Isaya 3:1-26

  • Viongozi wa Yuda wawapotosha watu (1-15)

  • Mabinti wa Sayuni wanaotongoza wahukumiwa (16-26)

3  Kwa maana tazama! Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,Anaondoa Yerusalemu na Yuda kila aina ya tegemeo na msaada,Tegemeo lote la kupata mkate na maji,+   Mwanamume hodari na shujaa,Mwamuzi na nabii,+ mbashiri* na mzee,   Mkuu wa 50,+ mwanamume mwenye kuheshimiwa, na mshauri,Mchawi hodari na mlozi stadi.+   Nitawafanya wavulana kuwa wakuu wao,Na watu wanaoyumbayumba* watawatawala.   Watu watakandamizana,Kila mmoja atamkandamiza mwenzake.+ Mvulana atamshambulia mwanamume mzee,Na mtu asiyeheshimiwa sana atamdharau yule anayeheshimiwa.+   Kila mmoja atamshika ndugu yake katika nyumba ya baba yake, na kusema: “Wewe una joho—uwe kamanda wetu. Lisimamie rundo hili la magofu.”   Lakini siku hiyo atakataa akisema: “Mimi sitakuwa mfunga-majeraha* wenu;Sina chakula wala nguo katika nyumba yangu. Msiniweke kuwa kamanda juu ya watu.”   Kwa maana watu wa Yerusalemu wamejikwaa,Na watu wa Yuda wameanguka,Kwa sababu wanampinga Yehova kwa maneno na matendo;Wanatenda kwa ukaidi mbele za uwepo wake mtukufu.*+   Hali ya nyuso zao inatoa ushahidi dhidi yao,Nazo zinatangaza dhambi yao kama Sodoma;+Hawajaribu kuificha. Ole wao,* kwa maana wanajiletea msiba! 10  Waambie waadilifu kwamba mambo yatawaendea vema;Watathawabishwa kwa yale wanayotenda.*+ 11  Ole wake mtu mwovu! Atapatwa na msiba,Atatendewa yale ambayo mikono yake imetenda! 12  Na kuhusu watu wangu, wasimamizi wao wa kazi wanawatesa,Na wanawake huwatawala. Watu wangu, viongozi wenu wanawafanya mtangetange,Nao wanavuruga mwelekeo wa njia zenu.+ 13  Yehova anachukua nafasi yake ili kutoa mashtaka;Anasimama ili kuwahukumu watu. 14  Yehova atawahukumu wazee na wakuu wa watu wake. “Mmeliteketeza kabisa shamba la mizabibu,Na vitu mlivyowaibia maskini vimo ndani ya nyumba zenu.+ 15  Mnawezaje kuwaponda watu wanguNa kusaga nyuso za maskini mavumbini?”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi. 16  Yehova anasema: “Kwa sababu mabinti wa Sayuni ni wenye majivuno,Nao wanatembea wakiwa wameinua vichwa vyao juu,*Wakipepesa-pepesa macho kwa utongozi, wakitembea kwa hatua fupifupi,Wakiwa na vikuku vinavyotoa milio kwenye vifundo vya miguu, 17  Yehova pia atawapiga mabinti wa Sayuni kwa upele kichwani,Na Yehova atafunua wazi paji la uso wao.+ 18  Siku hiyo Yehova ataondoa umaridadi wa bangili zao,Tepe za kichwani na mapambo yenye umbo la mwezi mwandamo,+ 19  Herini,* vikuku, na shela, 20  Vitambaa vya kichwani, mafurungu, na mavazi ya kifuani,*Chupa za marashi* na hirizi,* 21  Pete za vidole na pete za puani, 22  Kanzu za sherehe, kanzu fupi za nje, majoho, na mikoba, 23  Vioo vya mkononi+ na mavazi ya kitani,*Vilemba na shela. 24  “Badala ya mafuta ya zeri,+ kutakuwa na harufu ya uozo;Badala ya mshipi, kamba;Badala ya mtindo maridadi wa nywele, upara;+Badala ya vazi lenye thamani, nguo ya magunia;+Na alama iliyotiwa mwilini badala ya urembo. 25  Wanaume wako watauawa kwa upanga,Na wanaume wako hodari watauawa vitani.+ 26  Milango yake italia na kuomboleza,+Naye ataketi ardhini katika hali ya ukiwa.”+

Maelezo ya Chini

Au “mwaguzi.”
Au “wasio na msimamo.”
Au “tabibu.”
Tnn., “machoni pa utukufu wake.”
Au “Ole wa nafsi zao.”
Tnn., “Watakula matunda ya matendo yao.”
Tnn., “wakiwa wamerefusha shingo (koo) zao.”
Au “Kigwe.”
Au “ukumbuu.”
Tnn., “nyumba za nafsi.”
Au “kauri zinazovuma zinazotumiwa kama mapambo.”
Au “nguo za ndani.”