Isaya 32:1-20

  • Mfalme na wakuu watatawala kwa haki ya kweli  (1-8)

  • Wanawake wanaopuuza mambo waonywa (9-14)

  • Kumiminwa kwa roho kwaleta baraka (15-20)

32  Tazama! Mfalme+ atatawala kwa uadilifu,+Na wakuu watatawala kwa haki.   Na kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujificha* kutokana na upepo,Na mahali pa kujisitiri* kutokana na dhoruba ya mvua,Kama vijito vya maji katika nchi isiyo na maji,+Kama kivuli cha jabali kubwa katika nchi iliyokauka.   Kisha macho ya wale wanaoona hayatafungwa tena,Na masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.   Moyo wa wale wanaofanya mambo bila kufikiri utatafakari ujuzi,Na ulimi wa wenye kigugumizi utazungumza kwa ufasaha na waziwazi.+   Mtu mpumbavu hataitwa tena mkarimu,Na mtu asiye na msimamo hataitwa mheshimiwa;   Kwa maana mtu mpumbavu atazungumza upumbavu,Na moyo wake utatunga mambo yanayodhuru,+Ili kuendeleza uasi imani* na kusema mambo mapotovu dhidi ya Yehova,Kusababisha mwenye njaa akae njaaNa kumnyima mwenye kiu maji ya kunywa.   Mipango ya mtu asiye na msimamo ni mibaya;+Anaendeleza mwenendo wa aibuIli kumwangamiza kwa uwongo mtu anayeteseka,+Hata maskini anaposema jambo lililo sawa.   Lakini mtu mkarimu ana nia ya ukarimu,Naye huendelea kutenda matendo ya ukarimu.*   “Enyi wanawake mnaopuuza mambo, simameni msikilize sauti yangu! Enyi mabinti msiojali,+ sikilizeni ninachosema! 10  Katika muda unaozidi mwaka mmoja hivi, ninyi msiojali mtatetemeka,Kwa sababu hakuna matunda yatakayokuwa yamekusanywa mavuno ya zabibu yatakapokwisha.+ 11  Tetemekeni, ninyi wanawake mnaopuuza mambo! Tetemekeni, ninyi msiojali! Vueni nguo mbaki uchi,Na mvae nguo za magunia viunoni.+ 12  Pigeni vifua vyenu kwa kuombolezaKwa sababu ya mashamba yanayotamanika na mzabibu unaozaa matunda mengi. 13  Kwa maana ardhi ya watu wangu itafunikwa kwa miiba na michongoma;Itazifunika nyumba zote zenye furaha,Naam, jiji la shangwe.+ 14  Kwa maana mnara wenye ngome umeachwa;Jiji lenye kelele limeachwa.+ Ofeli+ na mnara wa mlinzi vimebaki ukiwa daima,Mahali panapopendwa na punda wa mwituni,Malisho ya mifugo,+ 15  Mpaka roho itakapomiminwa juu yetu kutoka juu,+Na nyika iwe shamba la matunda,Na shamba la matunda lionwe kuwa msitu.+ 16  Kisha haki itakaa nyikani,Na uadilifu utakaa katika shamba la matunda.+ 17  Matokeo ya uadilifu wa kweli yatakuwa amani,+Na mazao ya uadilifu wa kweli yatakuwa utulivu wa kudumu na usalama wa kudumu.+ 18  Watu wangu watakaa katika makao ya kudumu yenye amani,Katika makao salama na mahali pa kupumzika penye utulivu.+ 19  Lakini mvua ya mawe itauangusha chini msitu,Na jiji litabomolewa kabisa. 20  Wenye furaha ni ninyi mnaopanda mbegu kando ya maji yote,Mnaowatoa nje* ng’ombe dume na punda.”+

Maelezo ya Chini

Au “kibanda cha kujificha.”
Au “mahali pa kukimbilia.”
Au “kutenda kwa kutomwogopa Mungu.”
Au “matendo mema.”
Au “Mnaowafungua.”