Isaya 23:1-18

  • Tangazo dhidi ya Tiro (1-18)

23  Tangazo kuhusu Tiro:+ Ombolezeni kwa sauti, enyi meli za Tarshishi!+ Kwa maana bandari imeharibiwa; haiwezi kuingiwa. Wamefunuliwa habari kutoka katika nchi ya Kitimu.+   Nyamazeni, enyi wakaaji wa pwani. Wafanyabiashara kutoka Sidoni+ wanaovuka bahari wamekujaza.   Nafaka* ya Shihori* ilienda juu ya maji mengi,+Mavuno ya Nile, mapato yake,Yalileta faida ya mataifa.+   Ona aibu, Ee Sidoni, ngome ya bahari,Kwa sababu bahari imesema: “Sijapata uchungu wa kuzaa, nami sijazaa,Wala sijalea vijana wa kiume wala wa kike.”*+   Kama wakati waliposikia habari kuhusu Misri,+Watu watateseka kwa sababu ya habari kuhusu Tiro.+   Vukeni mpaka Tarshishi! Ombolezeni kwa sauti, enyi wakaaji wa pwani!   Je, hili ndilo jiji lenu lililokuwa na furaha tangu kale, tangu nyakati zake za zamani? Miguu yake ilikuwa ikimpeleka nchi za mbali ili akae huko.   Ni nani ambaye ameamua jambo hili dhidi ya Tiro,Anayewavika watu mataji,Ambaye wafanyabiashara wake walikuwa wakuu,Ambaye wafanyabiashara wake waliheshimiwa duniani kote?+   Yehova wa majeshi mwenyewe ameamua hivi,Kutia unajisi kiburi chake kwenye uzuri wake wote,Kuwafedhehesha wote walioheshimiwa duniani kote.+ 10  Vuka nchi yako kama Mto Nile, ewe binti ya Tarshishi. Hakuna tena kiwanda cha meli.*+ 11  Ameunyoosha mkono wake juu ya bahari;Amezitikisa falme. Yehova ameamuru ngome za Foinike ziangamizwe.+ 12  Naye anasema: “Hutafurahi tena,+Ewe uliyekandamizwa, binti bikira wa Sidoni. Simama, vuka mpaka Kitimu.+ Hata huko hutapata utulivu.” 13  Tazama! Nchi ya Wakaldayo.+ Hawa ndio watu—haikuwa Ashuru+Walimfanya kuwa mahali pa wale wanaokaa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya kuzingira;Wameivua minara yake yenye ngome;+Na kumfanya awe magofu yanayoporomoka. 14  Ombolezeni kwa sauti, enyi meli za Tarshishi,Kwa maana ngome yenu imeharibiwa.+ 15  Siku hiyo Tiro litasahauliwa kwa miaka 70,+ sawa na muda wa* maisha ya mfalme mmoja. Mwishoni mwa miaka 70, Tiro litakuwa kama wimbo huu wa kahaba unavyosema: 16  “Chukua kinubi, lizunguke jiji, ewe kahaba uliyesahauliwa. Piga kinubi chako kwa ustadi;Imba nyimbo nyingi,Ili wakukumbuke.” 17  Mwishoni mwa miaka 70, Yehova atalikazia fikira Tiro, nalo litarudia malipo yake na kufanya ukahaba na falme zote za ulimwengu zilizo duniani. 18  Lakini faida yake na malipo yake yatakuwa kitu kitakatifu kwa Yehova. Hayatahifadhiwa wala kuwekwa akiba, kwa sababu malipo yake yatakuwa kwa ajili ya wale wanaokaa mbele za Yehova, ili wale na kushiba na kuvaa mavazi ya kifahari.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Mbegu.”
Yaani, kijito cha Mto Nile.
Tnn., “mabikira.”
Au labda, “bandari.”
Tnn., “siku za.”