukukamata kwa nguvu. 18  Hakika atakufunga kwa nguvu na kukurusha kama mpira katika nchi pana. Utafia huko, na huko magari yako yenye utukufu yatakuwa fedheha kwa nyumba ya bwana wako. 19  Nami nitakung’oa madarakani na kukufukuza kutoka katika cheo chako. 20  “‘Siku hiyo nitamwita mtumishi wangu Eliakimu+ mwana wa Hilkia, 21  nami nitamvisha kanzu yako na kumfunga kwa nguvu ukumbuu wako,+ nami nitatia mamlaka yako* mkononi mwake. Naye atakuwa baba kwa wakaaji wa Yerusalemu na nyumba ya Yuda. 22  Nami nitauweka ufunguo wa nyumba ya Daudi+ juu ya bega lake. Atafungua na hakuna yeyote atakayefunga; naye atafunga na hakuna yeyote atakayefungua. 23  Nitampigilia kama kigingi mahali panapodumu, naye atakuwa kama kiti cha ufalme cha utukufu kwa nyumba ya baba yake. 24  Nao watauning’iniza juu yake utukufu* wote wa nyumba ya baba yake, wazao na watoto,* vyombo vyote vidogo, vyombo vyenye umbo la bakuli, na pia mitungi yote mikubwa. 25  “‘Siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘kigingi kilichopigiliwa mahali panapodumu kitang’olewa,+ nacho kitakatwa na kuanguka, na mzigo ulio juu yake utaanguka na kuharibika, kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.’”

Maelezo ya Chini

Inaonekana maneno haya yanarejelea Yerusalemu.
Tashihisi ya kishairi, ambayo labda inaonyesha sikitiko au huruma.
Au “wapanda farasi.”
Au “inatayarisha.”
Au “wapanda farasi.”
Au “ulinzi wa Yuda utaondolewa.”
Au “Mtengenezaji.”
Au “jumba la mfalme.”
Tnn., “makao.”
Au “milki yako.”
Tnn., “uzito.”
Au “machipukizi.”