Isaya 28:1-29

  • Ole kwa walevi wa Efraimu! (1-6)

  • Makuhani na manabii wa Yuda wapepesuka (7-13)

  • “Agano na Kifo” (14-22)

    • Jiwe la pembeni lenye thamani katika Sayuni (16)

    • Kazi ya Yehova isiyo ya kawaida (21)

  • Mfano kuhusu nidhamu ya Yehova yenye hekima (23-29)

28  Ole kwa taji* la kujionyesha* la walevi wa Efraimu+Na ua linalonyauka la uzuri wake wenye utukufu,Lililo kwenye kichwa cha bonde lenye rutuba la wale waliolemewa na divai!   Tazama! Yehova ana mtu mwenye nguvu na hodari. Kama dhoruba ya mvua ya mawe yenye mngurumo, dhoruba ya upepo inayoharibu,Kama dhoruba yenye mngurumo ya mafuriko yenye nguvu,Atalitupa chini kwa nguvu duniani.   Mataji ya kujionyesha* ya walevi wa EfraimuYatakanyagiwa chini kwa miguu.+   Na ua linalonyauka la uzuri wake wenye utukufuLililo juu ya kichwa cha bonde lenye rutuba,Litakuwa kama tini ya mapema kabla ya wakati wa kiangazi. Mtu anapoiona, huimeza mara tu inapokuwa mkononi mwake.  Siku hiyo Yehova wa majeshi atakuwa taji la utukufu na shada maridadi kwa watu wake waliobaki.+  Naye atakuwa roho ya haki kwa yule anayeketi katika hukumu na chanzo cha nguvu kwa wale wanaozuia mashambulizi langoni.+   Na hawa pia wanapotea njia kwa sababu ya divai;Wanapepesuka kwa sababu ya vileo vyao. Kuhani na nabii wanapotea njia kwa sababu ya kileo;Divai inawavuruga,Nao wanapepesuka kwa sababu ya kileo chao;Maono yao yanawafanya wapotee njia,Nao wanajikwaa wanapohukumu.+   Kwa maana meza zao zimejaa matapishi machafu—Yamejaa kila mahali.   Mtu atamfundisha nani ujuzi,Na mtu atamfafanulia nani ujumbe? Je, ni wale walioachishwa kunyonya hivi karibuni,Wale walioondolewa kwenye matiti hivi karibuni? 10  Kwa maana ni “amri baada ya amri, amri baada ya amri,Mstari kwa mstari, mstari kwa mstari,*+Hapa kidogo, pale kidogo.” 11  Kwa maana atazungumza na watu hawa kupitia watu wenye kigugumizi* na kwa lugha ya kigeni.+ 12  Alikuwa amewaambia: “Hapa ndipo mahali pa kupumzika. Yule aliyechoka na apumzike; hapa ndipo mahali pa kuburudika,” lakini walikataa kusikiliza.+ 13  Basi neno la Yehova litakuwa kwao: “Amri baada ya amri, amri baada ya amri,Mstari kwa mstari, mstari kwa mstari,*+Hapa kidogo, pale kidogo,” Ili wanapotembea,Wajikwae na kuanguka nyumaNa wavunjike na kunaswa na kukamatwa.+ 14  Basi sikieni neno la Yehova, ninyi mnaojigamba,Enyi watawala wa watu hawa wa Yerusalemu, 15  Kwa maana ninyi watu mnasema: “Tumefanya agano na Kifo,+Na tumefanya mapatano* na Kaburi.* Mafuriko makubwa ya ghafla yatakapopita,Hayatatufikia,Kwa maana tumeufanya uwongo kuwa kimbilio letuNasi tumejificha katika udanganyifu.”+ 16  Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazama, ninaweka jiwe lililojaribiwa liwe msingi katika Sayuni,+Jiwe la pembeni lenye thamani+ la msingi imara.+ Hakuna yeyote anayeonyesha imani atakayeshikwa na wasiwasi.+ 17  Nami nitaifanya haki kuwa kamba ya kupimia+Na uadilifu utakuwa kifaa cha kusawazishia;*+Na mvua ya mawe itafagilia mbali kimbilio la uwongo,Na maji yatafurika mahali pa kujificha. 18  Agano mlilofanya na Kifo litavunjwa,Na mapatano yenu na Kaburi* hayatasimama.+ Mafuriko makubwa ya ghafla yatakapopita,Yatawaponda ninyi. 19  Kila mara yanapopita,Yatawafagilia mbali;+Kwa maana yatapita asubuhi baada ya asubuhi,Mchana na usiku. Ni hofu tu itakayowafanya waelewe walichosikia.”* 20  Kwa maana kitanda ni kifupi sana mtu asiweze kujinyoosha juu yake,Na shuka iliyofumwa ni nyembamba sana isiweze kumfunika mtu. 21  Kwa maana Yehova atasimama kama katika Mlima Perasimu,Atainuka kama katika bonde lililo* karibu na Gibeoni,+Ili afanye tendo lake —tendo lake la ajabu—Na ili afanye kazi yake—kazi yake isiyo ya kawaida.+ 22  Sasa msidhihaki,+Ili vifungo vyenu visikazwe zaidi,Kwa maana nimesikia kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi,Kwamba maangamizi yamekusudiwa kuipata nchi yote.*+ 23  Tegeni sikio, muisikilize sauti yangu;Kazeni fikira na msikilize ninachosema. 24  Je, mkulima huendelea kulima mchana kutwa kabla hajapanda mbegu? Je, huendelea kuyagongagonga mabonge ya udongo na kusawazisha shamba lake?+ 25  Baada ya kusawazisha ardhi,Je, hatawanyi jira na kupanda bizari,Na je, hapandi ngano, mtama, na shayiri mahali pakeNa kusemethi+ kwenye mipaka? 26  Kwa maana Yeye humfundisha* njia inayofaa;Mungu wake humfundisha.+ 27  Kwa maana jira haisagwi kwa kifaa cha kupuria,+Na gurudumu la gari la kukokotwa halizungushwi juu ya bizari. Badala yake, jira hupigwa kwa fimbo,Na bizari kwa gongo. 28  Je, mtu huiponda nafaka ili apate mkate? Hapana, haendelei kuipura mfululizo;+Na anapozungusha gurudumu la gari lake la kukokotwa juu yake akiwa na farasi wake,Yeye haipondi.+ 29  Na haya pia yanatoka kwa Yehova wa majeshi,Ambaye shauri* lake linastaajabishaNa ambaye ametimiza mambo makuu.*+

Maelezo ya Chini

Inaonekana neno hili linarejelea jiji kuu, Samaria.
Au “majivuno; kiburi.”
Au “majivuno; kiburi.”
Au “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”
Tnn., “midomo yenye kigugumizi.”
Au “Kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia, kamba ya kupimia juu ya kamba ya kupimia.”
Au labda, “tumetekeleza maono.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “timazi.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au labda, “Watakapoelewa, watashikwa na hofu kubwa.”
Au “nchi tambarare ya chini iliyo.”
Au “kuipata dunia yote.”
Au “humtia nidhamu kwa; humwadhibu kwa.”
Au “kusudi.”
Au “ambaye hekima yake inayotumika ni kuu.”