Isaya 30:1-33

  • Msaada wa Misri ni bure kabisa (1-7)

  • Watu wakataa ujumbe wa kinabii (8-14)

  • Mtakuwa na nguvu mkiendelea kuwa na tumaini (15-17)

  • Yehova awaonyesha kibali watu wake (18-26)

    • Yehova, Mfundishaji Mkuu (20)

    • “Hii ndiyo njia” (21)

  • Yehova atatekeleza hukumu dhidi ya Ashuru (27-33)

30  “Ole wao wana wakaidi,”+ asema Yehova,“Wanaotekeleza mipango ambayo si yangu,+Wanaofanya miungano,* lakini si kwa roho yangu,Ili kuongeza dhambi juu ya dhambi.   Wanashuka kwenda Misri+ bila kuniomba ushauri,*+Ili kupata usalama chini ya ulinzi wa Farao*Na kupata kimbilio katika kivuli cha Misri!   Lakini ulinzi wa Farao utawaletea aibu,Na kukimbilia katika kivuli cha Misri kutawaletea fedheha.+   Kwa maana wakuu wake wako Soani,+Na wajumbe wake wamefika Hanesi.   Wote wataaibishwaNa watu ambao hawawezi kuwanufaisha,Ambao hawawapi msaada wowote wala manufaa yoyote,Isipokuwa aibu na fedheha.”+  Tangazo dhidi ya wanyama wa kusini: Katika nchi ya taabu na hali ngumu,Ya simba, simba anayenguruma,Ya nyoka kipiri na nyoka wa moto arukaye,*Wanabeba mali zao juu ya migongo ya pundaNa mizigo yao juu ya nundu za ngamia. Lakini vitu hivyo havitawanufaisha watu.   Kwa maana msaada wa Misri haufai kitu.+ Kwa hiyo nimemwita huyu: “Rahabu,+ anayeketi tuli.”   “Sasa nenda, iandike juu ya bamba mbele yao,Na uiandike katika kitabu,+Ili itumike siku ya baadayeKama ushahidi wa kudumu.+   Kwa maana wao ni watu waasi,+ wana wadanganyifu,+Wana wasiotaka kusikia sheria* ya Yehova.+ 10  Wanawaambia waonaji, ‘Msione,’ Na wale wanaopata maono, ‘Msituambie maono ya kweli.+ Tuambieni mambo yanayotupendeza;* oneni maono ya udanganyifu.+ 11  Tokeni kwenye njia; ondokeni kwenye kijia. Acheni kumweka Mtakatifu wa Israeli mbele yetu.’”+ 12  Kwa hiyo Mtakatifu wa Israeli anasema hivi: “Kwa kuwa mnalikataa neno hili+Nanyi mnatumaini ulaghai na udanganyifuNa mnayategemea mambo hayo,+ 13  Kwa hiyo uovu huu utakuwa kwenu kama ukuta uliobomoka,Kama ukuta mrefu uliofura unaokaribia kuanguka. Utaanguka ghafla, mara moja. 14  Utavunjwa kama mtungi mkubwa wa mfinyanzi,Utapondwapondwa kabisa hivi kwamba hakuna kigae chochote kitakachobakiIli kitumiwe kukusanya moto jikoniAu kuchota maji kutoka kwenye kidimbwi.”* 15  Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mtakatifu wa Israeli, anasema hivi: “Mkirudi kwangu na kupumzika, mtaokolewa;Mtakuwa na nguvu mkiendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.”+ Lakini hamkutaka.+ 16  Badala yake, mlisema: “Hapana, tutakimbia kwa farasi!” Basi mtakimbia. “Nasi tutapanda farasi wenye mbio!”+ Kwa hiyo wale wanaowafuatia watakuwa na mbio.+ 17  Watu elfu moja watatetemeka wakitishwa na mtu mmoja;+Mtakapotishwa na watu watano mtakimbiaMpaka mbaki kama mlingoti juu ya mlima,Kama nguzo ya ishara juu ya kilima.+ 18  Lakini Yehova anangoja kwa subira* ili kuwaonyesha kibali,+Naye atainuka ili kuwaonyesha rehema.+ Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki.+ Wenye furaha ni wote wanaoendelea kumtarajia.*+ 19  Watu watakapokaa Sayuni, Yerusalemu,+ hamtalia kamwe.+ Kwa hakika atawaonyesha kibali mara tu atakaposikia kilio chenu cha kuomba msaada; atawajibu mara tu atakaposikia kilio chenu.