Isaya 29:1-24

  • Ole kwa Arieli! (1-16)

    • Ibada ya midomo tu yashutumiwa (13)

  • Viziwi watasikia; na vipofu wataona (17-24)

29  “Ole kwa Arieli,* Arieli, jiji ambalo Daudi alipiga kambi ndani yake!+ Endelea mwaka baada ya mwaka;Mzunguko wa sherehe+ na uendelee.   Lakini nitaliletea taabu Arieli,+Na kutakuwa na kilio na maombolezo,+Nalo litakuwa kwangu kama jiko la madhabahu ya Mungu.+   Nitapiga kambi pande zote dhidi yako,Nami nitakuzingira kwa ngomeNa kujenga maboma dhidi yako.+   Utashushwa chini;Utazungumza kutoka ardhini,Na mambo utakayosema yatakuwa mnong’ono kwa sababu ya mavumbi. Sauti yako itatoka ardhini+Kama sauti ya mtu anayewasiliana na roho,Na maneno yako yatatoka mavumbini kama sauti ya ndege.   Umati wa maadui wako* utakuwa kama ungaunga laini,+Umati wa waonevu kama tu makapi yanayopeperuka.+ Na jambo hilo litatokea haraka, ghafla.+   Yehova wa majeshi atawakazia fikiraKwa mngurumo na tetemeko la ardhi na kelele kubwa,Kwa upepo wa dhoruba na tufani na miali ya moto unaoteketeza.”+   Kisha umati wa mataifa yote yanayopigana vita na Arieli+—Wale wote wanaopigana vita naye,Minara inayomzingira,Na wale wanaomsababishia taabu—Watakuwa kama ndoto, maono ya usiku.   Naam, itakuwa kama mtu aliye na njaa anayeota kwamba anakula,Lakini anaamka akiwa na njaa,*Na kama mtu mwenye kiu anayeota kwamba anakunywa,Lakini anaamka akiwa amechoka na akiwa na kiu.* Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa umati wa mataifa yoteYanayopigana vita dhidi ya Mlima Sayuni.+   Pigweni na butwaa na mshangae;+Jipofusheni na mpofushwe.+ Wamelewa, lakini si kwa divai;Wanapepesuka, lakini si kwa sababu ya kileo. 10  Kwa maana Yehova amewamwagia roho ya usingizi mzito;+Ameyafunga macho yenu, enyi manabii,+Naye amefunika vichwa vyenu, enyi waonaji.+ 11  Maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya kitabu ambacho kimefungwa kwa muhuri.+ Wakimpa mtu anayejua kusoma na kumwambia: “Tafadhali, kisome kwa sauti,” atasema: “Siwezi, kwa maana kimefungwa kwa muhuri.” 12  Na wakimpa kitabu hicho mtu asiyejua kusoma na kumwambia: “Tafadhali, kisome kitabu hiki,” atasema: “Sijui kusoma hata kidogo.” 13  Yehova anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyaoNao huniheshimu kwa midomo yao,+Lakini mioyo yao iko mbali sana nami;Na hofu yao kunielekea inategemea amri za wanadamu ambazo wamefundishwa.+ 14  Kwa hiyo, mimi Ndiye nitakayewatendea tena watu hawa mambo ya ajabu,+Maajabu juu ya maajabu;Na hekima ya watu wao wenye hekima itatoweka,Na uelewaji wa watu wao wenye busara utafichwa.”+ 15  Ole wao wanaojitahidi sana kumficha Yehova mipango yao.*+ Wanatenda matendo yao mahali penye giza,Huku wakisema: “Ni nani anayetuona? Ni nani anayejua kutuhusu?”+ 16  Jinsi mnavyopotosha mambo!* Je, mfinyanzi anapaswa kuonwa kuwa sawa na udongo?+ Je, kitu kilichotengenezwa kinapaswa kusema kuhusu yule aliyekitengeneza: “Hakunitengeneza?”+ Na je, kitu kilichotengenezwa kinasema kuhusu yule aliyekitengeneza: “Hana uelewaji”?+ 17  Katika muda mfupi, Lebanoni itageuzwa kuwa shamba la matunda,+Na shamba hilo la matunda litaonwa kuwa msitu.+ 18  Siku hiyo viziwi watasikia maneno ya kile kitabu,Na kutoka katika utusitusi na giza macho ya vipofu yataona.+ 19  Wapole watashangilia sana katika Yehova,Na maskini miongoni mwa watu watashangilia katika Mtakatifu wa Israeli.+ 20  Kwa maana mwonevu hatakuwapo tena,Anayejigamba ataangamia,Na wote wanaokaa macho ili kusababisha madhara wataangamizwa,+ 21  Wale ambao kwa neno la udanganyifu wanawafanya wengine wawe na hatia,Wanaotega mitego ili kumnasa mtetezi* katika lango la jiji,+Na wale ambao kwa mashtaka yasiyo na msingi humnyima haki mwadilifu.+ 22  Basi Yehova, aliyemkomboa Abrahamu,+ anaiambia hivi nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataona aibu tena,Na uso wake hautabadilika rangi tena.*+ 23  Kwa maana anapowaona watoto wake,Ambao ni kazi ya mikono yake, katikati yake,+Watalitakasa jina langu;Naam, watamtakasa Mtakatifu wa Yakobo,Nao watamwogopa Mungu wa Israeli.+ 24  Wale waliopotoka rohoni watapata uelewaji,Na wale wanaolalamika watakubali mafundisho.”

Maelezo ya Chini

Huenda jina hili linamaanisha “Jiko la Madhabahu ya Mungu,” inaelekea ni Yerusalemu.
Tnn., “wageni wako.”
Au “nafsi yake ikiwa tupu.”
Au “nafsi yake ikiwa imekauka.”
Au “shauri lao.”
Au “Jinsi mlivyopotoka!”
Tnn., “anayekaripia.”
Yaani, kwa sababu ya aibu na kukata tamaa.