Isaya 25:1-12

  • Baraka nyingi kwa watu wa Mungu (1-12)

    • Karamu ya Yehova ya divai bora (6)

    • Kifo hakitakuwepo tena (8)

25  Ee Yehova, wewe ni Mungu wangu. Ninakukweza, ninalisifu jina lako,Kwa maana umetenda mambo yanayostaajabisha,+Mambo yaliyokusudiwa* tangu nyakati za kale,+Kwa uaminifu,+ kwa kutegemeka.   Kwa maana umelifanya jiji kuwa rundo la mawe,Mji wenye ngome kuwa magofu yanayoporomoka. Mnara wa wageni si jiji tena;Halitajengwa tena kamwe.   Ndiyo sababu watu wenye nguvu watakutukuza;Jiji la mataifa yenye uonevu litakuogopa.+   Kwa maana umekuwa ngome kwa mtu wa hali ya chini,Ngome kwa maskini katika taabu yake,+Kimbilio kutokana na dhoruba ya mvua,Na kivuli wakati wa joto.+ Wakati mlipuko wa waonevu ni kama dhoruba ya mvua inayopiga ukuta,   Kama joto katika nchi iliyokauka,Unazikomesha ghasia za wageni. Kama joto linavyokomeshwa na kivuli cha wingu,Ndivyo wimbo wa waonevu unavyonyamazishwa.   Katika mlima huu+ Yehova wa majeshi atawaandalia watu wa mataifa yoteKaramu ya vyakula vinono,+Karamu ya divai bora,*Ya vyakula vinono vilivyojazwa urojorojo,Ya divai bora, iliyochujwa.   Katika mlima huu ataondoa* kifuniko kinachowafunika watu woteNa kifuniko kilichosokotwa* juu ya mataifa yote.   Atameza* kifo milele,+Na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atafuta kabisa machozi katika nyuso zote.+ Shutuma ya watu wake ataiondoa katika dunia yote,Kwa maana Yehova mwenyewe amesema hayo.   Siku hiyo watasema: “Tazama! Huyu ndiye Mungu wetu!+ Tumemtumaini yeye,+Naye atatuokoa.+ Huyu ndiye Yehova! Tumemtumaini yeye. Na tufurahi na kushangilia katika wokovu wake.”+ 10  Kwa maana mkono wa Yehova utatulia juu ya mlima huu,+Na Moabu itakanyagwa-kanyagwa mahali pake+Kama nyasi zinavyokanyagwa-kanyagwa na kuwa rundo la mbolea. 11  Atapigapiga mikono yake ndani yakeKama mwogeleaji anavyopigapiga mikono yake ili kuogelea,Naye atakishusha kiburi chake+Kwa mwendo stadi wa mikono yake. 12  Na jiji lenye ngome, pamoja na kuta zako ndefu za usalama,Ataziangusha chini;Atazibomoa na kuziangusha ardhini, mpaka mavumbini kabisa.

Maelezo ya Chini

Au “Mashauri ya.”
Au “divai iliyowekwa kwenye machicha.”
Tnn., “atameza.”
Au “shela iliyosokotwa.”
Au “Ataondoa.”