+ 20  Ingawa Yehova atawapa taabu kama mkate na ukandamizaji kama maji,+ Mfundishaji wako Mkuu hatajificha tena, nawe utamwona Mfundishaji wako Mkuu+ kwa macho yako mwenyewe. 21  Na masikio yako mwenyewe yatasikia neno nyuma yako likisema, “Hii ndiyo njia.+ Tembeeni ndani yake,” ikiwa mtaenda upande wa kulia au mtaenda upande wa kushoto.+ 22  Nanyi mtaitia unajisi fedha inayofunika sanamu zenu za kuchongwa na dhahabu inayofunika sanamu zenu za chuma.*+ Mtazitupa mbali kama kitambaa cha hedhi na kuziambia, “Potelea mbali!”*+ 23  Naye ataleta mvua kwa ajili ya mbegu mtakazopanda ardhini,+ na chakula* kitakachotoka ardhini kitakuwa kingi na chenye lishe.*+ Siku hiyo mifugo yenu italisha katika malisho makubwa.+ 24  Na ng’ombe na punda wanaolima mashamba watakula chakula cha mifugo kilichokolezwa kwa mboga chungu, kilichopepetwa kwa sepetu na kwa uma. 25  Na juu ya kila mlima mrefu na juu ya kila kilima kirefu kutakuwa na vijito na mitaro ya maji,+ katika siku ya mauaji makubwa wakati ambapo minara itaanguka. 26  Na mwangaza wa mwezi mpevu utakuwa kama mwangaza wa jua; na mwangaza wa jua utaongezeka mara saba,+ kama mwangaza wa siku saba, katika siku ambayo Yehova atalifunga jeraha* la watu wake+ na kuponya kidonda kikubwa kilichosababishwa na pigo alilowaletea.+ 27  Tazama! Jina la Yehova linakuja kutoka mbali sana,Likiwaka kwa hasira yake na kwa mawingu mazito. Midomo yake imejaa ghadhabu,Na ulimi wake ni kama moto unaoteketeza.+ 28  Roho* yake ni kama mto unaofurika unaofika mpaka shingoni,Ili kuyatikisa mataifa katika chujio la maangamizi;*Na mataifa yatakuwa na lijamu katika mataya yao+ ambayo inawapotosha. 29  Lakini wimbo wenu utakuwa kama wimbo unaoimbwa usikuMnapojitayarisha* kwa ajili ya sherehe,+Na moyo wenu utashangilia kama mtuAnayetembea na* filimbiAkielekea kwenye mlima wa Yehova, kwa Mwamba wa Israeli.+ 30  Yehova atafanya sauti yake kuu+ isikiweNaye ataonyesha mkono wake+ unaposhuka kwa hasira kali,+Ukiwa na mwali wa moto unaoteketeza,+Tufani ya mvua na dhoruba yenye ngurumo+ na mvua ya mawe.+ 31  Kwa maana kwa sababu ya sauti ya Yehova, Ashuru itashikwa na hofu;+Ataipiga kwa fimbo.+ 32  Na kila pigo la fimbo yake ya adhabuAmbalo Yehova ataleta juu ya AshuruLitaambatana na matari na vinubi+Anapoutikisa mkono wake dhidi yao vitani.+ 33  Kwa maana tayari Tofethi*+ yake imetayarishwa;Pia imetayarishwa kwa ajili ya mfalme.+ Amefanya rundo la kuni liwe na kina kirefu na liwe pana,Kwa wingi wa moto na kuni. Pumzi ya Yehova, kama mto wa kiberiti,Itaiwasha moto.

Maelezo ya Chini

Tnn., “wanaomwaga sadaka ya kinywaji,” inaonekana inarejelea kufanya mapatano.
Tnn., “katika ngome ya Farao.”
Au “bila kutafuta ushauri kutoka katika kinywa changu.”
Au “nyoka mwenye sumu anayerukaruka.”
Au “mafundisho.”
Tnn., “mambo laini.”
Au labda, “tangi la maji.”
Au “anaendelea kuwatarajia.”
Au “wanaomngoja kwa hamu.”
Au “sanamu za kuyeyushwa.”
Au labda, “na kuziita uchafu.”
Tnn., “mnono na wenye mafuta.”
Au “mkate.”
Au “jeraha la kuvunjika.”
Tnn., “chujio la ubatili.”
Au “Pumzi.”
Au “mnapojitakasa.”
Au “akisikia sauti ya.”
Hapa neno “Tofethi” linatumiwa kurejelea mahali pa mfano pa kuteketezea vitu, panafananisha maangamizi.