Isaya 33:1-24

  • Hukumu na tumaini kwa waadilifu (1-24)

    • Yehova ni Mwamuzi, Mpaji-sheria, na Mfalme (22)

    • Hakuna atakayesema: “Mimi ni mgonjwa” (24)

33  Ole wako wewe, mwangamizaji ambaye hujaangamizwa;+Ewe msaliti ambaye hujasalitiwa! Utakapomaliza kuangamiza, utaangamizwa.+ Utakapomaliza kusaliti, utasalitiwa.   Ee Yehova, tuonyeshe kibali.+ Tunakutumaini wewe. Uwe mkono wetu*+ kila asubuhi,Naam, wokovu wetu wakati wa taabu.+   Watu wanakimbia kwa sababu ya sauti ya ghasia. Unapoinuka, mataifa yanatawanyika.+   Kama nzige wanaokula sana wanavyokusanyika, ndivyo nyara zako zitakavyokusanywa;Watu watazikimbilia kama makundi ya nzige.   Yehova atakwezwa,Kwa maana anakaa katika vilele vilivyo juu. Ataijaza Sayuni haki na uadilifu.   Yeye ndiye tegemeo imara la nyakati zako;Wingi wa wokovu,+ hekima, ujuzi, na kumwogopa Yehova+—Hiyo ndiyo hazina yake.   Tazama! Mashujaa wao wanalia kwa sauti barabarani;Wajumbe wa amani wanalia kwa uchungu.   Barabara kuu zimebaki tupu;Hakuna mtu anayesafiri kwenye vijia. Amelivunja* agano;Ameyakataa majiji;Hamheshimu mwanadamu anayeweza kufa.+   Nchi inaomboleza* na kunyauka kabisa. Lebanoni imeaibika;+ imeoza. Sharoni imekuwa kama jangwa,Na Bashani na Karmeli zinapukutisha majani yake.+ 10  “Sasa nitainuka,” asema Yehova,“Sasa nitajikweza mwenyewe;+Sasa nitajitukuza mwenyewe. 11  Mnachukua mimba ya majani yaliyokauka na kuzaa majani makavu. Roho yenu wenyewe itawateketeza kama moto.+ 12  Na watu watakuwa kama chokaa iliyoteketea. Watawashwa moto kama miiba iliyokatwa.+ 13  Ninyi mlio mbali sana, sikieni jambo nitakalofanya! Nanyi mlio karibu, tambueni uwezo wangu! 14  Watenda dhambi walio Sayuni wanaogopa;+Waasi imani wanatetemeka: ‘Ni nani kati yetu anayeweza kuishi mahali palipo na moto unaoteketeza?+ Ni nani kati yetu anayeweza kuishi na miale isiyoweza kuzimwa?’ 15  Yule anayetembea katika uadilifu wa daima,+Anayesema mambo manyoofu,+Anayekataa faida isiyo ya haki, ya ulaghai,Ambaye mikono yake inakataa rushwa badala ya kuichukua kwa nguvu,+Anayeziba sikio lake ili lisisikilize mazungumzo ya umwagaji wa damu,Na anayefunga macho yake ili yasione maovu 16  Atakaa katika vilele;Kimbilio lake salama* litakuwa katika ngome zilizo kwenye miamba,Atapewa mkate wake,Naye maji yake hayataisha kamwe.”+ 17  Macho yako yatamwona mfalme katika fahari yake;Yataona nchi iliyo mbali sana. 18  Moyoni mwako utakumbuka* jambo linaloogopesha: “Yuko wapi mwandishi? Yuko wapi yule aliyepima ushuru?+ Yuko wapi yule aliyeihesabu minara?” 19  Hutawaona tena watu wenye dharau,Watu ambao lugha yao ni ngumu sana kueleweka,*Ambao huwezi kuelewa ulimi wao wenye kigugumizi.+ 20  Tazama Sayuni, jiji la sherehe zetu!+ Macho yako yataona Yerusalemu kama makao matulivu,Hema ambalo halitaondolewa.+ Vigingi vyake vya mahema havitang’olewa kamwe,Na hakuna kamba yake yoyote itakayokatwa. 21  Lakini huko, yule Aliye Mkuu, Yehova,Atakuwa kwetu eneo la mito, la mifereji mipana,Ambako hakuna kundi la merikebu litakaloenda hukoNa hakuna meli za kifahari zitakazopita huko. 22  Kwa maana Yehova ni Mwamuzi wetu,+Yehova ni Mpaji-sheria wetu,+Yehova ni Mfalme wetu;+Yeye Ndiye atakayetuokoa.+ 23  Kamba zako zitalegea na kuning’inia;Haziwezi kushika mlingoti usimame imara wala kutandaza tanga. Wakati huo nyara nyingi zitagawanywa;Hata mtu mlemavu atachukua nyara nyingi.+ 24  Na hakuna mkaaji* atakayesema: “Mimi ni mgonjwa.”+ Watu wanaokaa katika nchi watasamehewa dhambi yao.+

Maelezo ya Chini

Au “nguvu zetu.”
Yaani, adui.
Au labda, “inakauka.”
Au “kilele salama.”
Au “utatafakari.”
Tnn., “ina kina kirefu isiweze kueleweka.”
Au “mwenyeji.”