Isaya 27:1-13

  • Yehova amuua Lewiathani (1)

  • Wimbo kuhusu Israeli likiwa shamba la mizabibu (2-13)

27  Siku hiyo Yehova, akiwa na upanga wake mkali na mkubwa na wenye nguvu,+Atamwelekezea fikira Lewiathani,* yule nyoka anayenyiririka,Lewiathani, yule nyoka anayepindapinda,Naye atamuua mnyama mkubwa sana aliye baharini.   Siku hiyo mwimbieni hivi huyo mwanamke:* “Shamba la mizabibu la divai inayotoa povu!+   Mimi, Yehova, ninamlinda.+ Kila wakati ninammwagilia maji.+ Ninamlinda usiku na mchana,Ili mtu yeyote asimdhuru.+   Mimi sina ghadhabu.+ Ni nani atakayenikabili kwa vichaka vya miiba na magugu katika vita? Nitavikanyaga-kanyaga na kuvichoma moto vyote pamoja.   La sivyo, na ashikilie ngome yangu kwa nguvu,Na afanye amani pamoja nami;Acheni afanye amani pamoja nami.”   Siku zinazokuja Yakobo atatia mizizi,Israeli atachanua maua na kuchipuka,+Nao watajaza mazao katika nchi.+   Je, ni lazima apigwe kwa pigo la yule anayempiga? Au, je, ni lazima auawe kama watu wake walivyouawa?   Utashindana naye kwa mlio wa kushtua utakapokuwa ukimfukuza. Atamfukuza kwa mlipuko wake mkali katika siku ya upepo wa mashariki.+   Basi kwa njia hii uovu wa Yakobo utafunikwa,+Na haya ndiyo yatakayokuwa mazao kamili dhambi yake itakapoondolewa: Atayafanya mawe yote ya madhabahuYawe kama mawe ya chokaa yaliyopondwa na kuwa ungaunga,Na hakuna miti mitakatifu* au vinara vya uvumba vitakavyobaki.+ 10  Kwa maana jiji lenye ngome litaachwa tupu;Malisho yataachwa na kubaki kama nyika.+ Ndama atalisha humo na kulala humoNaye atakula matawi yake.+ 11  Vitawi vyake vitakapokauka,Wanawake watakuja kuvivunja,Na kuvitumia kuwasha moto. Kwa maana watu hawa hawana uelewaji.+ Ndiyo sababu Muumba wao hatawaonyesha rehema,Na Yule aliyewaumba hatawaonyesha kibali.+ 12  Siku hiyo Yehova atayapiga kabisa matunda kuanzia kijito kinachotiririka cha ule Mto* mpaka kwenye Korongo* la Misri,+ nanyi mtakusanywa mmoja baada ya mwingine, enyi watu wa Israeli.+ 13  Siku hiyo pembe kubwa itapigwa,+ na wale wanaoangamia katika nchi ya Ashuru+ na wale waliotawanywa katika nchi ya Misri+ watakuja na kumwinamia Yehova kwenye mlima mtakatifu huko Yerusalemu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Inaonekana ni Israeli, hapa anarejelewa kuwa mwanamke na kufananishwa na shamba la mizabibu.
Angalia Kamusi.
Yaani, Mto Efrati.
Angalia Kamusi.