Isaya 31:1-9

  • Msaada wa kweli unatoka kwa Mungu, hautoki kwa wanadamu (1-9)

    • Farasi wa Misri ni nyama tu (3)

31  Ole wao wanaoshuka kwenda Misri kutafuta msaada,+Wanaotegemea farasi,+Wanaotumaini magari ya vita kwa sababu ni mengi,Na farasi wa vita* kwa sababu wana nguvu. Lakini hawamtegemei Mtakatifu wa Israeli,Na hawamtafuti Yehova.   Lakini yeye pia ana hekima na ataleta msiba,Naye hatayabatilisha maneno yake. Atainuka dhidi ya nyumba ya watenda maovuNa dhidi ya wale wanaowasaidia wakosaji.+   Hata hivyo, Wamisri ni wanadamu tu, wao si Mungu;Farasi wao ni nyama wala si roho.+ Yehova atakapounyoosha mkono wake,Yeyote atakayetoa msaada atajikwaaNa yeyote atakayesaidiwa ataanguka;Wote wataangamia wakati mmoja.   Kwa maana Yehova ameniambia hivi: “Kama simba anavyonguruma, mwanasimba mwenye nguvu,* juu ya mawindo yake,Kundi lote la wachungaji linapokusanywa kupigana naye,Naye haogopi sauti yaoAu kutishwa na kelele zao,Ndivyo Yehova wa majeshi atakavyoshuka ili kupigana vitaJuu ya Mlima Sayuni na juu ya kilima chake.   Kama ndege wanaoshuka kwa ghafla, ndivyo Yehova wa majeshi atakavyolilinda Yerusalemu.+ Atalilinda na kuliokoa. Atalihifadhi na kuliokoa.”  “Rudini kwa Yule ambaye mmemwasi bila aibu, enyi watu wa Israeli.+  Kwa maana siku hiyo kila mmoja ataikataa miungu yake ya ubatili ya fedha na miungu yake ya dhahabu ambayo haina thamani, ambayo mikono yenu wenyewe ilitenda dhambi kwa kuitengeneza.   Na Mwashuru atauawa kwa upanga, lakini si wa mwanadamu;+Na upanga, usio wa mwanadamu, utamwangamiza. Atakimbia kwa sababu ya upanga,Na wanaume wake vijana watalazimishwa kufanya kazi za kulazimishwa.   Jabali lake litapitilia mbali kwa sababu ya woga mwingi,Na wakuu wake wataogopa kwa sababu ya nguzo ya ishara,” asema Yehova,Ambaye nuru yake iko* Sayuni na ambaye tanuru lake liko Yerusalemu.

Maelezo ya Chini

Au “wapanda farasi.”
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Au “moto wake uko.”