Isaya 24:1-23

  • Yehova ataifanya nchi kuwa tupu (1-23)

    • Yehova ni Mfalme katika Sayuni (23)

24  Tazama! Yehova anaifanya nchi* kuwa tupu na ukiwa.+ Anaigeuza juu chini*+ na kuwatawanya wakaaji wake.+   Kila mtu atapatwa na hali ileile: Watu na pia kuhani,Mtumishi na bwana wake,Kijakazi na bimkubwa wake,Mnunuzi na muuzaji,Mkopeshaji na mkopaji,Anayedai na anayedaiwa.+   Nchi itafanywa kuwa tupu kabisa,Itaporwa kabisa,+Kwa maana Yehova amesema neno hilo.   Nchi inaomboleza;*+ inadhoofika. Nchi inayozaa inanyauka; inafifia. Watu mashuhuri wa nchi wananyauka.   Nchi imechafuliwa na wakaaji wake,+Kwa maana wamezivunja sheria,+Wamebadili amri,+Na kuvunja agano linalodumu.*+   Ndiyo sababu laana inaimeza nchi,+Na wakaaji wake wamehesabiwa kuwa na hatia. Ndiyo sababu wakaaji wa nchi wamepungua,Na watu wachache sana wamebaki.+   Divai mpya inaomboleza,* mzabibu unanyauka,+Na wote walio wachangamfu moyoni wanalia kwa uchungu.+   Furaha ya matari imekoma;Kelele za wanaosherehekea zimekoma;Sauti ya furaha ya kinubi imekoma.+   Wanakunywa divai bila wimbo,Na kileo ni kichungu kwa wale wanaokinywa. 10  Mji uliohamwa umebomolewa kabisa;+Kila nyumba imefungwa ili mtu yeyote asiweze kuingia. 11  Wanalilia divai barabarani. Kushangilia kote kumetoweka;Shangwe ya nchi imetokomea.+ 12  Jiji limeachwa likiwa magofu;Lango limevunjwavunjwa na kuwa rundo la kifusi.+ 13  Kwa maana hivi ndivyo itakavyokuwa katika nchi, miongoni mwa mataifa: Kama mzeituni unapopigwa,+Kama masalio yanavyokusanywa baada ya mavuno ya zabibu kuisha.+ 14  Watapaza sauti zao,Watapiga vigelegele kwa shangwe. Kutoka baharini* watatangaza ukuu wa Yehova.+ 15  Ndiyo sababu watamtukuza Yehova katika eneo la nuru;*+Katika visiwa vya bahari watalitukuza jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 16  Kutoka miisho ya dunia tunasikia nyimbo: “Utukufu* kwa Aliye Mwadilifu!”+ Lakini ninasema: “Ninadhoofika, ninadhoofika! Ole wangu! Wenye hila wametenda kwa hila;Kwa hila wenye hila wametenda kwa hila.”+ 17  Hofu na mashimo na mitego inakusubiri, mkaaji wa nchi.+ 18  Yeyote anayeikimbia sauti inayotia hofu ataanguka shimoni,Na yeyote anayetoka shimoni atanaswa na mtego.+ Kwa maana malango ya mafuriko yaliyo juu yatafunguliwa,Na misingi ya nchi itatetemeka. 19  Nchi imepasuka;Nchi imetikiswa;Nchi inafurukuta kwa fujo.+ 20  Nchi inapepesuka kama mlevi,Nayo inayumbayumba kama kibanda katika upepo. Makosa yake yameilemea sana,+Nayo itaanguka, hivi kwamba haitasimama tena. 21  Siku hiyo Yehova atalielekezea fikira zake jeshi lililo juuNa wafalme wa dunia walio duniani. 22  Nao watakusanywa pamojaKama wafungwa waliokusanywa shimoni,Nao watafungiwa katika gereza lililo chini ya ardhi;Baada ya siku nyingi watakaziwa uangalifu. 23  Mwezi mpevu utafedheheshwa,Na jua linalong’aa litaaibishwa,+Kwa maana Yehova wa majeshi amekuwa Mfalme+ katika Mlima Sayuni+ na YerusalemuAkiwa na utukufu mbele ya wazee wa watu wake.*+

Maelezo ya Chini

Au “Anausokota uso wa dunia.”
Au “dunia.”
Au labda, “inakauka.”
Au “la kale.”
Au labda, “inakauka.”
Au “magharibi.”
Au “mashariki.”
Au “Pambo.”
Tnn., “mbele ya wazee wake.”