Isaya 38:1-22

  • Hezekia ashikwa na ugonjwa kisha apona (1-22)

    • Wimbo wa shukrani (10-20)

38  Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa karibu afe.+ Nabii Isaya+ mwana wa Amozi akaja na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Wape maagizo watu wa nyumba yako, kwa maana utakufa; hutapona.’”+  Ndipo Hezekia akaugeuza uso wake kuelekea ukutani, akaanza kusali hivi kwa Yehova:  “Nakusihi, Ee Yehova, tafadhali, kumbuka+ jinsi ambavyo nimetembea mbele zako kwa uaminifu na kwa moyo kamili,+ nami nimetenda mambo mema machoni pako.” Kisha Hezekia akaanza kulia sana na kububujikwa na machozi.  Kisha neno la Yehova likamjia Isaya, likisema:  “Rudi ukamwambie Hezekia,+ ‘Yehova, Mungu wa Daudi babu yako anasema hivi: “Nimesikia sala yako.+ Nimeona machozi yako.+ Sasa ninakuongezea miaka 15 ya kuishi,*+  nami nitakuokoa wewe na jiji hili kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru, nami nitalilinda jiji hili.+  Hii ndiyo ishara kutoka kwa Yehova itakayokuonyesha kwamba Yehova atatimiza neno alilosema:+  Nitafanya kivuli cha jua kinachoshuka kwenye ngazi* ya Ahazi kirudi nyuma hatua kumi.”’”+ Basi jua likarudi nyuma hatua kumi kwenye ngazi ambayo tayari lilikuwa limeshuka.  Haya ni maandishi ya* Mfalme Hezekia wa Yuda, aliposhikwa na ugonjwa na kupona ugonjwa wake. 10  Nilisema: “Katikati ya maisha yanguLazima niingie katika malango ya Kaburi.* Nitanyimwa miaka yangu iliyobaki.” 11  Nilisema: “Sitamwona Yah,* Yah katika nchi ya walio hai.+ Sitawaona tena wanadamuNitakapokuwa pamoja na wakaaji wa mahali ambapo kila kitu hukoma. 12  Makao yangu yameng’olewa na kuondolewa kwangu+Kama hema la mchungaji. Nimeukunja uhai wangu kama mfumaji wa nguo;Ananikata kabisa kama nyuzi za mtande. Kuanzia mapambazuko mpaka usiku unaendelea kunimaliza.+ 13  Nimejituliza mpaka asubuhi. Kama simba, anaendelea kuivunja mifupa yangu yote;Kuanzia mapambazuko mpaka usiku unaendelea kunimaliza.+ 14  Ninaendelea kulia kama mbayuwayu au teleka;*+Ninaendelea kulia kama njiwa.+ Macho yangu yanatazama kileleni kwa uchovu:+ ‘Ee Yehova, ninataabika sana;Uwe msaada wangu!’*+ 15  Niseme nini? Amezungumza nami na kutenda. Nitatembea kwa unyenyekevu* miaka yangu yoteKwa sababu ya mateso yangu makali.* 16  ‘Ee Yehova, kila mwanadamu anaishi kwa mambo haya,*Na katika mambo hayo kuna uhai wa roho yangu. Utaniponya na kunihifadhi hai.+ 17  Tazama! Badala ya amani, nilikuwa na uchungu mwingi;Lakini kwa sababu ulinipenda sana,*Uliniokoa kutokana na shimo la maangamizi.+ Umezitupa dhambi zangu zote nyuma ya mgongo wako.*+ 18  Kwa maana Kaburi* haliwezi kukutukuza,+Kifo hakiwezi kukusifu.+ Wale wanaoshuka shimoni hawawezi kuutumaini uaminifu wako.+ 19  Walio hai, walio hai wanaweza kukusifu,Kama ninavyoweza leo hii. Baba anaweza kuwapa wanawe ujuzi kuhusu uaminifu wako.+ 20  Ee Yehova, niokoe,Nasi tutapiga nyimbo zangu kwa vinanda+Siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yehova.’”+ 21  Ndipo Isaya akasema: “Leteni keki ya tini kavu zilizoshinikizwa mlipake jipu hilo, ili apone.”+ 22  Hezekia alikuwa ameuliza: “Ni ishara gani itakayonionyesha kwamba nitapanda kwenda katika nyumba ya Yehova?”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “katika siku zako.”
Labda hatua hizo za ngazi zilitumiwa kuhesabu muda, kama saa ya kivuli.
Au “Huu ni utungo wa.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “Uwe dhamana yangu.”
Au labda, “korongo.”
Au “kimyakimya.”
Au “uchungu wa nafsi yangu.”
Yaani, maneno na matendo ya Mungu.
Au “Umeziondoa dhambi zangu zote kutoka mbele ya macho yako.”
Au “uliipenda sana nafsi yangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.