Isaya 41:1-29

  • Mshindi kutoka mashariki (1-7)

  • Israeli achaguliwa kuwa mtumishi wa Mungu (8-20)

    • “Rafiki yangu Abrahamu” (8)

  • Miungu mingine yajaribiwa (21-29)

41  “Nisikilizeni mkiwa kimya,* enyi visiwa;Mataifa na yapate nguvu tena. Na yakaribie; kisha yaongee.+ Na tukutane pamoja kwenye hukumu.   Ni nani amemwinua mtu kutoka mashariki,*+Akimwita katika uadilifu aje miguuni Pake,*Ili amkabidhi mataifaNa kumfanya awatiishe wafalme?+ Ambaye anawafanya wawe mavumbi mbele ya upanga wake,Kama majani makavu yanayopeperushwa na upepo mbele ya upinde wake?   Anawafuatia, anapita bila kuzuiwaKwenye njia ambazo miguu yake haijawahi kupita.   Ni nani ametenda na kufanya jambo hili,Kuviita vizazi tangu mwanzoni? Mimi, Yehova, Ndiye wa Kwanza;+Na kwa wale wa mwisho mimi ni yuleyule.”+   Visiwa vimeona hivyo na kuogopa. Miisho ya dunia ilianza kutetemeka. Wanakaribia na kuja mbele.   Kila mmoja anamsaidia mwenzakeNa kumwambia ndugu yake: “Uwe imara.”   Kwa hiyo fundi anamwimarisha mfua chuma;+Yule anayelainisha kwa nyundo ya chumaAnamwimarisha yule agongaye kwenye fuawe. Anasema hivi kuhusu lehemu: “Ni nzuri.” Kisha inapigiliwa misumari ili isianguke.   “Lakini wewe ni mtumishi wangu, Ee Israeli,+Wewe niliyekuchagua, Ee Yakobo,+Uzao wa* rafiki yangu Abrahamu,+   Wewe, niliyekuchukua kutoka kwenye miisho ya dunia,+Na wewe, niliyekuita kutoka sehemu zake za mbali zaidi. Nilikuambia, ‘Wewe ni mtumishi wangu;+Nimekuchagua wewe; sijakukataa.+ 10  Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe.+ Usihangaike, kwa maana mimi ni Mungu wako.+ Nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia,+Nitakushika kwelikweli kwa mkono wangu wa kuume wa uadilifu.’ 11  Tazama! Wale wote wanaowaka hasira dhidi yako wataaibishwa na kufedheheshwa.+ Wale wanaopigana nawe watafanywa kuwa si kitu na wataangamia.+ 12  Utawatafuta watu wanaopambana nawe, lakini hutawapata;Watu wanaopigana nawe watakuwa kama kitu kisichokuwepo, watakuwa si kitu kabisa.+ 13  Kwa maana mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika kwa nguvu mkono wako wa kulia,Mimi ninayekuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’+ 14  Usiogope, wewe mnyoo* Yakobo,+Ninyi watu wa Israeli, nitawasaidia,” asema Yehova, Mkombozi wenu,+ Mtakatifu wa Israeli. 15  “Tazama! Nimekufanya uwe kifaa cha kupuria,+Kifaa kipya cha kupuria chenye meno yenye makali pande mbili. Utaikanyaga-kanyaga milima na kuipondapondaNa kuvifanya vilima viwe kama makapi. 16  Utawapepeta,Na upepo utawapeperusha mbali;Dhoruba ya upepo itawatawanya. Utashangilia katika Yehova,+Nawe utajigamba katika Mtakatifu wa Israeli.”+ 17  “Wenye uhitaji na maskini wanatafuta maji, lakini hayapo. Ulimi wao umekauka kwa sababu ya kiu.+ Mimi, Yehova, nitawajibu.+ Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.+ 18  Nitafanya mito itiririke kwenye vilima visivyo na kitu+Na chemchemi katika mabonde tambarare.+ Nitaigeuza nyika kuwa dimbwi la maji lenye mateteNa nchi isiyo na maji kuwa chemchemi za maji.+ 19  Nitapanda mwerezi jangwani,Mshita na mhadasi na msonobari,+Nitapanda mberoshi katika jangwa tambarare,Pamoja na mtidhari na mvinje,+ 20  Ili watu wote waone na kujuaWakaze fikira na kuelewaKwamba mkono wa Yehova umetenda hayo,Na Mtakatifu wa Israeli ameliumba jambo hilo.”+ 21  “Leteni kesi yenu,” asema Yehova. “Toeni hoja zenu,” asema Mfalme wa Yakobo. 22  “Leteni ushahidi na mtuambie mambo yatakayotendeka. Tuambieni kuhusu mambo ya zamani,*Ili tuyatafakari* na kujua matokeo yakeAu mtutangazie mambo yanayokuja.+ 23  Tuambieni mambo yatakayotokea wakati ujao,Ili tujue kwamba ninyi ni miungu.+ Naam, fanyeni jambo, zuri au baya,Ili tushangae tutakapoliona.+ 24  Tazameni! Ninyi ni kitu kisichokuwepo,Na mafanikio yenu si kitu.+ Mtu yeyote anayewachagua ninyi anachukiza.+ 25  Nimemwinua mtu kutoka kaskazini, naye atakuja,+Kutoka upande wa mapambazuko ya jua,*+ atakayeliitia jina langu. Atawakanyaga-kanyaga watawala* kana kwamba wao ni udongo,+Kama mfinyanzi anayeukanyaga-kanyaga udongo wenye maji. 26  Ni nani aliyesema jambo hilo tangu mwanzoni, ili tulijue,Au kutoka nyakati za zamani, ili tuseme, ‘Yeye anasema kweli’?+ Kwa kweli, hakuna mtu aliyelitangaza! Hakuna mtu aliyelisema! Hakuna mtu aliyesikia lolote kutoka kwenu!”+ 27  Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni: “Tazama! Wako hapa!”+ Na kwa Yerusalemu nitamtuma mtu anayepeleka habari njema.+ 28  Lakini niliendelea kutazama, na hapakuwa na mtu;Hakukuwa na mtu yeyote kati yao ambaye angetoa ushauri. Nami niliendelea kuwaomba wanijibu. 29  Tazameni! Wote ni udanganyifu.* Kazi zao si kitu. Sanamu zao za chuma* ni upepo na ubatili.+

Maelezo ya Chini

Au “Nyamazeni mbele zangu.”
Au “upande wa mapambazuko ya jua.”
Yaani, ili amtumikie Yeye.
Tnn., “Mbegu ya.”
Yaani, mtu wa hali ya chini asiye na ulinzi.
Tnn., “kwanza.”
Au “tuyaelekezee moyo wetu.”
Au “mashariki.”
Au “watawala wasaidizi.”
Au “kitu kisichokuwepo.”
Au “Sanamu zao za kuyeyushwa.”